Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia katika suala hili. Kwa sababu ya muda naomba nianze kumpongeza Waziri wa Ardhi, Mheshimiwa Lukuvi na Naibu wake Mheshimiwa Angelina Mabula, pamoja na wataalam wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayofanya kukabiliana na changamoto mbalimbali za ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wangu wa Kijiji cha Lukonde wana matatizo makubwa, wanapata kipigo kutoka kwa mwekezaji wa Shamba la Kidago alilopata kwa njia ambazo sio halali toka Uluguru Toiler aliyewanyang’anya wananchi bila ya kufuata taratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huu ni mkubwa sana kwa Kijiji na Kitongoji cha Kidago, Lukonde, nyumba zao zaidi ya sitini (60) zimechomwa moto zaidi ya mara tatu tofauti na kwa miaka tofauti na kuchoma mazao yao na mfugaji huyo aliyepewa ardhi hiyo. Ombi langu, Mheshimiwa Waziri baada ya Bunge hili kumalizika naomba afike kidogo na kujionea hali halisi na kuwasaidia wananchi hawa ili waweze kuishi katika nchi yao kwa amani na usalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nataka kushauri Serikali kutenga Bajeti na kupima ardhi yote ya Halmashauri ya Morogoro Vijijini. Kwa kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi, kupanga matumizi ya ardhi kwa ajili ya wakulima na wafugaji na hifadhi na kujenga miundombinu ya kiufugaji kama majosho, mabwawa katika maeneo ya wafugaji na kutoa elimu kwa wafugaji kufuga kisasa na umuhimu wa kuwa na mifugo kutokana na ukubwa wa ardhi waliyonayo na miundombinu ya mifugo iliyopo sehemu husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuwaondoa wafugaji wavamizi waliokuja Morogoro vijijini na Morogoro kwa ujumla bila kufuata sheria Kanuni na taratibu za kuhamisha mifugo toka sehemu moja kwenda sehemu nyingine na kuharibu mazingira, mashamba ya wakulima, vyanzo vya maji na barabara zetu tulizojenga kwa gharama kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante.