Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Khamis Mtumwa Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwengwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MTUMWA ALI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia, aidha napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wananchi wa Jimbo la Kiwengwa kwa kunichagua kwa kura nyingi kuwa Mbunge wa Jimbo hili tiketi ya Chama cha Mapinduzi. Pia napenda kuwashukuru Watanzania kwa kumchagua Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kuwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na Mheshiimwa Dkt. Ali Mohamed Shein kuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Waziri, naomba niguse mambo mawili, matatu ambayo yamezungumzwa katika hotuba ya Upinzani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wapinzani katika hotuba yao wamezungumza kwamba wana hofu ya kuvunjika kwa Muungano, mimi napenda kusema kwamba hofu hii wataendelea kuwa nayo lakini Muungano huu hauvunjiki utaendelea kuwepo, kwa maslahi ya Watanzania wakiwemo Wazanzibari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema ukweli Muungano huu umeleta faida nyingi kwetu, wengine tunaozungumza hapa tumekuwepo kwa tiketi ya Muungano kama siyo Muungano maana yake tusingekuwemo humu na tusingefika hapa kuzungumza na kuchangia mambo mbalimbali ambayo yanahusu mustakabali wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wameendelea kusema eti Muungano huu unalindwa na CUF na Maalim Seif, kama siyo wao Muungano huu usingekuwepo. Nataka niwahakikishie kwamba, Muungano huu unalindwa na Watanzania wote, Watanzania wa Zanzibar na Watanzania wa Tanganyika ndiyo wanaoulinda Muungano huu, siyo Maalim Seif na wana-CUF. Kusema ukweli Upinzani Muungano huu hawautaki, iweje leo waulinde, sisi tutasema Serikali ya CCM ndiyo itaulinda Muungano huu na tutahakikisha kwamba unadumu kwa maslahi ya Tanzania na kwa maslahi ya Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba yao hii, wamezungumzia haki za binadamu, eti wamesema Serikali ya Muungano imeivamia Zanzibar kijeshi na Polisi kwenye uchaguzi wa marejeo. Hivi Zanzibar ina Serikali yake ivamiwe kijeshi kivipi, wao wanachotaka kufanya wanataka kufanya vurugu, lakini nafasi hiyo hawakuipata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nalipongeza Jeshi la Polisi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa kusimamia uchaguzi wa marudio, kurejewa kwa hali ya ukimya, hali nzuri ya ulinzi na usalama wa hali ya juu. Wananchi wote walipewa fursa ya kushiriki katika uchaguzi ule.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wale ambao wamekataa wenyewe wasisingizie kwamba Zanzibar imevamiwa, waseme ukweli kwamba walishindwa kushiriki kwa sababu wanajua kwamba hawawezi kurejea katika uchaguzi ule kwa sababu CCM tutawashinda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, njama zao za kuiba kura tulizibaini na bahati nzuri Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kupitia Jecha alwatan akafutilia mbali uchaguzi ule na hatima yake tukarudia uchaguzi ambao halali na hatimaye wameshindwa kuingia uwanjani wametia mpira kwapani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nawaambia zile pesa za posho na mshahara wanaopata wawasaidie wale wenzao waliouza mashamba yao ya mikarafuu kwa ajili ya kugombea baadaye wakakaa nyumbani wakaambiwa eti wapumzike sasa hivi wanajuta kwa nini hawakuingia katika uchaguzi ule. Iliyobaki ni kelele na kuwapa matumaini mabovu Wazanzibari kwamba kesho eti Jumuiya ya Madola itamtangaza Maalim Seif itakuja kumuapisha, yaguju. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wamekaa wanasema eti wapewe nafasi wapumue, sasa hivi ndiyo wakati mzuri tumeshawapa nafasi wapumue nje ya Serikali. Kwa sababu walikuwepo ndani ya Serikali hakuna walichokifanya, walikuwa wanaijejea Serikali, hawana maendeleo waliyoyaleta. Wamepewa Wizara ya Afya wameshindwa kuleta hizo huduma walizokuwa wanasema, maana walikuwa wanasema hata panadol hakuna, hatimaye wameshindwa kufanya hivyo. Kwa hiyo, hawa bora wakae nje waone sasa hivi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein ikifanya kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa nijielekeze katika kutoa mawili, matatu kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Kwanza nampongeza kwa hotuba yake nzuri na mwonekano mzuri ambao aliusema hasa kwa nia ya kuyarekebisha yale mambo ambayo yanahusiana na Muungano yanayohusu masuala ya kifedha. Huu mgao wa fedha ni vyema sasa ukaangaliwa kwa makini.
MHE. MTUMWA KHAMIS ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mgao huu ukiangaliwa kwa makini utasaidia zaidi kudumisha Muungano wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika naomba nizungumzie Mfuko wa Jimbo. Mfuko huu unakuja Zanzibar kama ulivyo na ni vyema ukapangiwa utaratibu mzuri ili tuweze kuupata katika wakati mzuri kama wanavyoupata wenzetu huku Bara. Kwa sababu pesa zikifika kule zinakuwa zinachelewa, kwa hiyo, tunamuomba Mheshimiwa Waziri afuatilie na apange utaratibu mzuri wa fedha hizi ziweze kupatikana kwa wakati mzuri ili kuweza kuhakikisha maendeleo ya wananchi wetu yanapatikana kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ajira za Muungano, ni jambo muhimu sana kuangalia ajira hizi zinapatikana kwa usawa. Tukiwa tunapata ajira hizi kwa usawa hata wale vijana ambao wana mihemko na hawaelewi kuhusiana na suala la Muungano wataweza kuelewa. Ikiwa kuna utaratibu mzuri wa upatikanaji wa ajira hizi katika hizi taasisi za muungano itasaidia sana kuhakikisha kwamba Muungano wetu huu unadumu kwa sababu upungufu mdogo mdogo uliokuwepo ukifanyiwa kazi utaweza kusaidia kuhakikisha kwamba Muungano wetu huu unaimarika na unadumu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mazingira, naomba nimpongeze Waziri kwa jitihada ambayo ameichukua kwa kuanza kwa kasi mpya kuhakikisha kwamba masuala ya mazingira yanafanyiwa kazi vizuri. Napongeza pia hatua anazozichukua sasa hivi kwa kutembelea Zanzibar kwa kwa kuwa Kisiwa cha Zanzibar…
MHE. MTUMWA KHAMIS ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.