Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii adhimu. Kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunifikisha hapa salama nikiwa mzima wa afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuchangia hii bajeti ambayo iko mbele yetu, nimshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya. Katika kipindi kifupi sana ameweza kusimamia mambo ya barabara, mambo ya umeme, mambo ya reli, makusanyo mazuri vilevile katika ununuzi wa ndege. Kwa kweli, Mheshimiwa Rais anapaswa kupongezwa kwa kazi kubwa anayofanya na sisi tunamuombea aendelee na speed hiyo, sisi Wabunge tuko nyuma yake kwa nguvu zote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye bajeti hii Wizara ya Fedha kwanza nimpongeze ndugu yangu Mheshimiwa Waziri Mpango na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji. Kwa kweli, bajeti ya safari hii ni nzuri, ni bajeti ya matumaini na mimi ni imani yangu kwamba bajeti hii kwa mwaka huu itaipa nafasi kubwa katika nchi yetu na kwa mwananchi wa kawaida, vilevile itampunguzia mzigo mkubwa sana. Nikupongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa bajeti nzuri pamoja na msaidizi wako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze hawa TRA kwa ukusanyaji wa mapato. TRA kwa kweli safari hii wamekuwa watu wastaarabu sana katika kuzungumza na wafanyabiashara tofauti na miaka ya nyuma, nina matumaini makubwa ikiwa TRA watakwenda hivi kukaa na wafanyabiashara tukafika mahali ikawa ni win-win situation basi, mapato ya nchi yataongezeka sana. Wasichukuliwe wafanyabiashara kama ni maadui katika nchi, lakini wafanyabisahara kwa kweli wana nafasi kubwa sana kuliingizia Taifa mapato. Kwa hiyo, niwapongeze sana wenzangu wa TRA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naunga mkono ongezeko la shilingi 40 kwenye mafuta. Hii itatusaidia sana katika kutatua matatizo yetu ya maji na umeme, lakini si vibaya Mheshimiwa Waziri ikiwa tutaongeza airport tax japo kwa dola tano kwa sababu, hizi dola tano hizi wasafiri wamekuwa wengi na itatuingizia Taifa pesa nyingi sana. airport tax ambayo haimuumizi mwananchi wa chini kwa sababu, wanaosafiri wote Alhamdulillah ni watu wanaojiweza ndio maana wanaruka. Kwa hiyo, mimi hilo nilikuwa nataka kuliongezea kwamba, kama kutaongezwa na aiport tax dola tano sio vibaya, kwa sababu nchi itapata pesa nyingi na tutapata kufanya mambo yetu mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu umenipa dakika tano ninakushukuru. Mimi naunga hoja ya bajeti hii asilimia mia moja. Inshallah... (Makofi)