Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hotuba ya Waziri kwa maandishi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze Waziri na Naibu Waziri wa Ardhi kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuhakikisha ardhi inawanufaisha Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo baadhi ya mambo ambayo lazima tuseme ili kusaidia kusukuma Wizara hii muhimu kwa Watanzania. Ofisi za Ardhi za Kanda, mpango huu ulipoanzishwa ulikuwa na nia ya kusogeza huduma karibu na wananchi. Kanda ya Kati, Mkoa wa Morogoro ndipo yalipokuwa Makao Makuu na Wizara/Serikali ilijenga Ofisi za Ardhi za Kanda kwa gharama kubwa. Ofisi hii zimesaidia sana chini ya Kamishna imepunguza kwa kiasi fulani migogoro na malalamiko ya ardhi hususan Mkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri amesema katika hotuba yake, Serikali imebadilisha/kuhamisha Ofisi ya Kanda Morogoro na kuhamishia Dodoma, hii si sawa. Kwa kipekee Mkoa wa Morogoro utazamwe kwa namna nyingine kutokana na kukithiri kwa migogoro ya ardhi ya mara kwa mara ambayo imegharimu maisha ya watu kwa kusababisha vifo na majeruhi hasa katika Wilaya za Kilosa, Kilombero, Mvomero na Morogoro Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukosefu wa vifaa vya kupimia ardhi; Maafisa Ardhi wanafanya kazi katika mazingira magumu ambapo unakuta mfano, Mvomero ina kifaa kimoja tu cha kupima, hali inayosababisha ucheleweshaji wa upimaji wa ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kero ya bomoa bomoa; katika vitu vinavyolalamikiwa na wananchi ni uvunjaji wa nyumba za wananchi wanaojenga kwa jasho kwa vibali vyote kwa kuzingatia masharti mbalimbali hasa waliopo kando ya barabara ambapo hivi sasa Serikali kupitia TANROAD wanakusudia kuvunja nyumba za wananchi na barabara ya Dar es Salaam, Morogoro kwa zaidi ya mita 20 kila upande.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hizi zinafanyaje kazi Ardhi na Miundombinu? Kwa nini kusiwe na mpango wa kuzuia wananchi kujenga badala ya kusubiri wananchi wajenge kisha waje kubomoa. Yapo maeneo ambayo wananchi nao wamepelekewa huduma muhimu kama maji, umeme na kadhalika