Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi kwa Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanazofanya kusimamia Wizara ambayo ndiyo heart beat ya uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania inabidi tutumie catch-up economic growth approach as opposed to endogenous technology – driven economic growth approach ambayo wenzetu nchi zilizoendelea zinatumia kwa kutumia industrial revolution ambayo diffusion yake ilianzia England na kusambaa West. Tanzania inabidi catch-up approach tuielekeze kwenye kilimo, ufugaji, uvuvi na ujasiriamali mdogo mdogo ili (taken together) tuweze kutoka kwenye umaskini ambao ni asilimia 65 ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara iangalie na kuzipa uwezo TIB na TADB ili ziweze kuwa mstari wa mbele na engine ya kusukuma catch up economic growth ninayozungumzia. Kwa hali ilivyo sasa, kwa kweli bado we are not walking the talk. Nashauri mkae na TIB na TADB muangalie synergies na nani atafanya nini na kwa nini lakini kwa kushirikiana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza Sera ya Bima inayoandaliwa 2017/2018. Nashauri NIC ajikite kwenye kusaidia majukumu ya kibima kwenye catch-up economic growth hapo juu. It has to be integrated badala ya kuendelea na business as usual ambayo quite frankly naona tija na weledi wa NIC in its current practice haupo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi milioni 50 kwa kila kijiji ni vema zikachelewa lakini tukajipanga, tukalenga kwenye kutekeleza catch–up economic growth as argued above. Nashauri mkae na UTT na TADB na kutumia uzoefu wao, washauri model ya kutumia milioni 50 kwa kila kijiji katika namna iliyo endelevu na inayolenga ku-achieve niliyoeleza hapo juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.