Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Wizara, kwa kazi nzuri mnayoifanya kutatua migogoro ya ardhi katika nchi yetu. Naiomba Serikali, kuendelea na juhudi ya kutatua migogoro ya ardhi katika Mikoa, Wilaya, Kata na Vijiji. Kuna migogoro ya kugombania mipaka kati ya wilaya na wilaya nyingine, mipaka ya kata na kata, kuna migogoro ya kijiji na kijiji. Ili kumaliza kabisa migogoro hii naishauri Serikali kupima ardhi yote ili kupata matumizi bora ya ardhi nchini. Kuna tatizo la ujenzi holela katika miji yetu naishauri Serikali, kusimamia upangaji wa miji yetu, kuwa na master plan ya miji na kuwaelimisha watu kufuata sheria ya mipango miji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iwapimie mashamba wakulima ili kila mkulima kuwa na shamba ambalo limepimwa na analipia. Katika upimaji naiomba Serikali iwapimie wananchi kwa bei nafuu ili hata watu wenye vipato vidogo, waweze kusajili mashamba yao na kupimiwa. Serikali ipunguze bei ya upimaji wa viwanja, wananchi wanashindwa kununua viwanja vya Serikali sababu bei ipo juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.