Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante sana kwa kunipatia nafasi hii, ninakushukuru sana. Nianze kwa kum-quote Profesa mmoja wa Kenya ambaye anaitwa Patrice Lumumba, yeye alisema kwamba; “Magufuli is the real deal.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wangu kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akiifanya kiasi ambacho amewafanya mpaka baadhi ya watu wameanza kuchanganyikiwa, wanahisi kama Mheshimiwa Magufuli amekaa miaka saba, wakati ndio kwanza ana mwaka mmoja na nusu. Na ninapenda kuwaambia kwamba hii ni mpaka 2025. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa ambayo leo hii nimeamua kusimama hapa, kwanza ni utendaji wake, lakini vilevile ni jinsi ambavyo ameshughulikia suala hili la makinikia. Suala hili la makinikia wananchi wangu, kwa mimi ambaye natokea Mkoa wa Shinyanga, wamenituma wanasema kwamba, katika vitu ambavyo utazungumza usiache kuelezea furaha kubwa tuliyokuwanayo sisi kwa jinsi ambavyo Rais ameweza kutusaidia, walau kuonyesha njia ambayo tunajua sasa tutafaidika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nimesoma magazeti, kuna gazeti moja nikasoma limeandika kwamba, kuna utafiti wa TWAWEZA, wanasema kwamba sijui umaarufu wa Mheshimiwa Rais Magufuli umeporomoka kwa sababu anapendwa na watu wa kada ya chini! Mimi nilikuwa nataka niseme jambo moja, wala hajakosea kwa sababu asilimia kubwa ya Watanzania ni maskini wale ambao ndio wanachukua asilimia kubwa asilimia 70. Kwa hiyo, kwa Rais kukubalika kwa watu asilimia 70 na kupingwa au kutokukubalika kwa ile asilimia 30 mimi naona ni jambo zuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa mtu yeyote, kiongozi yeyote ambaye unajua unachokifanya hiki ndicho ambacho kinatakiwa kufanyika. Wewe hutakiwi upendwe na watu wachache ambao tena wengi mara nyingi wanakuwa ni mafisadi au wanakuwa ni watu ambao umewagusa kwa namna moja au nyingine, inatakiwa wewe upendwe na wale watu ambao ndio wengi.

Kwa hiyo, kwa Rais kukubaliwa na watu wa kada hii ya chini ndio hasa kitu ambacho tunakiunga mkono na kwa kweli, ndio kinaonyesha kwambam Rais wetu yuko imara sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mara ya mwisho wakati nachangia…

TAARIFA ...

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu yeyote mwenye akili timamu lazima apokee hiyo taarifa. Ni ukweli kabisa utafiti umefanyika between mwezi wa tatu na mwezi tano na ndiyo kipindi masuala ya vyeti fake yamesemwa masuala ya mafisadi yamesemwa kwahiyo hawa wenzetu hii asilimia 30 tunawajua ni wakina nani na hawa wa Makinikia na wao pia tunawajua na wenyewe pia wanajijua na wengine wako humu humu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwenye kuzungumzia suala hili la makinikia mimi nina ushauri mdogo. Mtanisamehe sauti yangu kidogo inakwaruza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala hili la Makinikia mimi nilikuwa na ushauri kidogo biashara hii ni biashara kubwa sana, ninampongeza sana sana Profesa Mruma na pamoja na Profesa Osoro. Profesa Mruma nimekuwa naye kwenye board ya Williamson Diamond kwa kipindi cha miaka kama nane, kwa hiyo biashara hii ya diamond ninaifahamu kwa kiwango cha chake. Biashara hii inaitwa holding business. Biashara hii hata ikija kutokea duniani leo hii dhahabu zote zikaisha almasi zote zitakaisha kwenye mashino yetu aidha Afrika au sehemu nyingine yoyote. Of course sana sana ni Afrika. Biashara hii bado itaendelea kufanyika kutokana na nature ya hii biashara jinsi ilivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu nilikuwa naomba kushauri kwamba amekuja huyu CEO wa Barrick, lakini inatakiwa sisi kama Tanzania tukae naye. Mimi ambacho naomba kushauri naomba kwamba timu yetu ya Tanzania tufanye upembuzi mzuri sana wa watu wa kukaa na huyu mtu. Hawa wenzetu ni wazoefu sana wa hizi biashara ni tycoon wa hizi biashara, ni biashara ambazo zina pesa nyingi sana lakini wenzetu wame-deal na hivi vitu maeneo mbalimbali kupita kiasi zaidi yetu sisi. Kwahiyo, lazima kwenye kuchagua watu wa kukaa nao meza moja lazima tuchague watu ambao vichwa vyao viko sawa sawa kikweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye suala hili la makinikia mimi nilikuwa naomba kuuliza Wizara ya Fedha, miaka ya nyuma BOT walitoa wayver kwa makampuni yote ya madini ambayo wanachimba hapa Tanzania ambayo yanatoka nje kwamba mnaruhusiwa kuweka pesa zenu nje. Ile wayver ilitolewa wakati ule Gavana akiwa Dkt. Balali mpaka sasa hivi wayver ile haijarudishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu kubwa ya haya makampuni walisema kwamba sisi tunataka tuweke pesa zetu huku nje kwa sababu hapa Tanzania hakuna mabenki ambayo ni international, lakini vile vile na sisi ambao ni wafanyabiashara ya hizi biashara. Sisi mikopo yetu tunaitoa huko nje. Sasa hawa watu sasa hivi international bank zipo nyingi hapa Tanzania. Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa kweli mimi nitaomba jibu hapo baadaye utakapokuja kuhitimisha uje utuambie ni sababu zipi zilizofanya mpaka leo hiki kitu kimekuwa kimya hakisemwi kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu kama tunavyoelewa kwamba pesa hizi zilikuwa zinawekwa hapa Tanzania, sisi Tanzania hapa tumekuwa tunalalamika bei ya dola imekuwa kubwa wafanyakabiashara wanalalamika. Pesa hizi zikiwa zinawekwa hapa tutafaidika hata mzunguko wetu wa pesa, urari wa biashara utaweza kuonekana na mzunguko wetu wa pesa itakuwa ni rahisi zaidi kwa sababu hata dola itachuka at least ita-stabilize vizuri kuliko ilivyo sasa hivi. Nilikuwa naomba jambo hili liweze kuliangalia kwa macho makali zaidi na kwa kweli ulifanyie kazi kwa haraka sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine ambalo nilikuwa nataka nizungumzie. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha pamoja na Naibu wake dada yangu Dkt. Ashantu wanafanya kazi nzuri sana ni watu ambao siyo waongeaji sana lakini kwa kazi wanapiga vizuri sana. Mmefanyaka kazi nzuri sana bajeti ni nzuri sana kusema za ukweli. Huwezi kuwa mtu mwenye akili timamu ukasema bajeti hii ina matatizo ina dosari za hapa na pale kwa sababu ni ile tu kwamba hatuwezi kumaliza matatizo yote kwa mara moja. Lakini hatuwezi kusema kwamba bajeti hii mbaya, bajeti hii ni nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba kwenye suala zima la kuwasaidia wajasiriamali wadogo tusiishie tu kwenye masuala ya administrative pamoja na facilitation, mimi nilikuwa naomba tu tujikite zaidi kwenye jinsi ya kuwasaidia hawa wajasiriamali wadogo.

Mheshimiwa Waziri nilikuwa naomba kukuambia ujaribu kumulika pale Airport - TRA ya kwako. Kuna matatizo makubwa sana wakati tumekaa tunazungumzia habari za kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, Mheshimiwa Waziri wafanya biashara hawa wadogo wako akina mama, wako vijana wanaangaika wanakwenda nchi mbalimbali kuja kuleta bidhaa. Wanafanyabiashara ambazo mitaji yao ni dola 20000/30000 siyo pesa nyingi, lakini mtu analeta mzigo akifika pale airport anapata usumbufu wa hatari. Inakuwa inamkatisha mtu tamaa mpaka anaona kwa nini nimeanza kwenda. Anapata visa anamaliza anatoka anakenda huko nje kwenda kufanya hiyo biashara lakini akiingia hapa Tanzania anapata usumbufu kupita kiasi na rushwa pale imezidi. Mimi nakuambia kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mwisho ambalo nilikuwa nataka nilizungumzie, Wizara ya Afya, uchumi ni afya, Wizara ya Afya nilikuwa naomba nitoe wazo Bunge hili liunde Kamati ya kushughulikia suala zima la Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali. Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeoza, haifai na kama ikiwezekana Mheshimiwa Rais na angekuwepo hapa leo Mheshimiwa Waziri Mkuu, nadhani ningempa message kwa sababu yeye alijua jinsi ya kuzungumzia angeifuta kabisa. Ofisi ya Mkemia Mkuu inatakiwa ifanye control ya chemicals ambazo zinaingia Tanzania jambo ambalo hawafanyi hata kidogo. Kuna kampuni inaitwa TECHNO imeiingiza chemical kampuni moja tu. Imeingiza chemical ambazo ni nyingi wanaulizwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali hawajui hata idadi ya Chemicals ambazo zimeingizwa hapa Tanzania. Kemikali hizi zinatumika hospitalini, kwenye mashule yetu, wanafunzi wanakwenda kufundishwa kwa ma-chemicals ambazo zime expire, wanafunzi wanakwenda kufundishwa kwa chemicals ambazo nyingine siyo zenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitu kama hivi tukiendelea kukaa tukivinyamazia, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara kwa Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali akakutana na hili jambo linatia aibu nasikitika tu kwamba sikupata nafasi ya kulizungumza kwa urefu wakati wa Wizara Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.