Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Kwanza kabisa namshukuru sana na kumpongeza sana Mheshimiwa Rais Magufuli kwa kuthubutu kuthubutu kuanza kushughulika na masuala haya ya mchanga wa dhahabu, makinikia kwa lugha nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huko nyuma tulikuwa tunalalamika sana kwamba kuna mikataba mibovu tumeingia, tunapata hasara, hatulindi rasilimali za nchi. Leo Mheshimiwa Rais amethubutu kufanya hiki, ninashangaa kuna watu wanabeza hiki kinachoendelea. Ni ajabu sana.
(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni hatua kubwa sana ambayo Rais ameifikia, sisi kama wananchi wa Tanzania bila kujali itikadi zetu za vyama, ni lazima tumpongeze Mheshimiwa Rais kwa hatua hii. Hata kama kungekuwa na concequences zozote ambazo nchi inakwenda kuzipata kwa hili ambalo Rais amelifanya, ni lazima tukubaliane kama nchi kwamba hili ni letu wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, wale wanaoanza kutoa lawama bado mapema, tayari Wizara ya Nishati na Madini inakuja, tusubiri, tuache nafasi ya Wizara nyingine kuendelea kuchangia kuhusu hili suala zima la mchanga wa dhahabu. Kwa hiyo, naomba tuwe na kumbukumbu kwamba tuliilaumu sana Serikali kwamba haichukui hatua, sasa Mheshimiwa Rais amechukua hatua. Napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa sababu hatua hizi zikiendelea kuchukuliwa, uchumi wetu unakwenda kutengemaa na hatimaye maisha mazuri yaliyoahidiwa yanakuwa ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja.