Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Kaka yangu Waziri wa Fedha pamoja na Naibu wake. Lakini kwa namna ya kipekee naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Jemedari wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya kwenye Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu nijielekeze kwenye vipaumbele viwili. Kwanza Mchuchuma na Liganga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkataba wa Mchuchuma na Liganga ulisainiwa mwaka 2012, sasa hivi ni takribani miaka mitano hakuna jambo lolote linaloendelea katika lile eneo. Kwa hiyo, nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa atueleze sababu zipi ambazo zimesababisha mpaka leo mradi ule haujaanza kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili katika eneo hilo, nataka Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa atuambie kwa nini Serikali mpaka leo haijaanza kujenga transmission line ya kutoka Makambako - Songea mpaka Ngaka? Hakuna umeme rahisi baada ya umeme wa maji kama umeme wa makaa ya mawe na nchi nyingi duniani ikiwemo Marekani, South Africa wanategemea umeme wa makaa ya mawe. Sasa ni jambo la kushangaza sana sisi kwenye eneo ambalo tuna makaa ya mawe ya kutosha tunashindwa kutumia facility iliyopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu wa Sweden kupitia SIDA Grants walikuwa tayari kuisaidia Serikali hii dola za Kimarekani milioni 64 kwa ajili ya kujenga transmission line ambayo ingeweza ku-produce megawati 120 yenye kilowati 220 ambayo ingekuwa source kubwa ya kuwasaidia watu wa Kusini pamoja na maeneo mengine. Umeme huu ungekuwa ni rahisi kuliko umeme mwingine automatically ungeenda kupunguza cost of production na ungefanya bidhaa ambazo tuna-produce ndani ya nchi hii ziwe cheaper zaidi. Kwa hiyo, namuomba sana Mheshimiwa Waziri, atakapokuja hapa atuambie kwa nini mradi huu haujaanza? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo jingine ambalo napenda kuchangia ni suala la Kurasini Hub. Mwaka 2012 tulienda Beijing tukasaini ule mkataba wa Kurasini Hubs na sisi kama Serikali ya Tanzania tulipewa majukumu, miongoni mwa majukumu tuliyopewa ilikuwa ni kukubali kulipa fidia watu wa Kurasini wote na hilo jambo tumelifanya, lakini toka mwaka huo mpaka sasa hivi hatujaanza. Kama Kurasini Hub ingekuwa ime-take place tungeweza kuteka biashara za nchi zote za East and Central Africa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa njia moja au nyingine tunashindwa kufanya shughuli za msingi ambazo zingelisaidia Taifa hili kupata mapato. Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa atuambie nikwa nini mpaka leo Kurasini Logisitic Hub haijaanza kufanya kazi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba Mheshimiwa Waziri aangalie sana vijana wake wa TRA kuhusu tarrifs na export, hizi kwa njia moja au nyingine zinasababisha sisi tupoteze biashara. Kulikuwa kuna Wakongo, Wamalawi na Burundi wengi waliokuwa wanakuja kununua bidhaa hapa nchini, lakini cha kusikitisha unaweza kukuta colgate ya gramu 1,000 na colgate ya gramu 250 zinatajwa katika tarrif moja. Matokeo yake inasababisha gharama za ushuru kwa wafanyabiashara wa hapa nchini zinakuwa kubwa, matokeo yake wanashindwa kuziuza kwa watu wa nchi za nje na wale wanahama kwenda kule. Ule ushuru ungekuwa cheap automatically tungeweza kuuza sana na tungepata kodi nyingine kupitia VAT.

Kwa hiyo, tufanye utaratibu tuhakikishe tunaangalia kwenye hili eneo kusudi tuweze kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo kwa namna ya kipekee naomba nichukue fursa hii kuunga mkono hoja.