Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Nianze na ugatuzi mikoani, jinsi sasa hivi Serikali inavyo-treat masuala ya Serikali za Mitaa ni kama vile Serikali za Mitaa hazitakiwi. Ningemwomba Mheshimiwa Waziri Serikali hii inachotaka kukifanya ni kile ambacho Mwalimu Nyerere aliwahi kukifanya, kikashindikana na akaanza tena ku-empower Local Government. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mawaziri wa TAMISEMI wote hapa kila jambo likifanyika wanaelekeza kwamba kwenye Local Government nyie Wabunge ni Madiwani, mkakusanye hela, mhakikishe mambo yanafanyika lakini wakati huo huo mnanyang’anya vyanzo vyote vya mapato kwenye Local Government, kwa hiyo, mnasema jambo lingine na huku mnatenda jambo lingine.

Mheshimiwa Spika, kwa kifupi ni kwamba bajeti ya Mheshimiwa Waziri muundo wa ukusanyaji kodi una-cripple utendaji wa Local Government. Mlitoa Property Tax, marejesho yanayorudi kwenye Local Government yamekuwa ni kidogo sana ukilinganisha na jinsi tulivyokuwa tunakusanya. Kwa mfano, Iringa Mjini tulikuwa tunakaribia kupata karibu shilingi bilioni moja sasa hivi mmetuletea kama shilingi milioni 200 na bado main power watu wa TRA wanahitaji kutoka huko kwenye Local Government kitu ambacho hakina sababu mngetuachia tukusanye wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine kubwa ambalo tunalijadili wote na ambalo nami nataka niliseme kuhusiana na suala ambalo kama Taifa tunataka tupasuke lakini wakati huo huo hatutaki kwenda kwenye kina kuhusiana na suala hili la madini. Hili suala la madini mimi bado narudia approach, hawa wawekezaji waliokuja hapa nchini is unfair to call them ni wezi, mimi sikubaliani kuwaita kuwa wao ni wezi.

Mheshimiwa Spika, nasema hivyo kwa sababu mwaka 1997 na 1998 kuna sheria zililetwa humu ndani Bungeni na zikapitishwa. Chama cha Mapinduzi mlikuwa na sera yenu na mkanadi kwenye Ilani, Rais anapochaguliwa nyuma anasukumwa na policy ya chama, mtuambie sasa hivi policy ya madini ya chama chenu ni ipi. Policy ya madini ya chama chenu mkaleta, zikapitishwa humu ndani na haya mambo yote ambayo hawa wawekezaji waliingia nchini yalipitishwa kwa mujibu wa utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wabunge tusishabikie hivi vitu bila sababu kwa sababu mambo haya kabla mikataba haijafanyika, kuna timu za wataalam zinakaa, zinajadiliana baadaye Makatibu wa Wizara wanakaa, wanapitisha baadaye Mawaziri mnakaa ndipo Rais anasaini. Vinginevyo mtuambie hata Mheshimiwa Magufuli hizi nyumba za Serikali aliuza peke myake na kama aliuzam peke myake mna yeye tumchunguze aliuzaje nyumba za Serikali.

SPIKA.... Kidogo tu Mchungaji....

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nimekusikia, naomba ninukuu kidogo, nikumbushe zile sheria ambazo Bunge hili lilizipitisha na policy ya Chama cha Mapinduzi ilisimamia sheria hizi. Sheria ambazo zilitungwa na Bunge hili, namba moja, Sheria ya mwaka 1997 iliwapa wawekezaji wa kigeni ulinzi mkubwa wa manufaa mengi kama vile kuondosha nje fedha na faida yote wanayoipata kwa uwekezaji wao nchini na mikataba ilikuwa siri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu cha pili, Serikali hii hii ilikuwa inaongoza, Sheria ya Uwekezaji ya Tanzania ya mwaka 1997 iliwapa wawekezaji wa kigeni ulinzi mkubwa na manufaa mengi kama vile kuondosha fedha nje na faida yote wanayoipata kwa uwekezaji wao nchini, wanaondosha vyote sheria inasema hivyo, sasa tunawaitaje wezi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine, mwaka 1997 Bunge lilipitisha Sheria ya Madini ambayo ilitamka kwamba mwenye miliki ya madini na fedha yote itokanayo na mauzo ya madini ni mwenye leseni ya kuchimba madini hayo…

T A A R I F A......

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, mjadala ungekuwa mzuri kama tungepeana uhuru wa kuzungumza kwa sababu wenzetu wanazungumza mpaka wanaongezewa na dakika, you got to see our views, smooth water never develop a skillful sailor. You guys you are looking for smooth water, ukitaka upate baharia mzuri akumbane na maji magumu, hebu mpate maji magumu ili muonekane umahiri wenu basi, mbona mnaogopa tukisema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachokisema, hizo sheria zilikuja kwa Hati ya dharura hapa, tunachogaombana hapa, Serikali inafanya kazi kwa kuwajibika wote, lakini Mheshimiwa Rais mnalosema tumshangilie na tumuunge mkono, hakuna mtu anayekataa kuzuia wizi unaoonekana lakini Mheshimiwa Rais alikuwa miongoni mwa Baraza la Mawaziri. Wakati Zitto anazungumza na Karamagi hapa alikuwa ni miongoni mwa waliosema Zitto asulubiwe wakamtoa Zitto nje kuzungumza hii mikataba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa leo haya masuala ya madini…

T A A R I F A

Mheshimiwa Spika, lakini nimeipokea. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, alichokuwa anasema wajina wangu Peter Serukamba nakubaliana kabisa, lakini mimi siyo mtu ambaye napenda ku-embrace mediocrity. Kwa nini nasema hivyo? Let us be honesty, hakuna mtu anayekataa tusiibiwe lakini kama Chama cha Mapinduzi, Mheshimiwa Spika unasema kwamba siwezi kutoa ushahidi, Chama cha Mapinduzi ndiyo mmekuwa majority humu ndani, kwa hiyo, sheria yoyote hapa ndani haiwezi kupita bila ninyi kuipitisha. Kwa hiyo, sheria zote ziwe nzuri, ziwe mbovu zilipitishwa na Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, sasa tunachotaka kukisema kama Rais ni muungwana, anajua hawa hawa akina Tundu Lissu ambao leo mnawatukana walipambana na haya mambo toka zamani, asimame kwenye television aseme kwamba mimi nimegundua wezi hawana Chama, wanaweza kuwa CCM wanaweza kuwa CHADEMA na mimi nimegundua ndani ya Chama cha Mapinduzi kuna majizi. Kwa sababu ndani ya Chama cha Mapinduzi kuna majizi naomba tushikane wote mikono tung’oe wezi CHADEMA na tung’oe wezi CCM. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nawashangaa sana wenzangu wa Chama cha Mapinduzi, kimsingi Rais anachokifanya Sera ya Chama cha Mapinduzi ameweka pembeni anaongoza kama vile ni Mgombea Binafsi. Hiyo mimi namuunga mkono kwa sababu sera yenu kuhusu madini ni hiki kilichofanyika, sasa leo mnageukaje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana tunasisitiza kama kweli Mheshimiwa Magufuli ana dhamira ya kweli ya kuleta mabadiliko katika nchi hii hapa, alete mabadiliko kwenye Katiba ili Marais waweze kuhojiwa. Hiyo ndiyo dawa pekee kwa sababu vinginevyo hata yeye ameuza nyumba za Serikali kitu ambacho siyo kweli asingeuza bila Mkapa kusaini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeshangilia Muhongo kuondoka wakati sheria hizi mbovu maskini hata Muhongo hakuwepo wala hii sera hakuwepo, leo tunashangilia Muhongo kaondoka hakuwepo, he was not here.

KUHUSU UTARATIBU.....

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Vilevile tunatakiwa tuwe skillful tunapo-deal na hawa tunaowaita wezi. These are not intruders, we invited them in this country. Sasa kwa sababu tuliwa-invite siyo kwa sababu tu tuko vitani hatuendi blindly lazima tuwe skillful. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunachokizungumza hapa hata haya mambo unayosema yalikuwa ya World Bank hata madini ni World Bank hivyo hivyo, tuko-pushed hivyo hivyo lakini sisi hatukulazimishwa kula, hawatukushikia, tulisaini hapa wengine wakaenda usiku, mkapiga mayowe hapa, mkaunga mkono. Bunge lililopita kwa Mheshimiwa Spika Makinda nakumbuka mara ya mwisho hapa zililetwa sheria tatu za dharura, Mnyika alikuwa anaomba…

Kwa siku moja, tukalazimika tukatoka nje, tukazomewa, tukafukuzwa humu ndani sasa leo mnasema twende mbele tu, tulitoka humu ndani wote, mnasema twende mbele tu tusikumbuke nyuma, why? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii tunayosema kama mpo sincere mnataka tupigane hii vita kwa sababu kwanza hii vita mlikuwa hamuitaki, sasa kwa sababu Mheshimiwa Rais, yeye ameamua kutofuata...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)