Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuwa na uchumi imara na kuwa na mchango mkubwa wa pato katika uchumi ni muhimu Wizara kama msimamizi wa uchumi nchini iwe na kipaumbele katika ujenzi wa uchumi wa viwanda. Nashauri kwamba Wizara iwekeze katika viwanda vinavyohusiana na kilimo ili kuchochea uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo jema kuwa suala la pension kwa wastaafu limezingatiwa katika bajeti hii. Nashauri kwamba uhakiki ukamilike mapema na malipo yafanyike kwa wakati wakiwemo waliokuwa watumishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ni muhimu sana katika kudhibiti nidhamu ya matumizi Serikalini, lakini imekuwa haiwezeshwi kwa kiwango cha kutosha. Hivyo, nashauri CAG apewe fedha za kutosha kulingana na bajeti yake na fedha hizo zipatikane kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki ya Maendeleo ya Kilimo kwa umuhimu wake ipewe mtaji wa kutosha na kutanua mtandao wake ili iweze kuwafikia watu wengi zaidi wanaohitaji huduma yake hasa walioko vijijini, mfano, Ukerewe. Pia ukopeshaji katika benki hii utoe fursa vile vile kwa Sekta ya Uvuvi kunufaika na benki hii jambo ambalo litaongeza sana nguvu ya kiuchumi ya watu wetu hasa vijijini.