Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia Wizara hii ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na wenzangu kuwapongeza Waziri na Naibu wake pamoja na Watendaji wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri mnayoifanya.

Pamoja na kazi hii nzuri mnayoifanya naomba nielezee matatizo yaliyoko hasa katika Mkoa wangu wa Njombe nikianza na migogoro ya wananchi na watu wa TANAPA. Kwa mfano, nikiangalia maeneo ya Wanging’ombe, Kijiji cha Ruduga kuna tatizo la wananchi na watu wa TANAPA, mara kadhaa wamekuwa wakiwasumbua sana na kuna kipindi waliwakatia mazao yao.

Kwa hiyo, nimuombe Waziri kufika maeneo yale kutusaidia kutatua tatizo hili kwa sababu limekuwa ni tatizo la muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa sasa wametishiwa kwamba watatakiwa kuhama kwenye kile Kijiji cha Mpanga. Sasa wanakaa kwa wasiwasi wana hofu kubwa kwamba watahama na wana shida kwa sababu ya hofu hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee suala la migogoro katika Wilaya ya Makete. Katika Wilaya ya Makete kumekuwa na migogoro kati ya Hifadhi ya Kitulo na wananchi wa kijiji cha Misiwa. Watu wa hifadhi wameweka beacons kwenye mashamba ya wananchi wa maeneo yale ya Kitulo, wanasema kwamba wanapanua hifadhi. Hivyo, nimuombe Waziri kutusaidia suala hili angalau hawa wananchi kuwaondoa hofu maana yake nao sasa hivi wanashindwa kufanya uzalishaji kwa sababu wanaona wanaendelea kuingiliwa, mwisho wa siku hata mashamba yote yatachukuliwa, ninawaomba sana mtusaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba niongelee suala la migogoro Makete na Wanging’ombe. Kuna tatizo la mipaka kati ya Wanging’ombe na Makete, vilevile kuna tatizo kati ya shamba la Ludodolelo, kuna mwekezaji ambaye yuko katika shamba la Ludodolelo ambaye anawasumbua sana wananchi, sasa wanavutana kati ya wananchi na yule mwekezaji. Kwa hiyo, niwaombe Serikali mtusaidie mfike maeneo yale kusudi tuweze kutatua tatizo hili. Ahsante.