Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la ajira za nje na ushirikiano wa kimataifa kwa Afrika na Afrika Mashariki ni kubwa nchini lakini kuna tatizo katika ushirikiano huu, nafasi za ajira zimekuwa zinatangazwa muda mwingine kwa kufichwa, wananchi wanakuja kushtuka watoto wa wakubwa ndiyo wameajiriwa kimataifa huku watoto wa maskini hawapati fursa hizi. Je, kupitia tatizo hili ni ubaguzi huu kati ya watoto wa maskini na matajiri, Serikali imejipanga vipi kuondoa ubaguzi na urasimu wa ajira za kimataifa? Usawa uko wapi, ni lini watoto wa maskini watafarijika katika Taifa lao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la uchakavu wa Balozi Nje ya nchi, Balozi zina hali mbaya, tunapoteza fursa za uwekezaji, Balozi zinadaiwa mapango ya nyumba za ofisi na nyumba za watumishi ziko hovyo. Kwa bajeti hii moja kwa moja haioneshi kwamba inaweza kumaliza changamoto hizi katika Balozi zetu za Zimbabwe, Mozambique, Botswana na South Africa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mpango wa Serikali kusaidia wanafunzi waliopo masomoni katika nchi korofi, hivi karibuni yamejitokeza matatizo kwa wanafunzi wanaosoma nchi za nje, huko waliko kuna ubaguzi, vita, mitafaruku na wafanyakazi wa ndani kuuwawa nchi za nje, kutokana na matatizo hayo Serikali hii ya CCM haijawahi kusaidia moja kwa moja. Mfano tatizo la unyanyasaji na usafirishaji wa wafanyakazi wa ndani nchi za nje. Je, nini mkakati wa Serikali kupitia bajeti hii ihakikishe inasimamia waajiri wanaonyanyasa Watanzania wenzetu inaonekana nchi haiko katika mstari wa kusaidia/kuondoa tatizo hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali/utawala huu utaacha ukandamizaji wa demokrasia nchini ili sasa hawa wawekezaji na ushirikiano wa nchi jirani na nchi za Ulaya ili waone kwamba kama watawekeza basi watakuwa katika nchi salama, lakini kadri siku zinavyoenda wawekezaji wanapungua? Je, hamuoni kuwa tunapoteza uchumi?