Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DANIEL E. MTUKA: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nafasi hii fupi nitazungumzia mambo mawili tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Wizara, nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri, niseme tu kwamba Wizara hii mmeibadilisha mmeitoa mbali mmeibadilisha, wataalam wa ardhi tunajivunia sana kwa kweli kazi mnayoifanya mko aggressive, lakini pia mna- confidence na lakini la mwisho ni wachapakazi, tunawapongeza kwa hilo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maombi mawili mafupi, ombi la kwanza niunge mkono pia Wabunge wenzangu, retantion scheme ile asilimia 30 ya makusanyo ya kodi ya ardhi, naomba ibaki kwenye Halmashauri isiende huko Hazina, kwa sababu ikienda kule hairudi haraka mnatuchelewesha sisi tunataka tupime viwanja, squatter zinatusumbua, ninaomba sana hilo Mheshimiwa Waziri wakati una wind up hebu liweke vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unalia hapa kwamba malengo hayakutimia kwenye kupima viwanja na wataalam umeshawasambaza kwenye Kanda, acheni tupime ardhi Wilayani huku kwenye Halmashauri mnazipeleka hizo pesa za nini huko, nilikuwa nataka kulisisitiza hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tuna ombi Manyoni, tunao upungufu wa watumishi. Wataalam wa ardhi tulionao pale Halmashauri wanatakiwa wawe 21 lakini wapo wa wanne tu, watafanya kazi gani? Squatter hizi zitaendelea pamoja na hayo tunajitahidi kweli tangu mwaka juzi mpaka sasa ninavyozungumza tumepima viwanja karibu 991 ambavyo tayari tunavigawa kule, kwa shida kwa kujibana bana lakini viwanja 1,400 tumevipima viko kwenye hatua za mwisho tunakamilisha cadastral survey kwa ajili ya kupata approve.

Mkeshimiwa Mwenyekiti, 220 tumefanya regulazation tunaanda hati tupo kwenye hatua za mwisho, watumishi wanne hawa tunajitahidi. Kama haitoshi tumejibana fedha kwa shida, tume-order GPS RTK sisi watu wa Manyoni inakuja na tumeshailipia, tunaomba basi mtusaidie mtuunge mkono, hatuna gari kwa hawa watalaam wa ardhi, Mheshimiwa Lukuvi tusaidie gari kama juhudi zote hizi tumejitahidi si mtuunge mkono jamani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, tunayo Sheria Namba 8 ya Mipango Miji ya mwaka 2007, tangu mwaka huo imetungwa lakini haina regulations hazijatungwa, inatekelezwaje hii sheria bila regulations? Naomba mjitahidi hii sheria itungiwe regulation zake. Tunasema kwamba planning ndiyo inayoanza, sasa mnafanyaje kazi bila regulations tangu muda wote ule?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni hili la ujumla, hebu tuitumie ardhi vizuri, ujezi wa horizontal ambao wa mtawanyiko siyo mzuri tunamaliza ardhi hii, ardhi itaisha Dar es Salaam kama tunge-opt vertical development tungekuwa tumeishia Magomeni tu pale. Ile population ya Dar es Salaam siyo watu wengi, lakini kila mmoja anataka amiliki kiwanja na eneo afuge mpaka kuku, siyo rahisi ardhi itaisha hii, tuende juu tusitawanyike tubakishe na maeneo ya kulima, tutalima wapi? Sasa kila mahali ni kujenga tu, haiwezekani lazima tu- plan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahi National Housing wanavyojenga, kwa mfano nimeona ghorofa za Wanajeshi hapa Dodoma hapa, ziko vizuri, na scheme zingine za kujenga hebu waende ghorofa mbili tu juu watoe mfano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache naunga mkono hoja, lakini retention scheme, ile fedha ibaki kwenye Halmashauri ili iwasaidie kupima viwanja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja, ahsante sana.