Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nami kupata nafasi ya kuchangia Wizara hii ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ninayo mambo machache nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu wake na watendaji wake wote katika Wizara kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi hili la upimaji wa ardhi, upangaji na urasimishaji wa makazi, wananchi wengi walikuwa wanalisubiri kwa muda mrefu sana uliopita. Kule kwetu Wilayani Mbinga zoezi hili limepokelewa kwa mikono miwili kiasi kwamba ukiangalia kwenye makadirio ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wametoka kwenye shilingi bilioni tatu mpaka shilingi bilioni tisa, lakini makusanyo yao mengi yanatoka kwenye upimaji wa mashamba, muitikio ni mkubwa kiasi kwamba tunategemea pia kuboresha uchumi wetu wa Mbinga kupitia mpango huu wa upimaji ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nichukue fursa hii kumpongeza Mkurugenzi wangu Gombo Samandito Gombo yeye ni mtaalamu pia wa Mipango Miji na ndiyo maana zoezi hili linakwenda vizuri kule Mbinga. Ziko changamoto, changamoto ya kwanza ni elimu, mapokeo ya zoezi lenyewe wananchi wengi walidhani wakipimiwa mashamba yao Serikali inakwenda kunyang’anya mashamba hayo, inakwenda kumiliki mashamba hayo. Changamoto ya pili ni ada za ardhi za mwaka, changamoto ya tatu ni namna ya kugharamia upimaji mpaka watu wakapata hati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa mara nyingine Mkurugenzi wangu alifanya hesabu, Mbinga tunapima kipande cha heka moja kwa shilingi 100,000 lakini bado kuna changamoto namna ya kwenda, mtu ana mashamba ya heka kumi ishirini, tumeshirikisha sekta binafsi wale ni wafanyabiashara wamepata tender, wangependa wapime kiasi kikubwa ili wapate zaidi. Kwa hiyo, unakuta wale wakulima wamelimbikiziwa madeni katika eneo hili la upimaji. Nitoe shilingi milioni tatu kwa mkupuo hapana, tunaongeza umaskini kwa upande mmoja kwa hiyo iratibiwe namna ya kutengeneza malipo ya gharama hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika zoezi hili yako maeneo ambayo watu waliona kama wanaonewa, kwa maana kwamba mapokeo yalikuwa watu wavunjiwe nyumba baadhi ya maeneo, kwa hiyo likaleta shida. Pale Mbinga Mjini maeneo ya Tangi la Maji kulitokea na Mkanganyiko huo mlijenga holela kwa hiyo inabidi tuwavunjie kabla ya mipango miji kuwafikia, ikawa shida, mtu huyu amekaa hapa miaka yake hamsini unamvunjia leo nyumba anakwenda wapi? Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri hili litolee maelekezo vizuri. Kama mnaamua kurasimisha makazi ya watu basi elimu ishuke wale Watendaji kule chini waielewe ili, zoezi lenyewe litekelezwe namna gani, vinginevyo kuna kauonevu ndani yake na pengine utekelezaji wake sasa unasuasua kwa sababu hiyo watu wanasita kwa sababu wanahisi sasa hapa nitavunjiwa, hapa nitahamishwa. Mheshimiwa Waziri kwa upande wa Mbinga mimi nilikuwa nataka kusema hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, iko changamoto kwa upande wa upangiliaji, upimaji na urasimishaji wa miji, mimi ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Msingwa kule Dar es salaam Kata ya Msigani. Tunalo zoezi hili, tunayo kampuni binafsi ambayo imepitia kwenu Wizarani, imepitia Halmashauri, tumeshafanya mikutano kadhaa, mapokeo ni mazuri sana na nitumie pia fursa hii kukualika Mheshimiwa Waziri baada ya kumaliza mikutano hii nitakualika kwenye mtaa wangu tukazindue mpango wa upangiliaji miji kule Kata ya Msigani, tutaleta barua rasmi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapokeo ni mazuri, changamoto iliyoko kubwa ni gharama hizi za upimaji, bei elekezi ni kweli Serikali imetoa lakini gharama za umilikishaji ni tatizo, Wizara hamjaziweka wazi, kuna tozo pale zipatazo tisa mpaka uje upate hati mjini, ndiyo maana hati nyingi hazijatolewa kwa sababu ya hizi gharama za umilikishaji. Ziko gharama pale zinahesabika, ziko tisa. Iko gharama ya kuchukua form, premium, ada ya hati miliki, lakini iko ada ya uandaaji wa hatimiliki, hati ya usajili na tunayo ada ya uandikishaji. Sasa tulifanya ukokotoaji pale kwenye Mtaa wangu wa Msingani Dar es Salaam…

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwenye kiwanja cha square metre 600 kinagharimu shilingi 873,000 ada ya umilikishwaji, acha ile ya upimaji kwa kampuni binafsi.

Kwa hiyo naomba Wizara muangalie upande huu, huo utatukwamisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante.