Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie fursa hii kuwapongeza Waheshimiwa Mawaziri ambao wamebaki kwenye nafasi zao na Mawaziri wapya na Naibu Mawaziri walioteuliwa na Mheshimiwa Rais katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri la hivi karibuni, niwatakie kila la kheri katika kutimiza wajibu wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 wakati tunajadili mpango ndani ya Bunge hili nilimtahadhalisha Waziri wa Mipango nikimwambia kwamba mpango unaouleta hatutofikia economic growth ya seven percent kwa sababu Mpango huu unaacha sehemu kubwa ya Watanzania nje, sio mpango inclusive. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 wakati tunajadili Bajeti nilirudia maneno haya na mwaka huu wakati tunajadili Bajeti nilimwambia kuna conflict kati fiscal policy ambazo Wizara za Fedha inazisimamia na monetary policy these two policies zinapambana zenyewe na matokeo yake yataonekana. Naomba nitumie takwimu zifuatazo kama alivyosema Ndugu Serukamba uchumi wowote duniani una mirror (kioo) na kioo cha uchumi wowote unaokuwa ama unaosinyaa ama unaoshuka moja ni financial Institution, mbili ni
trade, tatu ni stock exchange. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, personal landing mwaka 2015 ilikuwa ni 50% today ni 8.9 percent. Trade ilikuwa ni 24% this is a landing to trade ilikuwa 24%, leo ni 9% na maneno haya siyatoe kwingine ni ripoti za BOT na quarterly report ya BOT ya inayoishia Juni, lakini taarifa zingine ni mwongozo wa Bajeti alioleta yeye na ni mpango wake aliouleta yeye. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, agriculture leo ni negative nine from six percent land capacity ya mwaka 2015, manufacturing from thirty percent landing to three percent, transport and communication from twenty four percent landing to negative twenty five, bulding from twenty two to sixteen. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, our economy it is said inakua, ukisoma projection ni 6.8. Lakini taarifa ya mwisho ya economic bulletin for the quarter ending June, 2017 imetuambia ni 5.7 sio maneno yangu. Food inflation lets go categorically its 10.1 percent sio maneno yangu taarifa ya Septemba ya BOT hii hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, why are we facing this, it’s not a rocket science. Waziri wa Fedha ukurasa wa sita wa Mpango unasema export naomba iingie kwenye Hansard ya Bunge. Nimeangalia taarifa za monthly za BOT toka mwaka 2011 mpaka Septemba mwaka huu, for the first time in the history hamjaweka performance export and imports, why? Mnaficha nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, alisema ndugu Abdulrahman Kinana, wakati anaongea katika function ya Kigoda pale Universty of Dar es Salaam alisema hivi namnukuu, Katibu Mkuu wa chama chetu; “Jambo muhimu la kiongozi ni kusikiliza watu wake.” Viongozi hamna monopoly right wisdom, viongozi hawana monopoly right ya trueth, viongozi hawana monopoly right ya wao wako sahihi kila siku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna jambo muhimu katika kupanga mipango yoyote duniani kama takwimu. Ukurasa wa saba wa document ya mapendekezo ya Mpango unaonesha mwenendo wa ukuaji wa Pato la Taifa toka mwaka 2011 hadi 2017, 2011 our growth was 9.1 percent. Today its projected 6.8 lakini as per this report ni 5.7.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ninukuu maneno yafuatayo , ukurasa wa saba unasema; kufikia Juni, 2017 export zilikuwa zimeshuka kwa asilimia 29.8. Lakini Waziri anatupa a counseling statement kwamba matarajio ni kurejea kwa exportation, kuongezeka eti kwasabbu tunajenga kukuza viwanda sasa twendeni tukasome hivyo viwanda vya export, siyo maneno yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Mpango Waziri ametaja viwanda, ukurasa wa 26, kiwanda cha kuchenjua madini kulichopo Geita, kusindika nyama Kisivani Shinyanga- Mitobotobo Farmers Company Limited, kuzalisha mafuta ya kula, kuchambua pamba, kiwanda cha kuzalisha vifungashio (Global Packing), kiwanda cha kuzalisha vinywaji baridi (Sunny Food Company - Sayona) hivi ndiyo tuta-export kurudisha asilimia 29. Kuzalisha bidhaa za ujenzi; brother tumeahidi kuondoa umaskini wa watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo maneo yangu mimi na- quote maneno ya Waziri wa Mpango. Twendeni ukurasa wa 68 - sekta ya kilimo look at this, hii ndiyo sekta imeajiri asilimia 65 mpaka 70 ya wananchi wetu na tafiti zilizofanyika Watanzania zaidi ya asilimia 80 walioko kwenye sekta ya kilimo yaani ile 70 percent, 80 percent ya hiyo 70 percent inafanya kazi mbili (dual), inalima na inafuga kama siyo ng’ombe, mbuzi, kuku, bata na vitu vya namna hiyo, anafanya dual, now look at this two things.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya mifugo, Serikali imepanga kufanya uhimilishaji, tunahimilisha, kufanya insemination ng’ombe 450,000. Lakini tunapanga kuzalisha chakula hay. Hay ni yale majani ya ng’ombe, tunapanga kuzalisha chakula kwa mwaka hey 445,000 kitakwimu hay moja ina uzito wa kilo 25, chakula hiki ukikigawa kwa siku 360 kinalisha ng’ombe 1,600 huku unapanga kuzalisha ng’ombe 400,000 lakini unaandaa mpango wa chakula ng’ombe 1,600. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa Wabunge wamejadili suala la kilimo, hakuna sehemu Waziri wa Kilimo ana-plan kuanzisha price stabilization ya mazao ya chakula. Leo kuzalisha kilo moja ya mahindi, gharama ya shambani ni shilingi 357, haya siyo maneno yangu, it is scientifically proved, halafu huyu mkulima anayetumia shilingi 357 kuzalisha kilo moja ya mahindi bado gharama ya kupeleka store, gharama ya kuweka mifuko, gharama ya kuweka dawa halafu atakapoweka store yake kuna kauli inasemwa hapa walanguzi ndiyo wana mahindi, this is total misconception ya business principal. Kote duniani kuna producer, kuna distributor, kuna retailer kwahiyo unataka kuniambia mimi ninayelima Nzega-Nata Mahindi yangu niyabebe, niende nikayauze Nairobi? Kuna intermediaries and this is the duty of your fiscal mono-policies kufanya intermediaries wafanye biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano mwingine, profitability ya financial institution imeshuka over 50 percent, Waziri ana hoja moja dhaifu sana anaitumia ndani ya mipango. Money circulation imepungua kutoka bilioni 222 mpaka bilioni 12 na hoja anayosema ni nini? Matumizi yasiyokuwa ya lazima ya Serikali yamepungua. Sasa najiuliza bajeti ya recurrent imepungua? Kutoka mwaka 2011, 2012, 2013 imepungua recurrent budget? No, spending ya government ipo, kwa hiyo nilitarajia kwamba itakuwa wisely tutaiona imeleta positive impact, lakini hakuna. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ushauri wangu kwa Waziri wa Fedha Mheshimiwa Dkt. Mpango narudia this is the third time, naheshimu your academic background, sijawahi ku-doubt. Kaka hauwezi kuondoa umaskini wa nchi hii bila kuwekeza kwenye kilimo, never. Hauwezi kuleta mapinduzi ya viwanda bila kuwekeza kwenye kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkulima wa nchi hii ndiyo kageuka punching box ya nchi hii. Tuna-control inflation ya chakula kwa gharama ya mkulima, how come? Haiwezekani, hatuwezi kufanikiwa kwa namna hii. Yaani sisi tunadhibiti mfumuko wa bei kwa kumtia umasikini mkulima, aina gani za economy hizi? (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikupe mfano mdogo tena aangalie, hatuwezi kuondoka kwenye umaskini kama mawazo ya Wizara ya Fedha hayatakuwa ni productive oriented badala ya kuwa tax base approach. Angalia Mpango huu unakuwa financed namna gani. Waheshimiwa Wabunge tuchukue document ya Mpango muusome how are we going to finance Mpango. Page number 29 ya muongozo wa maandalizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilindie dakika zangu dakika moja tu. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri anasema kwamba how to finance, anazungumzia kwamba ata-improve EFD machine, ataanzisha maabara ya TRA, it is all about tax base approach. Haumsikii anasema kwamba tutawekeza bilioni moja kwenye kilimo cha mahindi ili tuweze ku-yield X hausikii, hauwezi kukamua maziwa ya ng’ombe usiyemlisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia VAT, Pay As You Earn zimeshuka hazifikii target aliyojiwekea kwenye bajeti ya 2017 na hapa anasema kwamba makampuni yamepunguza wafanyakazi an unajua ni kwa nini? Is not a rocket science, tulimshauri kwenye Kamati ya Bajeti kwamba unaongeza exercise duty kwenye TBL utapunguza uwezo wa uzalishaji wa hawa watu, hakusikia! Tumemwambia kwenye Kamati ya Bajeti I was there. Tumemwambia Waziri wa fedha unaua viwanda vya soft drink kwa ku-impose 10 percent eti kwa udhaifu wao TRA wa kusimamia sukari inayoingia wameweka asilimia 10 tena on top kwa hiyo Coca cola akiingiza sukari kwenye nchi hii analipa 25 percent instead of 15 percent, what kind of economy is this?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge hasa wa chama changu, tumepewa dhamana ya nchi hii na Watanzania, let not allow mistake za Waziri Mpango kuharibu nafasi ya kuchanguliwa kwa Rais wetu mwaka 2020. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, samahani nikupe mfano mdogo, kampuni zote za vinywaji baridi zilikuja mbele ya Kamati ya Bajeti na sisi tukawaita Wizara ya Fedha, hawana capacity ya kwenda kukagua bonded warehouse, hawana capacity hiyo madhara yake unajua wamefanya nini? Wameamua kuanzisha kodi mpya ya ku-withold. Sasa hivi private sector inadai TRA over eight hundred billion shillings za returns on tax, hawalipi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Wana-sufocate, this is very wrong na mimi nimalizie samahani, kama Waziri wa Fedha hatobadilika hatuwezi kutoka hapa.