Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa. Awali ya yote, nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha sote salama na kuendelea kulifanya Taifa letu kuwa salama na tulivu pamoja na misukosuko yote ambayo tumekuwa tukikabiliana nayo. (Makofi)
Vilevile nitumie nafasi hii kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Nzega kwa heshima walionipa ya kukichagua Chama cha Mapinduzi na kunichagua mimi kuwa Mbunge wao wa Jimbo la Nzega. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa hotuba aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge. Wataalamu wengi wa utawala wametoa criteria na quality za viongozi ambapo viongozi wa aina mbalimbali na Taifa hili kwa muda mrefu tumekuwa tukiomba kupata kiongozi ambaye ni transformational wa kuweza kutusaidia kui-transform society yetu na kuipeleka mbele. Nitumie nafasi hii ku-copy sehemu ya presentation aliyowahi kuifanya Dkt. Mpango akielezea sifa za kiongozi ambaye ni transformational. Moja ya sifa ya kiongozi ambaye ni transformational ni kiongozi uncompromising katika jambo analoliamini na lenye maslahi ya watu wake. Katika presentation ya Dkt. Mpango alitumia neno moja no gain without pain. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuchangia hotuba ya Rais, wenzetu walisema kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano amekuwa akivunja na kukanyaga sheria katika maamuzi ambayo amekuwa akiyafanya sasa. Mimi niseme, moja ya tatizo kubwa linalokabili Taifa letu ni uwepo wa sheria zinazoruhusu watu kuzitumia kuliibia Taifa hili. Sheria hizi zimewapa fursa watendaji wengi kuiibia nchi yetu. Mmeona wizi mwingi ambao umefanyika katika Taifa hili umehifadhiwa katika sheria. Tunahitaji kiongozi mwenye sifa ya Rais Magufuli kuzikanyaga hizi sheria ili tuweze kupambana na wizi wa nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, yalisemwa hapa na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge kwamba Rais amepeleka fedha katika sekta ya elimu bila kuleta mini-budget. Swali tu la mantiki, tulitaka watoto wasiende shule tusubiri Bunge la Februari tuwaleteeni mini-budget mpitishe? Tumeambiwa barabara ya Morocco, fedha zilizokuwa allocated kwa ajili ya sherehe za uhuru zimepelekwa pale bila kufanyika utaratibu wa kumpata mkandarasi. Walitaka tutumie miezi sita kumpata mkandarasi ili barabara ile ijengwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambieni, jambo la kwanza ambalo tunatakiwa kulifanya sasa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kaka yangu Mwakyembe kaeni mzipitie hizi sheria hovyo mzilete kwenye Bunge la Aprili tuzifute, Sheria ya PPRA ni wizi mtupu. Leo kujenga tundu moja la choo mkandarasi anakuletea bajeti ya shilingi milioni 25 na imefuata taratibu za evaluation na process zote, kile choo kina nini? Kwa hiyo, nimuunge mkono Mheshimiwa Rais katika hatua anazochukua, Taifa letu liko kwenye dharura, linahitaji aina hii ya leadership ili tuweze kwenda mbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, nijikite sasa kwenye hotuba ya Rais. Tumeona political will ya Rais ya kutaka kulifanya Taifa hili kuwa la viwanda lakini yapo mambo ya msingi ambayo tunatakiwa tuyafanye kama Waheshimiwa Wabunge na Watanzania. Jambo la kwanza ambalo naiomba Wizara ya Fedha, nia ya Rais haiwezi kufanikiwa kama Wizara ya Fedha haitakaa chini na kufanya strategic decision ni maeneo gani ya viwanda tunataka kuwekeza ambayo yatakuwa na matokeo chanya kwa watu wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nashauri na ningeomba Waheshimiwa Wabunge na Wizara ya Fedha tukubaliane, nchi hii tunasema ni nchi ya wakulima ni kweli. Hata hivyo, ukitazama takwimu uchangiaji wa sekta ya kilimo katika pato la Taifa kwa mwaka 2014 umeshuka kwa asilimia kumi na nne. Aidha, Watanzania waliokuwa wamejiajiri katika sekta ya kilimo mwaka 2012 walikuwa asilimia 76 leo ni asilimia 66 maana yake ni kwamba Watanzania wamehama kwenye sekta ya kilimo wameenda kwenye sekta zingine. Hii inamaanisha nini? Maana yake tukifanya maamuzi yasiyokuwa sahihi katika uwekezaji wa viwanda, tukaenda katika maeneo ambayo hayatakuwa na matokeo chanya kwa watu wetu wengi, umaskini wa Watanzania utaendelea kuwepo hata tukiwa na viwanda vyingi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili kwenye suala la viwanda, hatuwezi kufanikiwa kwenye suala la viwanda kama hatujamsaidia Mheshimiwa Profesa Ndalichako katika eneo la elimu kuhakikisha kwamba tunawekeza fedha nyingi kwenye sekta ya elimu ili ku-improve skills za vijana wetu waweze kwenda kusaidia uzalishaji katika viwanda. Tusipohakikisha kwamba elimu yetu inatoa majibu sahihi kuweza kufikia lengo la viwanda, matokeo yake ajira nyingi za viwanda hazitachukuliwa na Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba Waheshimiwa Wabunge, tukaipa kipaumbele Wizara ya Elimu na kuiagiza Wizara ya Elimu ije na mpango mkakati wa namna gani technical schools zetu kama vyuo vya VETA vitatoa wanafunzi ili waweze kwenda kuajiriwa katika sekta ya viwanda vya Agro Based Industries. Hivi ndivyo viwanda ambavyo vitatuondolea matatizo. Textiles Industries, hivi ndivyo viwanda ambavyo vitaajiri vijana wetu wengi. Tunaotoka katika maeneo ambayo pamba inalimwa mmeona wakulima wamepoteza matumaini. Tukiongeza jitihada katika viwanda vya textiles, mazao ya pamba yakawa processed katika viwanda vyetu, wakulima wetu watakuwa na moyo wa kufanya kazi, watakuwa na soko la uhakika na hii itasaidia sana nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunazungumzia viwanda lakini hakuna jambo la msingi kama infrastructure ya reli. Nimeangalia Mpango wa Maendeleo wa mwaka mmoja, Waziri amesema tutajenga reli ya standard gauge. Habari ya kujengwa reli imekuwepo kabla mimi sijaja hapa Bungeni, nimekuwa nikiisikia, niwaombe Wabunge, bajeti itakayokuja kama haitatuambia imetenga fedha kiasi gani za kujenga reli ya standard gauge, tusikubali kuunga mkono bajeti hiyo. Kama bajeti ya Serikali itakuja bila suala la reli kupewa kipaumbele cha kutosha tusikubali kuunga mkono.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumzia suala la uzalishaji wa viwanda, tumsaidie Mheshimiwa Profesa Muhongo. Leo 41% ya uzalishaji wetu wa umeme wanazalisha Independent Power Producers na tunanunua umeme kwa shilingi ngapi, ni ghali. Kwa hiyo, tuisaidie Serikali uzalishaji wa gesi uweze kutusaidia kama nchi. Tufanye maamuzi ya lazima, haya mambo ya 100% owned by private, anakuja anatumia gesi yetu, sisi hatu-own stake katika huu uzalishaji, ameenda kukopa nje hatumsimamii alikokopa, bado tutaununua umeme kwa bei kubwa. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Bashe muda wako umekwisha.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais. (Makofi)