Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

HE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa fursa ya kuwa mchangiaji wa mwisho kwenye Kikao hiki cha Bunge. Ninapenda sana kumpongeza Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana pamoja na Naibu Waziri, hakika mmetutoa kimasomaso, hakika mmejibu kiu ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haya yanayotendeka, kwa sakata zima la makinikia, Mkoa wa Kilimanjaro umeniagiza kwenye Bunge lako hili Tukufu kwamba, wao wamesimama na Mheshimiwa Rais kwa sababu nao ni wahanga hata kupitia machimbo ya Tanzanite. Kwa hiyo, wamenituma niseme kwenye Bunge lako hili Tukufu, ikitokea leo Mheshimiwa Rais anaomba kwenda Mkoa wa Kilimanjaro watahitaji miezi sita waweze kupanua ule uwanja uliompokea juzi kwenye Mei Mosi ili waweze kukaanae na kumpa hongera hizi. Kwa kweli Mheshimiwa Rais popote ulipo pokea pongezi za dhati kutoka kwa Mkoa wangu wa Kilimanjaro. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasita leo kujiuliza maswali mengi, nimemuangalia kaka yangu Mheshimiwa Januari Makamba simuoni! Nilitaka nimuulize neno moja, hivi huu sio ule utabiri wa Mzee Makamba tulipokuwa pale kwenye ule Mkutano Mkuu ambapo walisema alisema huyu ajaye atatubatiza kwa moto, hivi huu sio moto? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu, imefika tunaongea hata tusiyoyajua. Network zimekata, connection hakuna, links hakuna chochote kinachoendelea katika Bunge hili. Wamekuja watu hapa wanatuambia kwamba makinikia ni suala la mtaani, limeletwa hapa kuja kutufunga midomo, kuja kuchafua Bunge, wapi na wapi?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kaka yangu pale, namheshimu sana Mheshimiwa Ally Saleh, tuko kikao kimoja kule SADC, michango yako naiheshimu sana, lakini kwa kweli leo umenifanya pengine hata nitakosa usingizi juu ya mchango wako juu ya leo. Mbona ilipaswa mpaka tunapokuja kuchangia tuwe tumesoma ripoti ya Profesa Mruma, lakini pia na ripoti ya Profesa Osoro, kwani hatufahamu…

TAARIFA ....

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, sioni tofauti ya kutugawa na migongano ya kifikra na kimaslahi. Ripoti imeeleza bayana tunapoteza shilingi trilioni tisa kwa mwaka mmoja kwa miaka 17, tumepoteza shilingi trilioni 108. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunaotambua uchungu wa wavuja jasho wa Taifa hili lazima tulisemee hapa. Kuna direct link, tunaona mahusiano ya moja kwa moja kwenye upotevu huu wa pesa pamoja na michango yetu katika Bunge lako hili Tukufu hususan kwa kupitia Wizara hii, Wizara hii na bajeti ya fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sio hivyo tu, kama sio huu ubatizo wa moto, ninashangaa wengine wanasema hapa sisi tumekuja kuimba nyimbo za mashetani! Ngoja nikuulize rafiki yangu kijana wewe unayejiita kijana wa Dodoma hii, sikiliza, sisi hatuimbi nyimbo za mashetani, ndugu yangu tunaimba za kucheza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Ninyi mlikaa kwenye Ilani yenu, mlihubiri kufufua wafu, akina Balali mlituambia mnataka kumfufua Balali, ni nani anayeimba nyimbo za mashetani humu ndani? Ni nani anayeongea lugha za kufufua mashetani humu ndani kama sio wao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sio hivyo tu, wamejitahidi sana kutuvunja mioyo humu ndani. Walikuja wakatwambia kwamba, tutaenda kushtakiwa kwenye Mahakama ya Kimataifa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)