Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na wimbi kubwa sana la migogoro ya ardhi hapa nchini; migogoro ya wakulima na wafugaji na migogoro hii inasababishwa na wawekezaji hasa maeneo ya hifadhi

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri ni Kata ya Kyanyari, wananchi wanateseka sana wamefukuzwa kwenye makazi yao kwa lengo la Serikali eti kupisha hifadhi. Wananchi hawa toka wamefukuzwa wanahangaika sana hadi sasa hawana makazi maalum ya kuishi na hawana matumaini ya maisha yao, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha inawapa makazi ya kuishi wananchi hawa pamoja na mashamba (maeneo) kwa sababu maeneo waliyofukuzwa ndiyo yaliyokuwa yanawasaidia kwa makazi pamoja na mashamba lakini kwa sasa hawana sehemu ya kulima na wananchi hawa walitegemea sana kilimo ili kuinua kipato cha maisha yao ya kila siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwaondoa kwenye maeneo yao kumewaathiri sana wananchi wa Kata ya Kyanyari wanateseka na kutia huruma. Napende kuishauri Serikali iwe inawatengea maeneo mbadala kabla ya kuwahamisha wananchi kwa lengo la kupisha hifadhi tofauti na sasa kuwahamisha wananchi bila kuwatengea maeneo kwani wanapowaondoa bila kuwatengea maeneo wanategemea wananchi hao watakwenda wapi? Pia Halmashauri husika ihakikishe inasimamia na kutetea haki ya wananchi wake katika maeneo husika.