Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Awali ya yote naomba niwatakie Waislam wote nchini na duniani kote Ramadhan Kareem. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kipekee kabisa nimpongeze Mheshimiwa Rais, Jemedari wetu kwa tendo lake la kihistoria na la kizalendo kabisa juu ya suala zima la mchanga wa dhahabu unaojulikana kama makinikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba mikataba mibovu na kukosa uzalendo ndivyo vilivyotufikisha hapa tulipo, wala siyo siri. Pamoja na hayo, hii ni vita yetu sote Watanzania, kama Mheshimiwa Lema alivyozungumza, Mama Mheshimiwa Profesa Tibaijuka naye amezungumza masuala ya UNCTAD, lakini lazima tumuunge mkono Mheshimiwa Rais wetu. Hii vita ni yetu sote kwa vizazi na vizazi vijavyo, kwa sababu vita hii aliyoanzisha Mheshimiwa Rais ni vita ya uhuru wa nidhamu na uchumi katika masuala mazima ya kidiplomasia ya uchumi. Nina uhakika hata Mheshimiwa Waziri husika naye ataliweka hili jambo kidiplomasia zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo nataka kuzungumzia kwa uharaka sana ni suala zima la commercial attaches wetu katika Balozi. Nimekuwa nikisema hili kwa muda mrefu sana, kuwa Mabalozi wetu na commercial attaches wetu kwa diplomasia ya kiuchumi ambayo imeanza tangu mwaka 2001, tunahitaji Mheshimiwa Waziri atakapokuja ku-wind up atueleze performance targets zao kama wanapewa ama hawapewi kwa maana ya kwamba, je, wanapewa marbles? Vilevile mid reviews zinafanyika ama hazifanyiki? Tunaomba hilo tuweze kuelezwa kama wanafanya kazi kimkakati, basi tunahitaji wawe kimasoko zaidi na matokeo chanya tuweze kuyaona. Vinginevyo ikishindikana nitashika shilingi ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri, ukurasa wa 18 mpaka 50 amezungumzia conference diplomacy, tunampongeza, matokeo chanya tumeyaona, sihitaji kwenda kwa urefu na mapana ni viongozi gani ambao wameweza wakijadiliana nao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala zima la shuttle diplomacy. Mimi natoka katika Mkoa wa Mbeya, kuna Ziwa Nyasa ambalo mgogoro wake ni wa muda mrefu sana. Hii shuttle diplomacy kama imeshindikana, worse to worse basi tuingie katika sanctions kama ambavyo iko kule katika nchi ya Burundi. Shuttle diplomacy naona haifanyi kazi inavyotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijakaa, naomba niipongeze Serikali kwa kufungua Balozi mbalimbali pamoja na Ubalozi wa Israel. Nimekuwa nikilia kwa muda mrefu sana lakini nikasema pia wengine kule sisi ni Taifa teule, ndiko tunakokwenda kuhiji na pia kama nchi mengi tunajifunza kutoka kule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda wangu ni mfupi, naunga mkono hoja, nakushukuru. Ahsante.