Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi nchini ni moja ya kero kubwa inayokwamisha maendeleo ya kiuchumi na ya watu wetu. Migogoro hii imedumu muda mrefu na kama nchi lazima tunatakiwa kuchukua hatua sasa. Ili kumaliza migogoro hii Serikali ni lazima ihakikishe ardhi yote imepangwa, imepimwa na kumilikishwa kisheria. Kuhusu migogoro ya mipaka kati ya Mkoa na Mkoa, Wilaya na Wilaya na Kijiji na Kijiji, nishauri Serikali kufanya utaratibu wa kutafsiri GN zilizounda maneno hayo ili haki itendeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Karatu inayo mashamba 40 ya wawekezaji (Mikataba). Mengi ya mashamba hayo hayajaendelezwa kwa kiwango cha kuridhisha na yamekuwa chanzo cha migogoro. Shamba la Tembo na Tembe lenye ekari 562 na 545 ambayo yote yametekelezwa kwa chini ya 50% yamekuwa kero kubwa katika Wilaya ya Karatu. Naomba Serikali ichukue hatua ya kuyachukua mashamba hayo au hata sehemu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shamba la Acacia Hill, lenye ekari 1556, nalo tunaomba sehemu yake irudishwe kwa wananchi maana nalo limeendelezwa kwa chini ya asilimia 50%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, shamba la Bendhu Limited lenye ekari 472 limetelekezwa baada ya mmiliki wake kufariki. Tayari Halmashauri ya Wilaya imeshaomba shamba hilo kufutiwa umiliki na lipewe wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niiombe Wizara iongeze wataalam wa ardhi na vifaa katika Wilaya ya Karatu.