Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipatia nafasi na mimi niweze kutoa mchango wangu kwenye bajeti hii ya pili ya Serikali ya Awamu ya Tano, Serikali ambayo mwaka jana wakati tunachangia bajeti humu ndani ilijinasibu sana na tukawa tunaambiwa Waheshimiwa Wabunge tulieni bajeti ni ya kwanza.

Mimi jinsi ninavyoamini kati ya awamu zote zilizopita na zinazoendelea naweza nikasema kuwa, awamu itakayofanya vibaya na Watanzania watakuja kulia sana ni Serikali hii ya Awamu ya Tano ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnawaahidi Watanzania mnaacha kutekeleza mliyoyaahidi mnakuja mnatekeleza mambo tofauti na vile mlivyoahidi, yaani mnaimba kama malaika mnakuja kucheza kama mashetani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mliwaahidi Watanzania kuwajengea barabara….

TAARIFA .....

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kuweza kuniruhusu niweze kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee, wakati wagombea wakijinadi na vyama mbalimbali vikijinadi kwa Watanzania, vilikuwa vinanadi mambo mbalimbali ama shughuli mbalimbali za kijamii ambazo vyama hivyo


vitatekeleza kama vitapewa ridhaa.Mliwaahidi Watanzania kuwajengea barabara ili ziweze kupitika kwa mwaka mzima kipindi cha masika na kipindi cha kiangazi, hamjajenga barabara hata moja, mnawapelekea Watanzania waende wakawalipie motor vehicle.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hujajenga barabara unaenda unampelekea mwananchi wa kijijini akakulipie motor vehicle na Wabunge mko humu ndani mnapiga makofi, wananchi wenu kule vijijini barabara zisizopitika kipindi cha masika waende wakalipe hii motor vehicle hii siyo sawa, kwenye Ilani ipi ya Chama cha Mapinduzi mstari upi, ukurasa gani uliandika kwamba mtaenda kuwalipisha Watanzania motor vehicle. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii motor vehicle mmeamua kwenda kuwapelekea Watanzania kwa kupandisha mafuta ya taa, diesel na petrol yaani leo Watanzania wa nchi hii, umeme ni anasa, walibakia na mafuta ya taa, nayo mafuta ya taa yanaenda kuwa anasa kwa Watanzania. Mnaturudisha enzi za huko nyuma zama za kale za kwenda kuanza kutembea na vijinga kwenye vyumba kwa nini tunawafanyia Watanzania vitu vya namna hii ninyi? Hivi kwa nini hamna moyo wa huruma! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapokwenda kupandisha mafuta ya taa wakati umeme umeshindwa kuwafikishia Watanzania unakwenda kuendeleza kumdhoofisha Mtanzania maskini aendelee kuwa maskini mpaka siku yake ya kufa, hii inajidhihirisha kuwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Ilani yenu inajidhihirisha kuwa hamjawahi kuwa na dhamira ya dhati ya kwenda kuwaondoa Watanzania kwenye umaskini na ndio maana mnachokiadi hamtekelezi na mnajua mkitekeleza watu hawa wakiwa na uwezo wakawa na uchumi wao kwa story zenu hawatawachagua, kwa hiyo, mnabakia kila siku mnaahidi hiki mnaenda kutekeleza kitu kingine ili baada ya miaka mitano ikiisha mrudi tena kwenda kuahidi namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili suala la


kwenda kuhamisha motor vehicle kuwapelekea Watanzania waende wakalipe si sawa, si sawa kuwahamisha yaani motor vehicle ya Kunti nimpelekee mtu mwingine kule kijijini aende akanilipie motor vehicle, kila mmoja aende atimize wajibu na majukumu yake, Watanzania wale hawajatutuma sisi tununue magari, ni Watanzania wangapi wenye magari? Watu wengi waliopo vijijini hawana magari kwa hili suala nadhani halikai sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona Wabunge mnasema kwamba eti ile shilingi 40 iende kwenye maji, unakumbuka tulipendekeza hapa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji tulisema tutoe shilingi 50 iende kwenye maji, leo mnasema 40 iende kwenye maji, aliyewaambie inaenda kwenye nani? Nani aliyewaambieni inaenda kwenye maji? Hii inapelekwa badala ya motor vehicle, motor vehicle itakatwa kule tukinunua mafuta ndio umelipa motor vehicle, kwa hiyo, hili suala si sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala zima la kodi ya majengo, Watanzania hawa wanajenga kwa shida kweli, lakini kitu cha kwanza Mtanzania huyu analipa kodi ya ardhi, Mtanzania huyu analipa kodi kwenye cement, kwenye nondo, kwenye bati, kwenye kila kitu mpaka mchanga anaochota ardhini ukisombwa pale anaulipia kodi, leo tena hivi vijumba vyao ambavyo wamejijengea kwa shida mnaenda tena kuwanyonya hawa Watanzania waende wakawalipieni tena kodi, tena mnaenda kuwapandishia kutoka shilingi 3,000 mpaka shilingi 10,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawataka nini hawa Watanzania wa watu yaillai toba maulana, wametukosea nini Watanzania? Hivi kuwapa ridhaa ya kuongoza nchi hii ndio imekuwa adhabu kwao? Waoneeni huruma hawa Watanzania, mlienda kuwapigia pushapu mpaka misamba ya suruali ikachanika, kwa hiyo, waoneni kwamba ile huruma waliowapeni basi hebu itumieni kuweni na moyo wa huruma kwa binadamu wenzenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kodi ya majengo si


sawa, mngekuja mimi nilikua najua hapa mngekuja mkasema kwamba kama mnataka kodi ya majengo basi vifaa vya ujenzi vipinguzwe kodi ama viondolewe kabisa, ili muweze kuchukua hiyo kodi ya majengo, hamtoi vifaa vya ujenzi vinapanda kwa kupandisha mafuta vifaa vya ujenzi vitapanda. Lakini pili mnawapandishia hivyo vifaa vya ujenzi mnakwenda tena mnawatoza na kodi za majengo huko waliko, jamani mnawakamua kiasi hiki wamewakosea kitu gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu shilingi milioni 50, ni suala lile lile tunaimba kama malaika tunacheza kama mashetani, mliahidi hapa na mwaka jana tulisema, hili suala la milioni 50.

TAARIFA .....

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mdogo wangu Mariam nimsamehe bure tu, Jimbo lenyewe la Chemba halijui huyu, hiyo barabara imepita wala wananchi wa Chemba hawanufaiki na chochote kwenye lile Jimbo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Chemba, tulieni ninyi nini mnachozomea kitu gani? Tulieni hiyo, vitulizeni taratibu cristapen iingie, vitulizeni visiwashe saa hizi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina dakika zangu tatu zimebaki naomba unilindie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la shilingi milioni 50, mliwaahidi Watanzania kila kijiji kuwapatia shilingi milioni 50, tunataka tujue shilingi milioni 50 ni lini au ni deni watakuja kuwadai waanzie wapi kudai shilingi milioni 50, hatujaziona kwenye kitabu cha Waziri humu shilingi milioni 50 ziko wapi? Mlijinasibu na shilingi milioni 50 leo mwaka wa pili, bajeti ya pili hii kitabu kinapita empty, hata dalili wala harufu wala sisikii Mbunge wa CCM akiongelea suala la shilingi milioni 50, ni lini hizo shilingi milioni 50 mtazitoa?

TAARIFA.....

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nahisi Waheshimiwa Wabunge wa Chama cha Mapinduzi hawanielewi. Nimesema hivi jamani mlichokiahidi sicho mnachokitekeleza ni miaka miwili sasa, mliahidi shilingi milioni 50, mliahidi barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mmeahidi shilingi milioni 50 mmeenda kujenga uwanja wa Chato wa ndege! Hivyo ndiyo vitu shilingi milioni 50 mtaitoa lini? Siyo suala kwamba miaka Mitano, hivi vingine havikuwepo hata kwenye Ilani yenu, vimepatikanaje? Halafu unakuja unaniletea story hapa eti Ilani ya Chama cha Mapinduzi inanihusu nini mimi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka Waziri akija hapa atuambie, shilingi milioni 50 ni lini zinaanza kutolewa kwa Watanzania wetu, ukidai ujue na kulipa.