Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Niruhusu nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, muumba mbingu na ardhi, aliyetujalia sote uhai, afya na uzima na kutuwezesha kuwa hapa tukijadili hili suala tunalojadili kwa mara ya pili sasa katika kipindi hiki au awamu hii ya uongozi tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nifuatilize kwa jambo jema kabisa ambalo limewahi kutendwa hapa duniani ambalo ni kuhusiana na kuusia mema na hasa kuusia kumcha Mwenyezi Mungu. Basi na mimi niwausie kama ninavyousia nafsi yangu kumcha Mwenyezi Mungu kwa namna inavyopasa kumcha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni chini ya uongozi thabiti wa Mheshimiwa Mbowe, akisaidiwa na mimi hapa ndugu yake, lakini pia chini ya usaidizi mkubwa kabisa wa Mwenyekiti Mwenza, kaka yangu mpenzi, Mheshimiwa James Mbatia. Ama timu ya UKAWA inafanya kazi na kwenye ukweli siku zote uongo hujitenga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika pongezi ambazo ningependa kuzitoa leo hii kwa uzito wa kipekee kabisa, nimpongeze kiongozi wangu mwadilifu, mcha Mungu, muungwana, mpenda amani na yeye mwenyewe ni kipenzi cha watu; huyu sio mwingine ni Katibu Mkuu Mwenza wa UKAWA, Mheshimiwa Maalim Seif Sharrif Hamad ambaye yeye siyo tu ana dhamira ya kuendeleza amani, bali anafanya kwa kitendo. Anatekeleza suala hili, anaendeleza amani na maelewano katika nchi hii na kwa kweli penye ukweli pasemwe. Laiti Maalim Seif angekuwa kama viongozi wengine wa Afrika wale ambao wana maslahi binafsi au wana ubinafsi, basi Bunge hili inawezekana ingekuwa saa hizi tunajadili mengine au nchi hii kwa ujumla wake ingekuwa katika hali tofauti na hii tunayoiona sasa hapa. Nampongeza sana, namwomba Mwenyezi Mungu amzidishie subira na ucha Mungu na kwa hakika yeye ni miongoni mwa wenye kufaulu duniani na akhera. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi wala si mtaalam sana wa takwimu lakini masuala mengine yamekuwa tabled hapa wiki iliyopita na kwa vigelegele kabisa mpaka watu wakasimama wima mimi nilikuwa nashangaa na naamini ulikuwa unaniona, nilikuwa nashangaa hivi kweli hotuba hii inastahiki kusimamiwa, kwa lipi lililomo mle jipya? Walichojitahidi sana ni kucheza na maneno, semantics genetics tu, sarakasi za maneno lakini hazina jipya lilotuletea hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, semeni kwa ukweli wa dhati wa mioyo yenu Waheshimiwa hivi unapoongeza tozo kwenye mafuta ya taa nia yako hasa ni nini? Wapiga kura wetu walio wengi lile wenyewe wanaita jiko la mchina ndiyo gesi yao na ndiyo electric cooker yao. Hivi unavyowaongezea hiyo gharama ya kununua mafuta ya taa unataka waende wapi? Unaongeza bei ya mafuta wakati ambapo tunakaza nati kwenye masuala ya mazingira na kuwazuia kukata miti, hao wananchi waishi maisha ya namna gani hebu niambieni Waheshimiwa? Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri ukija hapa tuambie hawa walala hoi wa Tanzania wewe unataka waishi maisha ya aina gani mwaka huu wa 2017/2018? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesahau yule Malkia wa Ufaransa alikuwa wa mwaka gani lakini katika kituko chake cha ile kuonyesha kiasi cha yeye kuwa mbali na realities na uhalisia wa mambo, wananchi walipoandamana wakasema hatuna mikate akawaambia why don’t you eat cake, hamna mkate kuleni keki. Kumbe wenzie wanasema hawana mkate yaani hawana hata kile cha kuendesha maisha ya kawaida, sasa ndiyo tunachokifanya hapa. Tumeshindwa kutafuta shilingi trilioni zile pungufu 29 leo tunasema tunataka shilingi trilioni 32 tunazitoa wapi kwa hali halisi? Halafu hatuonyeshi mbadala ulio mahsusi na makini wenye kueleweka kwamba hivi ndiyo vyanzo ambavyo vinakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani nakusihi sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, hebu soma kwa uadilifu bila hiyana maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ambayo Masha Allah leo kijana wangu Silinde kaya-present yakiwa kwenye fomu yake hasa. Yapitie kwa umakini kabisa, utaona mapendekezo gani yamo mle kuhusu vyanzo vya mapato, lakini pia kuhusu ipi iwe ndiyo budget figure yetu. Tuache kucheza na maneno hapa, tuache kuwadanganya walimwengu lakini mwisho wa yote tunajidanganya sisi wenyewe. Hivi unaposema nitakimbia kilometa saba ukashindwa ukaishia mbili na nusu halafu unakuja tena unasema sasa mara hii nataka kukimbia kilometa kumi, inatokea wapi mambo hayo? Jamani kwa nini tunajidanganya hivi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwalimu Bilago pale kauliza huyo aliyeturoga nani huyu? Sisi kule kwetu wanasema ukiona hali kama hii huyo aliyekuroga kafa maana angekuwa hai angekuhurumia. Laiti yule aliyeturoga Watanzania angekuwa hai akatuona tunavyodhalilika humu, tunavyosema mambo ambayo hayana kichwa na miguu wala hayana mbele wala nyuma angetuhurumia. Basi akapunguza, wanasema anapunguza ile dozi, basi na sisi tungepata ahueni. Waheshimiwa Wabunge nawasihi sana tumwogope Mwenyezi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwalimu wangu mmoja wa jiografia nilipokuwa O-level, Mrs. Seif, Mwenyezi Mungu ambariki sijui yuko wapi sasa hivi, katika ufundishaji wake mzuri sana wa geography ya maeneo alikuwa anatupandisha ndege na meli lakini tuko Kisutu Sekondari. Anatuambia fumba macho leo tunaondoka Zanzibar kwa boti namba fulani tumeingia baharini, mawimbi yanafanya vile, fumba macho na kweli tunafumba macho tuna-internalize ile safari yote mpaka lile aneo jipya tunalokwenda. Hebu na sisi tufumbe macho tu-internalize haya mambo, tu-internalize hii bajeti process yetu kila figure, tumvute kwenye picha hii kubwa kila mtu ambaye anaguswa na bajeti hii, tusijifikirie sisi wenyewe tu Waheshimiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mambo ambayo mimi naamini au katika vitu ambavyo ninajua kabisa bila hata kufundishwa wanasema, I am spill of effect au trickling down effect ni masuala ya mafuta. Unapoongeza tozo kwenye diesel na petrol unatarajia hao wenye mabasi yao akina Mheshimiwa Shabiby watawacha nauli ile ile, si watapandisha? Madaladala si watapandisha nauli? Mwalimu Bilago kasema hapo unadhani bidhaa itakayotoka Dar es Salaam mpaka ikafika huko Kakonko sijui itakuwa bei ile ile, itakuwa bei juu. Sasa sisi tunafanya nini jamani mbona tunagusa mahali sipo!

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tunafanya jambo kama hili wakati tunadai eti tunataka kuwasaidia walalahoi, hatuwasaidii walalahoi. Labda mniambie mmekuja na system ambayo mtatengeneza kwenye vile vituo vya mafuta ile gari ikienda inakuwa detected, hii ni ya Mheshimiwa Ashatu mkate huyu, hii ni gari la daladala usikate labda iwe hivyo lakini kama tunaweka hii blanket amount halafu kwa system hii ya kawaida kwa kweli tunakwenda kuwaumiza watu wetu na walio wengi wataanza sasa kutumia hii tunaita TZ eleven, watatembea kwa miguu badala ya kutumia vyombo vya usafiri kwa sababu hawatamudu kutoa gharama hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, waswahili wanasema kama ilivyo dawa ya jipu kulitumbua dawa ya deni kulipa. Msitumie maneno lihahimilika, linavumilika, linahamishika, linakwenda wapi? Bado linabaki ni deni letu la taifa, tulilipe, tuwe na clean slate halafu tunaanza upya. Watu tumelalamika hapa na Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti kasema kuhusu riba, riba tena inatuning’inia rohoni hapa hatujiwezi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitawaambia jambo lakini ninyi mtakasirika kwa sababu lilishaingia Bungeni humu likaleta siasa na chuki, go OIC ambapo tunapata mikopo haina riba. Kama OIC mnaiona ina ukakasi, mimi naamini kama hiyo economic diplomacy yetu tungeitumia vizuri wangetutafutia partners ambao wangeweza kutupa mikopo kwa bei nafuu kabisa. Naamini hao watu wapo, hizo nchi zipo kwenye Bara la Ulaya tungeweza kupata hao partners ambao wangetupa arrangements zenye unafuu sana na mikopo ambayo kweli tungeweza kuhimili. Siyo hii mikopo ambayo tunaenda kukopa kibiashara kwenye arrangements ambazo zinatutoza riba kubwa mwisho wa yote capital hatulipi na wala hiyo riba inayoongezeka kila mwaka hatulipi, tunaendelea kubadilisha maneno hapa mara leo linahimilika, kesho sijui litavumilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba sana Mheshimiwa Waziri husika hebu atuambie vizuri haya maneno hasa mwisho wake nini na nini anapotuambia tunaweza kuhimili deni ili mwisho wake iwe nini. Atuambie tu hii bajeti yake inajibu vipi vilio vile ambavyo tulivisikia hapa wakati tunajadili Sectorial Ministries. Tulipokuwa tunasema maji, kila mtu hana maji na Mheshimiwa kaka yangu Almas anamalizia hiyo imekwisha, Wizara ya Maji ilishapita na hii bajeti haina hata maji humu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejadili hapa kila kitu elimu matatizo, afya mtihani, maji ndiyo hayo, barabara hazisemeki, kila kitu kila kitu hakipo. Hii bajeti hii hapa hii ukiondoa hiyo dhamira ya kuendeleza amani ambayo wala haipo mnafanya nini ku-address vilio vyote vile ambavyo vimesemwa katika Bunge lako hili Tukufu kuhusu maisha ya Watanzania kwa mustakabali wa nchi yetu.