Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, kutokupeleka fedha kwenye Halmashauri kama zilivyopitishwa katika bajeti. Kama tunavyoambiwa Serikali inakusanya fedha wakati mwingine hadi kuvuka lengo, kwa nini sasa hazipelekwi katika Halmashauri zetu? Kutokutoa OC za Idara za Halmashauri zetu ni kuzidhoofisha na kusababisha makusanyo wanayokusanya kushindwa kufanya kazi iliyokusudiwa na badala yake fedha hizi za makusanyo ya Halmashauri kutumika kama OC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokulipa madeni ya Wazabuni kwa wakati, wakiwemo Mawakala waliosambaza pembejeo. Hii ni kuendelea kufanya wananchi wafilisike na kufilisiwa na taasisi zinazotoa mikopo ya fedha na vile vile kufanya huduma zilizokusudiwa kutotolewa kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kushindwa kurejesha asilima 30 ya makusanyo yanayotokana na makusanyo ya kodi ya majengo, hivyo kuyumbisha malengo na bajeti za Halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri Serikali kuheshimu bajeti zinazopitishwa na Bunge. Matumizi ya fedha za Serikali yafuate bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.