Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Wizara hii, bado napenda kuikumbusha Serikali kupitia Wizara hii kumaliza kulipa fidia Kurasini. Tathmini imefanywa muda mrefu lakini hadi leo wananchi wale hawajalipwa fidia hiyo pamoja na mapunjo yao. Fidia inapokaa muda mrefu huleta matatizo kwa raia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri awahimize NHC kuharakisha makubaliano yetu ya kujenga jengo la biashara ya fenicha pale Keko.