Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa kwenye Mabaraza ya Ardhi, Vijiji na Kata, ni vurugu na mambo ya ajabu. Mfano, hukumu inampa ushindi mtu kwa kuwa alileta mashahidi wengi kuliko upande wa pili. Wananchi wanazungushwa sana katika rufaa hawapewi hukumu mpaka anakata tamaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara imeruhusu makampuni binafsi ya upimaji waweze kushirikiana na Halmashauri zetu kibiashara/Huduma. Watendaji wa Halmashauri bado hawataki kushirikiana na Makampuni hayo mfano ni Halmashauri ya Biharamulo. Tunaomba uharakishwaji wa utatuzi wa migogoro mikubwa ambayo nimeorodhesha tayari. Mfano Mgogoro wa Jeshi na Kijiji cha Rwebya unasumbua sana.