Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ni kitu muhimu sana katika nchi yetu na dunia nzima kwani kila kiumbe kinachoishi duniani kiko chini ya ardhi ambapo kumekuwa na changamoto nyingi ambazo zinaikabili Wizara hii ambayo ni lazima kuwepo na mikakati ya makusudi kumaliza changamoto hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya wakulima na wafugaji; suala hili limekuwa ni changamoto kubwa kwa nchi yetu ambayo imesababisha madhara makubwa sana ikiwemo vifo kwa wakulima na wafugaji na pia kwa wawekezaji hasa kama hakukuwa na ushirikishwaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la mipaka, ni vyema Wizara ikawa na utaratibu madhubuti wa kupitia upya mipaka ya maeneo mbalimbali ikiwemo vijiji na vitongoji lakini maeneo yaliyotengwa kwa uwekezaji pamoja na maliasili zote ili kuondoa migogoro mbalimbali inayoweza kujitokeza katika maeneo yetu. Upatikanaji wa hati miliki, suala hili limekuwa na changamoto kubwa hasa kwa wananchi wa vijiji ambao makazi yao hayajapimwa, na kumekuwa na urasimu mkubwa kwa maafisa wa ardhi katika Halmashauri mbalimbali nchini ikiwemo Mkuu wa Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upungufu wa Maafisa Ardhi kwenye Halmashauri ikiwemo Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga; nashauri Serikali kuongeza Maafisa Ardhi kwenye Halmashauri mbalimbali nchini ili kuondoa migogoro isiyo ya lazima. Kutolewa mafunzo kwa Maafisa Ardhi na Maafisa Mipango Miji ili kuweka ufanisi katika maeneo na kazi zao ambao hazitaleta usumbufu kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la upimaji wa ardhi, suala hili limekuwa na changamoto kubwa, lakini linatokana pia na maafisa ambao sio waaminifu kwa kujipatia viwanja ambavyo Halmashauri na Serikali kwa ujumla hazinufaiki kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upatikanaji wa hati kuchukua muda mrefu na kupelekea mianya ya rushwa suala hili limekuwa likiwakatisha tamaa wananchi ambao hawana hati miliki. Nashauri Serikali kufuatilia suala hili kwa ukaribu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba; kuna changamoto kubwa hasa kwa suala la gharama kwani gharama za nyumba zinazojengwa ni kubwa ambazo wananchi wakiwemo wa Mkoa wa Rukwa hawawezi kumudu kabisa nyumba zijengwe kulingana na jiografia husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji wapewe ramani ili wayajue maeneo yao. Hii kwa kiasi kikubwa itachangia kuondoa migogoro isiyo na sababu.