Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Kwanza kabisa nitoe pongezi kwa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa hotuba nzuri ambayo imegusa maeneo strategic kwa ajili ya kulisaidia Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaongea kwa ufupi sana kwasababu haya yaliyoandikwa kwenye Mpango ambayo tumeelezewa na Mheshimiwa Mpango ni masuala ambayo yamekuwa yakijirudia, kwa hivyo tusipoteze muda kuendelea kurudia mambo ambayo tumekuwa tukiyarudia mara kwa mara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala moja la msingi sana Mheshimiwa Mpango naomba utakapokuja kuhitimisha unisaidie kulijibu nalo ni kuhusu umakini wa uandaaji wa Mpango. Huu Mpango unalenga kutekeleza Dira ya Taifa 2020/2025. Nilichokuwa nakitegemea ni Mpango huu kuonesha una lengo la kutekeleza Dira ya Taifa ya 2020/2025 kwa asilimia ngapi ili ije kuwa rahisi kuhoji.

Mheshimiwa Mpango wewe unajua, Mpango unapokuja kuleta humu Bungeni ni lazima uwe smart kwa maana aya lazima uwe specific, measurable, uwe realistic, uwe attained na uwe frame timed. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri ni Kenya. Kenya wanapokuja kuanda Mpango wanakuwa very serious. Unakuta wanaadika kwamba Mpango huu umelenga inapofikia wakati fulani ajira mpya zitazaliwa kwa asilimia kadhaa, hiyo inakuwa inasaidia tunapokuja kurudi humu ndani kuangalia tumefikia wapi na tumetokea wapi, nafikiri hili litakuwa ni tatizo la uhaba wa wataalam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mpango ambao unakuwa wanaleta Bungeni kuwa na mapungufu kama haya ndiyo maana mambo mengi yanakuwa hayaendi sawa sawa, ndiyo maana Taifa hili bado linaendelea kuwa katika mazingira magumu, wananchi wanakuwa wanaishi maisha ya kimasikini, maisha ya mateso, ukata ni mkubwa kweli kweli na hili mnaweza mkalikataa lakini ni kitu ambacho kimekuwa proved. Mna mamlaka kubwa ambazo zinahusika na tafiti mbalimbali, mfano, nimeona katika ripoti ya BOT Juni, 2017 na Juni, 2015 inaonesha mzunguko wa fedha umeporomoka kutoka asilimia 15 mpaka negative three percent ambacho hiki ni kiwango kikubwa cha run rate.

Mheshimiwa Mwenyekiti, BOT pia wanaonesha kwamba mikopo isiyolipika yaani non-performing loans imengonezeka kutoka asilimia tano mpaka tisa na hii ndiyo sababu kubwa ya mabenki yetu ku-collapse.

Mheshimiwa Mwenyekiti, World Bank Report ya mwezi huu imeonesha pia kwamba urahisi wa kufanya biashara yaani easy of doing business, Tanzania tumeporomoka kutoka nafasi ya 132 ya mwezi huu mpaka 137. Deni la Taifa ambalo linapaa kwa kasi ya ajabu linaongezeka kwa asilimia 17. Mheshimiwa Dkt. Mpango kwa hesabu ya kawaida tu kama deni linakuwa kwa asilimia 17 na uchumi unakua kwa asilimia 6 katika hali ya kawaida ni vigumu kulipa deni hili kwasababu huwezi kushindanisha baiskeli na bodaboda. Deni linakwenda kwa speed kubwa sana ambayo inakuwa siyo ya kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali na viongozi wake mmekuwa mkijinasibu mara kwa mara kwamba nyie ni Serikali ya watu wanyonge, ninyi ni Serikali ya watu mnaojali maslahi ya watu maskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 70 ya wakulima wa Kitanzania asilimia 75 ni wanawake, sijaona effort zozote za Serikali za kuweza kusaidia hawa wakulima wa Taifa hili hasa katika suala kubwa la mbolea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa napitia report ya Poverty and Human Development ambayo imeonyesha kwamba kwa wastani, mwananchi/mkulima wa Tanzania anatumia kilo tisa kwenye ekari moja ya shamba lake, lakini kwa nchi ndogo kama Malawi, mwananchi wa kawaida kwa wastani anatumia kilo 27 kwa ekari moja. Sasa ninashindwa kuelewa na natafuta reflection ya Serikali ambayo inajinasibu kwamba yenyewe ni Serikali ya wanyonge, natafuta reflection ya matendo yake na hawa wanyonge. Reflection ya Serikali ya wanyonge haipo kwenye kujenga kiwanja cha ndege wapi kule?

Chato! Reflection ya Serikali ya wanyonge haipo kwenye kununua bombadier ambazo hata uwezo wa kusimamia bado ni mdogo zaidi ya kuingiza hasara tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, reflection ya Serikali ambayo inajinasibu kwamba ni ya wanyonge sitegemei kama inaweza ikawaumiza sekta binafsi kwa sababu wote humu ndani tutajua umuhimu wa sekta binafsi katika maendeleo ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hebu tujaribu kuwa wakweli, hebu tuwasaidie hawa Watanzania, ninyi mnafahamu namna ambavyo mambo yanakwenda ambavyo siyo vizuri, lakini mnashindwa kusema hapa. Mshaurini Mheshimiwa Rais vizuri na nimefurahi kuona baadhi ya Wabunge wa CCM wamefunguka na wameonyesha concern yako ka Mheshimiwa Dkt. Mpango. (Makofi)

Mheshimiwa Dkt. Mpango, ukweli ni kwamba kama haya unayoambiwa hautayazingatia huko mbele ya safari kila kitu kitakuja kukurudia wewe, kwa sababu nchi inaporomoka. Ukiangalia Mheshimiwa Mkapa alivyokuja alikuta deni ni kubwa sana akalishusha mpaka ikawa trilioni 10, akaja Mheshimiwa Kikwete akaacha deni la trilioni 45 sasa kipindi kile kama mnakumbuka vizuri mwaka jana nilitoa maelezo binafsi kuhusiana na Deni la Taifa kutoa angalizo kwa Serikali na ninsahukuru na wewe ulikuja ukatoa maelezo kwa kuonesha concern yako kwamba umeyakubali na unayafanyia kazi, lakini cha kusikitisha ni kwamba ile concern ambayo uliionesha. Mheshimiwa Mpango unakataa, lakini tulizungumza na uliniambia. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natamani kuona Taifa la Tanzania ambalo kwa muda mrefu sana limekuwa ni Taifa la kimasikini tunaliangalia kwa jicho la tofauti katika kuleta maendeleo. Kama nilivyotangulia kusema kwamba sitakuwa na mengi ya kusema maana mengi tumeshayasema kwenye Mipango mingine iliyopita kwahiyo haya hata nikiendelea kuongea tutaendelea kurudia tu mambo ni yale yale hakuna kinachobadilika, hakuna kinachofanyika, kinachopangwa hapa sicho kinachofanyika, tunajadiliana mengine, yanafanyika mengine. Ukifuatilia matumizi ya pesa nyingi nyingine hazipitishwi na bajeti ambazo tunakuwa tunazipanga hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.