Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ahmed Juma Ngwali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ziwani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. AHMED JUMA NGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na nianze na hoja yangu kwenye ukurasa wa 47 kitabu cha bajeti kwenye maneno madogo sana ambayo nataka kuzungumzia kuhusu Electronic Revenue Collection System; ambayo mfumo mpya ulianzishwa hivi karibuni, mfumo ambao kimsingi nakubaliana nao na nakubaliana nao kwa sababu kabla ya uanzishwaji wa mfumo huu makampuni ya simu yalikuwa yakikusanya fedha wenyewe baadae wakiwaita Serikali ndio wakiaanza kugawana mapato. Pamoja na kuwepo mfumo wa TTMS lakini mfumo wa TTMS ulikuwa haukusanyi kodi, hiyo ndio kasoro Mheshimiwa Zungu alipigia kelele sana ulikuwa haukusanyi kodi.

Kwa hiyo, sasa kilichoendelea nikwamba makampuni ya simu yalikuwa na uwezo mkubwa sana wakufanya ambavyo wanajua dhidi ya kodi ya Serikali. Na hasa napongeza hata kwa upande wa Zanzibar sasa kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiingiza vocha maana yake kodi ya Serikali pale pale inachukuliwa na kwa upande wa Zanzibar ukiingaza vocha kodi inachukuliwa pale pale inakwenda ZRB, kwa hivyo kiufupi nikukubaliana na Serikali kwenye jambo hili ni jambo zuri na linafaa kuungwa kuungwa mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nilikuwa nazungumzia suala la michezo ya bahati nasibu. Michezo ya bahati nasibu sasa hivi pamoja nakuleta negative impact katika jamii, lakini imekuwa ni sehemu ambayo kama Serikali watakaa pamoja kuifanyia kazi ni sehemu ambayo inapatikana kodi kubwa sana kwa Serikali. Kwa mfano, sheria iliyokuweko sasa inawapa Gaming Board kukusanya kodi, lakini kwa mchezo ambao ulivyoendelea lazima tubadilishe sheria, TRA kwa sababu wanamtandao mpana wao ndio waweze kukusanya kodi kila maeneo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri na habari hii unaijua vizuri, nadhani katika bajeti ijayo kwa sababu nafikiri tumechelewa katika bajeti ijayo lazima tubadilishe sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ile GGR manaake ile Gambling Gross Gambling Revenue ambayo tunakusanya kwenye betting peke yake tuna- charge asilimia sita, asilimia sita ambayo kwa mujibu wa makadirio ya Gaming Board kwa mwaka huu kwa mwaka 2016/2017 basi tungeliweza kukusanya shilingi bilioni 24. Lakini kwa mujibu wa makadirio ya mwaka 2017/2018 tutaweza kukusanya shilingi bilioni 39 nukta kadhaa, lakini tukiongeza kutoka kwenye sport betting asilimia sita kwenda asilimia 20 pekeyake tutaweza kukusanya shilingi bilioni 37 kwa hivyo hilo ni eneo moja. Lakini katika casino pia tuna-charge sasa hivi katika pato ghafi la kamari tuna-charge asilimia 15, lakini tukiongeza tukifika asilima 20 manaa yake tutaweza kukusanya shilingi bilioni 20. Kwa hiyo hapo bado hatujaenda katika zile za slot machine; slot machine kwa sasa tunachaji shilingi 32,000 kwa slot machine moja.

Kwa hivyo lakini tukipeleka kwenye 60,000 tunaweza ku-charge shilingi bilioni 2.7 pia tunaweza kwenye upande wa competation yaani lottering Mheshimiwa Waziri wa Fedha tunapoteza fedha, lazima tubadilishe sheria. Sheria ile tubadilishe ili isiwe inamilikiwa na mtu mmoja, tuongeze watu ambao wataweza kuendesha lottery ya Taifa ili tuweze kukusanya shilingi bilioni 10 na inawezekana kabisa.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri mimi ningeomba katika bajeti ijayo jambo hili tukae jumla ya fedha ambazo tutazikusanya itafika shilingi bilioni 69 naa na kama TRA watakusanya vizuri basi tunaweza kufika hata shilingi bilioni 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu tuzungumzie suala la medical tourism, sports tourism na beach tourism. Medical tourism wenzetu wa Kenya wametenga kwa pesa za Tanzania shilingi bilioni 22. Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametuonesha njia, tunayo ile Jakaya Kikwete Cardiac Institute tunapokea wageni mbalimbali ambao wanakuja pale sasa kupata matibabu. Lakini ina double impact ya kwanza tunapata fedha moja kwa moja kutoka kwa wageni. lakini wageni wale wakifika pia wanatumia fedha kwa ajili ya mawasiliano, wanasafiri, wanakula tunapata pesa nyingi kutoka kwao. Lakini kinachosikitisha mpaka sasa Serikali haikutenga fedha yoyote katika eneo hili jambo ambalo tukilinganisha na trains za standard gauge pamoja na ndege ambazo Serikali wanazinunua tukiweza kuimarisha sekta ya afya katika nchi yetu na mzunguko wa nchi zilizotuzunguka hiyo itaweza kutusaidia sana na itaisaidia Serikali kuongeza mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia Mheshimiwa Waziri tunachokizungumza hapa ni kwamba hata sasa, hata hawa wataalamu ambao wanaendesha hiyo Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete bado hatuna wa kutosha kutoka nchini kwetu tunaagiza watu mbalimbali wanakuja kufanya, hatujawekeza fedha kuwasomesha watu wetu katika eneo hilo. Kwa hivyo mimi niiombe Serikali kwamba katika jambo hili ijitahidi inavyopaswa lakini iweze kuwekeza fedha kwa mfano, Tanzania sasa hivi kwa mujibu wa takwimu za karibuni wanasafirisha Watanzania wanaokwenda India kutibiwa karibu watu 23,000. Ukitizama Kenya wanakwenda karibu watu 40,000; ukitizama Sudani watu 8,000; ukitizama Nigeria karibu watu 34,000 wanakwenda, sasa tungeifanya sisi tungepata fedha nyingi sana. ili Mheshimiwa Waziri nikushauri kwamba bajeti ijayo uhakikishe kwamba unatenga fedha katika eneo hili kwa ajili ya maslahi ya Tanzania na watu wetu na afya itaboreka nina uhakika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie tena suala la blue economy, Ethopia hawana hata bahari, bahari yao ndogo sana kule pembeni pembeni lakini wana meli commercial ship 18 Tanzania tumezungwa na bahari hatuna commercial ship hata moja. Mizigo yote yanapita baharini asiimia 95 hili ni eneo situ kwamba kila kitu kifanywe na Serikali lakini Serikali itakapoonyesha dhamira basi stakeholders watakuja kufanya hiyo shughuli si lazima mfanye ninyi, kwa hivyo eneo hilo nalo pia lina tatizo.

Mheshimiwa Waziri aqua culture yaani ufugaji wa samaki. Uganda wanatumia ziwa Victoria pekeyake aqua culture inachangia pato la Taifa asilimia 7.5 tuna maziwa tuna Victoria, Tanganyika, tuna Nyasa tuna na bahari yaani acro culture hatuchangii hata shilingi 100 katika Pato la Taifa haiwezekani, lazima Mheshimiwa Waziri tukubali maeneo mengine ya kuweka fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la mwisho Mheshimiwa Waziri ambalo niliseme ni kuhusu mambo ya madini; na mimi kwenye madini ni seme kidogo ili na mie niweke kumbukumbu sahihi. Usalama wa Taifa wako wapi? Mali zote hizo zilizoibiwa siku zote Usalama wa Taifa wako wapi? Na nini jukumu la usalama wa Taifa katika nchi? Ikiwa Usalama wa Taifa wameacha mambo yote haya yameharibika kiasi hiki, hata sisi pia siwanaweza kutuuza?

Kwa hiyo, nafikiri usalama wa Taifa wajitathimini wasitake kumbebesha mtu mwingine msalaba wakati wao wana access ya kujua mambo mengi yanayotendeka katika nchi. Kwa hiyo jukumu la usalama wa Taifa, Mheshimiwa Rais kimsingi tunakubaliana naye katika mambo ya kupambana na watu ambao wanafanya tofauti lakini hakikisha Kitengo/ Taasisi cha Usalama wa Taifa inarekebishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru asante sana.