Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamuhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania)

Hon. Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba (Intergovernmental Agreement – IGA) baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamuhuri ya Uganda kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (East Africa Crude Oil Pipeline – EACOP) kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga (Tanzania)

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na mimi kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia kwenye hoja iliyo mbele yetu. Awali ya yote nimshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai mimi na sote tuliomo humu ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza kabisa niishukuru na kuipongeza sana Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufanikisha mradi huu wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu ni muhimu sana kwetu, na wote tunafahamu kwamba kulikuwa na kama mashindano hivi kati ya nchi hizi za Afrika Mashariki kuhusu bomba lipite hili wapi, lakini baada ya Serikali ya Tanzania kufanikiwa na mradi huu kuzinduliwa kule Tanga kwa kweli imekuwa ni faraja kubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Chemba bomba hili linapita si chini ya kilometa 170 kutoka mpakani na Kiteto hadi mpakani na Singida. Linapita Mrijo, Chandama, Songolo, Goima, Paranga, Farqwa, Kwamtoro, Ovada hadi Kinyamshindo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu, wananchi ni vizuri wakaelezwa mapema ili wasiendeleze baadhi ya maeneo yao kwamba bomba hili litapita wapi. Lakini pia itakuwa vyema sana kwa wale ambao wataguswa na eneo lao kuchukuliwa wakalipwa fidia yao stahiki kwa kipindi muafaka, litakuwa limewasaidia sana. Pia ni mradi mzuri kwasababu ukiangalia kwa siku, Mama Tibaijuka alikuwa anajaribu kupiga hesabu pale na mimi nimejaribu kupiga hesabu hapa kwamba kwa siku Tanzania tunapata dola 2,708,325, it’s a huge amount of money na hii hela itatusaidia sana.

Sasa mimi ombi langu ni kwamba ni vizuri Waheshimiwa Wabunge pamoja na Madiwani wa maeneo husika. Kwa sababu nimeanza kuona kuna tatizo moja dogo tu na ningeomba kuishauri Serikali; kwamba wanawashirikisha sana Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya. Hawa ni watendaji wa Serikali, lakini wanaoulizwa maswali ni Wabunge na Madiwani. Mbunge ukienda mahali wananchi wanakuuliza hebu tuambie bomba likipita hapa sisi tutafaidika nini? Mbunge unashindwa kutoa majibu kwasababu aliyekwenda kuhudhuria hivi vikao vingi vingi hivi ni Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa na nashukuru sana baadhi ya Waheshimiwa Wabunge ambako bomba hili linapita walishirikishwa kule Tanga.

Ningetoa rai kwamba sasa tunapokwenda kwenye process hii ya ku-finalize hili suala Waheshimiwa Wabunge na Waheshimiwa Madiwani wa maeneo husika ni vizuri wakashirikishwa. Seriakli msi-ignore sisi ni wawakilishi wa wananchi tu lakini sisi ndiyo responsible kwenye maswali ya wananchi. Kwa nia njema tu, tushirikisheni ili na sisi twende vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, kiwango hiki cha fedha tutakachokipata ni kikubwa kidogo. Maeneo mengi bomba hili litakapopita vijiji vingi havina maji, na ndiyo maana mimi na Wabunge wenzangu wa Mkoa wa Dodoma, Manyara na hata Tanga bomba lilikopita ndiko ilikopimwa barabara ya lami kutoka Handeni - Kiberashi - Kibaya - Mrijo, Chemba - Donsee - Farqwa - Porobanguma - Kwamtoro mpaka Singida. Kwa hiyo nadhani ni wakati muafaka saa Seriakli ijenge ile barabara kwa kiwango cha lami ili hata usimamizi na usalama wa bomba hili uwe mzuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema haya nakushuru sana na ninaipongeza sana Serikali na naunga mkono. Jambo hili ni jambo jema sana kwentu, ni jambo jema kwa Watanzania wote tuungane ili tufike pale Mheshimiwa Rais wetu anataka tufike pamoja na chama chetu, chama tawala. Ahsante sana.