Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nichukue nafasi hii kumpongeza kabisa Waziri wetu na Naibu wake ambao kama mnajua wamebobea pia katika nyanja za Kimataifa. Kwa hiyo, tunapowauliza habari za diplomasia ya uchumi, Wahaya tunasema, usimuulize mganga wa kienyeji kondoo kapita wapi? Kwa sababu anaelewa anachokifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawapongezeni kabisa kwamba hapa hatua tuliyopiga siyo haba na kazi kubwa ambayo inafanyika katika uwanja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kiasi cha kwamba sasa hili bomba lililokuwa linaenda Kenya tayari limeshaingia Tanzania, tunamshukuru sana. Hili ni jambo kubwa sana, siyo jambo la kuchukulia hivi hivi, linataka diplomisia ya kiuchumi ambayo inafanyika nyuma ya pazia, wanasema ni lobbying. Huwezi kupiga kelele ukafanya mapinduzi makubwa kama hayo. Kwa hiyo, tunampongeza sana Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili naomba nipongeze sana juhudi ambazo zinaendelea pia kupanua wigo wa nchi rafiki, nchi ambazo zimepiga hatua kama Uturuki, nimeiona ni nchi ambayo naifahamu sana, nimeifanyia kazi kule na imepiga hatua. Kwa hiyo, wakija kutusaidia, nalo siyo jambo dogo la kubeza, tunawapongezeni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa kuwa nina dakika tano mbali ya pongezi, naomba Mheshimiwa Waziri utakaposimama, nami unitoe dukuduku kwa yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, tuna tatizo la mipaka ya nchi hii ambayo haina mikataba (treaty). Nchi hii mwaka 1979 ilipigana vita Uganda kwa sababu ya kutokuwa na mpaka ambao una mkataba wa Kimataifa. Ninaomba nijue kabisa unachukua hatua gani kukamilisha jambo hili?

Jamani ndugu zangu naomba niwaambie, Rais Museveni akiondoka madarakani Uganda, msishangae tukienda pia kupigania huu mpaka. Kwa sababu ule mpaka ni one degree South of the Equator na ukifuata protocol hiyo, Tanzania itapoteza ardhi kubwa sana. Kwa hiyo, ni jambo ambalo lina utata, naomba nijue kama Mheshimiwa Waziri analifanyiaje kazi? Hii inaendelea kwenye mipaka sehemu kadhaa…


TAARIFA ....

MHE. PROF. ANNA K. TIBAIJUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mheshimiwa Lissu utafikiria na ungeamini kwamba anajua anachokiongea. Naweza kusema kwamba mimi kama mtaalam wa sekta, huyu hajui anachokiongelea sasa hivi Mheshimiwa Lissu. Kwa hiyo, siwezi kupokea taarifa ambayo haina knowledge. Ni lazima mpaka uwe na treaty. Hili tamko la African Union ni aspiration peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu nayakataa, naomba niendelee, nitakuja kumwelewesha zaidi Mheshimiwa Lissu baadaye nimpe habari anayotakiwa kuifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo naomba Mheshimiwa Waziri atakaposimama atueleze ni jinsi sasa Tanzania tutakavyojipambanua katika Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo Mwalimu Nyerere na Amir Jamal walileta heshima za nchi hii. Shirika la UNCTAD sikuliona hapa katika orodha ya watu unaowasiliana nao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Rais wetu amekazana tusiibiwe madini, lakini kama huna mashirika haya including South Center kule Geneva, taasisi ambayo ilianzishwa na Mwalimu Nyerere kupigania haki za mambo ambayo tulikuwa tumeonewa, tukaweza kufutiwa madeni. Sasa nataka kujua mkakati ulionao Mheshimiwa Waziri kuhusu UNCTAD kutusaidia kuondokana na hii kadhia ya mikataba mibovu ambapo tumekuwa tumeibiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kwenda na International Diplomacy sisi ni Taifa change, hatutaweza kufika, Rais wetu amejidadavua kama Mwalimu Nyerere, anapigania haki ambazo tulikuwa tumepokonywa. Sasa ninyi mnamsaidiaje kuhakikisha kwamba hatutatengwa? Kwasababu pia inabidi twende kimkakati (strategically), tusije tukajikuta tunaingia katika hatari ya kutengwa. Ni jambo ambalo nadhani ni diplomasia ya kiuchumi ambayo nilifikiria kwamba Mheshimiwa Mchungaji Msigwa angekuwa anaifahamu, lakini sikusikia akiizungumzia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho kwa dakika tano, nilikuwa nataka kusema kwamba Afrika Mashariki, sasa hivi Kenya wameridhia Mkataba wa EPA (Economic Partnership Agreement), napenda kusikia Waziri anajitayarishaje sasa kuhakikisha kwamba zile athari zinazoweza kutokana na hali kwamba nchi moja imeshasaini na sisi bado, ni ipi? Sisi ni nchi inayoendelea, tuko protected na World Trade Organization, lakini ni vizuri kwa Wizara ya Mambo ya Nje kuwa wamejipanga katika hili kwamba athari zitapoanza kuonekana sisi tutalindaje maslahi yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa dakika hizi tano, yangu ndio hayo. Ninaunga mkono hoja.