Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kupongeza kwa uwasilishaji wote mzuri. Naishauri Serikali kupeleka fedha zote zilizoidhinishwa na Bunge kwa wakati ili kukidhi matumizi ya balozi zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kukarabati au kujenga ofisi zake za balozi nchi husika ili kuondokana na upangaji aghali. Naishauri pia Serikali kufuatilia urasimu unafanywa na Mabalozi kuhusu wawekezaji wanaotaka kuwekeza Tanzania, wafungue milango ya Tanzania ya uwekezaji badala ya kuwapa masharti makubwa ambayo yanawakatisha tamaa wawekezaji.

Pia niishauri Serikali kufuatilia balozi zetu katika utendaji kwani vimekuwepo vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu kwa watu wetu wanaokwenda nje hali balozi zikishindwa kuwasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashauri pia Serikali kuangalia juu ya mipaka, mfano mpaka wa Tanzania na Malawi ambao una utata mpaka sasa hivi.