Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Freeman Aikaeli Mbowe

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Hai

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi leo nichangie kidogo mambo machache ya msingi ambayo nafikiri ni vyema tukakumbushana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira ya kawaida, ya namna utawala wa nchi yetu ulivyo Chama cha Mapinduzi kina dhamana kubwa kwa sababu ndicho chama kilichozalisha Serikali. Lakini wakati wa uchaguzi, wakati tayari imeshatoka ilani ni Chama cha Mapinduzi tulisikia kauli yenye ukakasi, badala ya kuwa Serikali ya Chama cha Mapinduzi mkaona raha sana kujiita Serikali ya Magufuli. Juzi katika ziara ya Mheshimiwa Rais amerudia kauli hiyo akisema CCM kuna majizi, kwenye vyama vya siasa kuna majizi alichanganya vyama vyote, vyote vya upinzani na chama chake akasema ndio sababu yeye anasema Serikali ni ya kwake. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunajiuliza hivi tuna Serikali ya Chama cha Mapinduzi, chama kinachosimamia Serikali yake ama tuna Serikali ya mtu, anajisimamia mwenyewe. Napata wakati mgumu sana ninaposikia Wabunge wa Chama cha Mapinduzi, Wabunge wenzetu wanajirasibu Serikali yetu ameshawaambia Serikali ni yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimesikia michango ya Waheshimiwa Wabunge wote wa pande zote mbili nimshukuru sana Mheshimiwa Bashe na Mheshimiwa Serukamba wamekuwa honesty na hatutaisaidia nchi hii kwa kuwa wanafiki, tutaisaidia nchi hii, tutaisaidia Serikali yetu, tutawasaidia wananchi wetu wote kwa kuwa wakweli, kuwa critical kwenye mambo ambayo tunafikiri ni ya lazima, tupongeze pale ambapo tunafikiri kuna haki ya kupongeza tuko tayari kupongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wakati tunapokosea tusipoikemea Serikali, tusipoiambia Serikali ukweli na wale wanao-criticize wanaonekana wana stahili ya kufa, wale wanaikosoa Serikali wanaonekana wana stahili ya kuumizwa, hatutafika. Chama cha Mapinduzi, chama chochote cha siasa kikifikia hatua ya kutokutaka ushauri, kikifikia hatua ya kuweka pamba masikioni kutokusikiliza watu wanasema nini, chama hicho hata kingekuwa kina nguvu kiasi gani za kijeshi lazima kitakufa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo, naomba Chama cha Mapinduzi kifanye wajibu wake, mtanisamaehe, nimefuatilizia ndani ya vikao vya Chama cha Mapinduzi kama hata mambo haya yanajadiliwa kwenye vikao vya chama. Lazima tuambiane ukweli ninyi mna dhamana kuliko sisi, sisi ni wapinzani lakini ninyi ndio watu ambao mmepewa dhamana ya nchi hii maumivu yanapotokea kwa wananchi nyinyi mko responsible kuanzia Rais ninyi Mawaziri, Wabunge wa Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninachokiuliza ni kwamba tuna mfumo upi? mmesimama wapi kwenye msingi wa kiitikadi? Ninachokiona kinachofanyika kwa juhudi sana ni kujaribu kulirejesha Taifa hili kwenye ujamaa. Ndugu zangu policy za ujamaa zinapendeza sana na ni tamu sana kuzizungumza, lakini ukweli wa uhalisia wa hali halisi ya binadamu inakwambia tukijaribu kung’ang’ania siasa za kijamaa we are bound to fail. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefanya makusudi nika- tweet asubuhi jana asubuhi nikizungumzia kuhusu suala la mahusiano ya Serikali na private sector. Nika-tweet halafu nione reaction ya watu watasemaje. Wakajitokeza watu wengi wakisema wapinzani mnajifanya ninyi mna mawazo mazuri sana, lakini nilichokuwa nakisema hatutajenga uchumi wa nchi hii kwa kutumia bunduki, hatutajenga uchumi wanchi hii kwa kutumia ubabe na vitisho, ni lazima Serikali itambue kwamba private sector ndio injini ya economy na Serikali ni bodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili gari liende linahitaji engine linahitaji matairi linahitaji bodi, bodi ni Serikali, matairi ni Serikali, engine ni private sector. Hakuna Taifa lolote limeendelea duniani kwa kuipuuza private sector, hakuna Taifa lolote limeendelea duniani kwa ku-disturb private sector, hakuna Taifa lolote limeendelea duniani kwa kufikiria private sector ni wezi tu. Kufanya biashara katika nchi hii chini ya Awamu ya Tano ni kiama, wafanyabiashara wote wa ndani na wa nje wanalia, Mheshimiwa Mpango tumemwambia kwenye Kamati ya Bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamwona Rais anahimiza viwanda unashangaa hivi Watanzania mnajua tumeanza sera ya industrialization lini? Soma historia ya industrialization process in Tanzania na challenge zake. Hakuna kipindi ambacho tunakabiliwa na tatizo kubwa kama kipindi hiki kwenye masuala ya uwekezaji kwenye upande wa viwanda, kwa sababu tunaandika paper nyingi, tuna-policy document nyingi, tatizo letu kubwa ni utekelezaji. Tunapanga mipango mingi ambayo hatuitekelezi sio awamu hii peke yake kuanzia awamu nyingi zilizopita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasoma maandiko ya wasomi wetu fulani wanasema; policy is crafted in Tanzania, modified in Uganda, implemented in Kenya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani Watanzania ni wazuri sana wa ku-craft policies, ndio nilikuwa nasema ukiangali policy mbalimbali ambazo zinazungumzia suala la viwanda nchini linasema nini, kwa miaka 10, 15 iliyopita tumekuwa na Industrial Development Policy, tumekuwa na Vision 2025 najaribu ku-define na kutoa ile frame work tumekuwa na kitu kinachoitwa Tanzania Integrated Industrial Development Strategy ya 2025. Tumekuwa na Mini-Tiger Plan ya 2020, tumekuwa na plan hizi za miaka mitano, mitano zipo tatu ambazo Mheshimiwa Mpango utakuwa unazijua, tuna National Trade Policy, tuna Small Medium Enterprises Development Policy ya 2003. Sasa ukiangalia policy zote hizo zinazungumza kitu kimoja na hakuna hata moja unaweza kusema imekamilika kwa asilimia 10 ama 15. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza habari ya kilimo kwanza tumezungumza haya mambo ya agrarian revolution tunazungumza mageuzi ya viwanda ya kilimo imezungumzwa sana chini ya Kilimo Kwanza, Kilimo Kwanza jamani leo kimeishia wapi? Tumetumia fedha chungu mzima, watu wamefanya plan chungu mzima where is consistency katika planning ya nchi haipo. Leo Rais anahimiza viwanda ili Tanzania by 2025 iwe nchi yenye uchumi wa kati. Nchi yenye uchumi wa kati ambayo inaweza ikaitwa ni industrialized country lazima viwanda vya kuzalisha yaani manufacturing na processing viweze kuchangia angalau asilimia 40 ya GDP. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, industrial hiyo Tanzania inachangangia less than 5% of the GDP, lakini tunajiuliza vilevile hivi viwanda vinavyohimizwa vijengwe soko liko wapi? Huwezi ukajenga uchumi wa viwanda kwa kutegemea soko lako la ndani ni lazima the biggest part of your production iende katika masoko ya jirani na ndio sababu wenzetu wa Asia walivyokuwa na ile Asia Mini Tiger Plan ya Asia ya Southern Eastern ya Asia na Vietnam walifungua kwanza mipaka yao, wakatengeneza National integration policies ili kwamba product inayotoka Tanzania inaweza ikauzwa Kenya, ya Kenya ikaenda Uganda lakini ukiangalia mahusiano yetu namna tunavyojenga mahusiano Afrika Mashariki actually leo tunafunga mipaka hatufungui mipaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachoma vifaranga, tunauza ng’ombe za watu, tunaharibu mahusiano yetu, katika misingi kama hiyo tunategemea tutawezaje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna suala la utawala bora hili jambo tunalizungumza wenzetu mnaliona kama ni utani hili jambo sio utani, hali ya nchi yetu leo kiusalama, ukizungumza leo unashatakiwa, ukichambua uchumi leo unashitakiwa, sisi wapinzani tufanye nini huo ndio wajibu wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatoa takwimu za uongo, Benki Kuu inatoa takwimu zinazotofautiana na Wizara ya Fedha na watu wa takwimu kila mmoja anatoa takwimu zake pengine ili kuilinda Serikali. Ndugu zangu ninachowambia ni kwamba kama tusipojipa ujasiri wa kuikosoa Serikali pale ambapo inabidi, tukaacha kuunda sheria ndogo ndogo za kudhibitiana humu ndani, za kudhibitiana nje ya Bunge tukawazuia Watanzania wasiongee, msiba utatuumbua, msiba utaumbua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali yetu ya uchumi ni ngumu na uchumi sio fly over wala uchumi sio ndege sita, uchumi ni kipato cha wananchi wa kawaida waweze kuboresha maisha yao kutoka pale walipo kwenda maisha bora zaidi. Watanzania wanazidi kuwa maskini na kundi dogo la watu ndilo ambalo linaweza kuona faida ya kukua kwa uchumi wa Taifa hili. Kukua tunakoambiwa kwa uchumi haku-reflect kwenye maisha ya wananchi, wananchi wanazidi kuwa maskini kila siku hili jambo tukilisema wenzetu mnaona labda sisi ni wachokozi, lakini ukweli ni kwamba yako mambo mengi yanaendelea nchi hii leo kama hamkumwambia Rais hamumsaidii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia na rafiki yangu Ndassa, ndugu yangu rafiki akizungumza suala la ukanda nakubaliana naye 100%; lugha ya kuanza kusema kanda hii kanda ile sio nzuri. Vilevile hebu tujipe ujasiri wa kufikiria chanzo cha maneno hayo ni nini? Kwa nini maneno hayo hayakuzungumzwa miaka minne iliyopita, hayakuzungumzwa miaka mitatu iliyopita, kuna mambo ambayo lazima tufike mahali tuelezane ili tuishi kama Taifa la Watanzania kila mmoja akionekana ana haki katika Taifa hili, tuache kuwa na double standard. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ni chama cha siasa tuna wanachama nchi nzima, tungependa tuwe kama Watanzania, tusingependa tuanze kunyoosheana vidole huyu ni kabila fulani, huyu ni dini fulani, huyu ni rangi fulani sio lugha inayopendeza. Lakini yako mambo yanayofanyika katika nchi yetu leo ambayo yanabagua baadhi ya watu wanaonekana wao wanakuwa disenfranchised, haya yasipozungumzwa misiba itakuja kutuumbua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mengine mumwambie bwana mkubwa kwamba unapofanya mambo mengine tenda haki pande zote, tutampongeza tutamsifu, lakini unapokuwa kwamba wewe haki hiyo labda unaipeleka mahali fulani na ukanda mmoja unawanyima. Niseme mfano mmoja ambao ni dhahili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchaguzi unazalisha viongozi kutoka maeneo mbalimbali na watu wote wana haki ya kuchagua na kihistoria katika nchi yetu viongozi waliotangulia Marais wetu waliotangulia walihakikisha kwamba hata nafasi za uteuzi katika Serikali, katika mashirika, katika taasisi za umma zinagawiwa kwa Watanzania kwa wote kwa kadri iwezekanavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo sio hali inayofanyika leo katika nchi hii na mkitaka nilete takwimu nitaleta takwimu za appointment zote za bwana mkubwa tangu ameingia madarakani kwamba kuna baadhi ya watu na baadhi ya mikoa ambayo makusudi kabisa imekuwa disenfranchised. Huu ni ukweli ambao ni lazima tuuseme mambo haya hayapendezi kwa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukija kwenye mambo ya msingi sana Awamu ya Nne ya Serikali iliyopita tulizungumza uchumi wa gesi, ukiangalia kwenye Mpango wote huu uchumi wa gesi ni kama vile umesahaulika hivi ni chama kilekile ama ni chama kingine? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimekwenda ukanda wa kusini kutembelea hiyo miundominu ya gesi ni mambo ya aibu, ni mambo ya kulia, tumejenga bomba la gesi kutoka Kusini kuja Dar es Salaam…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)