Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika haya yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukarabati wa mikakati ya kupunguza umaskini katika aya ya 26 limeongelewa suala na mafunzo kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii, je nini tofauti ya kada hizi? Kwa nini isijumuishwe ikawa kada moja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu taasisi za mafunzo aya ya 165, Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP); pamoja na kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka 5,852 hadi 6,500 bado idadi hiyo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya wanafunzi wanaoomba nafasi katika Chuo hicho na hivyo wakati mwingine kupunguza mapato na kufanya Chuo hicho kushindwa kujiendesha. Je, Serikali inasema nini kuhusu suala hilo? Je, Serikali inasema nini kuhusu kupeleka OC kwa wakati ili vyuo hivyo viweze kujiendesha na kufanya kazi zake za kutoa taaluma kikamilifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la road licence ni vema sasa Serikali ikaangalia upya mpango huu hasa kwa yale magari ambayo hayatembei. Ili kuondoa malalamiko kwa wananchi ni vema sasa tozo hii ikahamishwa kwenye mafuta ili mtumia chombo cha usafiri aweze kulipia tozo hiyo kwa chombo kinachotembea na yale yasiyopo barabarani yaachwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.