Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza napongeza kwa Mpango mzuri ambao umeletwa na Mheshimiwa Dkt. Mpango kwa ajili ya kutengeneza dira ya uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza nalotaka kuzungumza ni kuhusu mazao ya kilimo ambayo ni ya biashara, haya mazao ya tumbuku, chai na kahawa, ni mazao ambayo kwa muda mrefu yameshapoteza masoko hayana bei na wakulima wetu wanateseka. Nilitaka kuishauri Serikali kwamba sasa iangalie namna gani haya mazao ya kibiashara yanaweza yakapata masoko ili Serikali iweze kupata kodi, lakini na wakulima wetu waweze kupata faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine nilitaka kushawishi, hili zao la mahindi nilitaka sasa na lenyewe liingie kwenye Mpango kwamba ni zao la biashara. Mkulima anapolima aweze kupata mazao yake, auze anapotaka aendelee na maisha yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais ameshasema Serikali haina chakula cha kumgawia mtu, wakulima wameshaweka reserve chakula chao, chakula kilichopo hii bumper harvest iliyopo watu waruhusiwe waweze kupeleka mazao yao wanapotaka. Mtu asije na hoja kwamba tuna mikoa ambayo ina upungufu wa chakula, mwaka huu katikati mwezi wa saba na wa nane watu walikuwa wanachukua mahindi Kilindi na Kiteto kupeleka Shinyanga, leo hayo mahindi hayaendi kama kuna deficit Shinyanga kwa nini biashara hii haifanyiki leo? Ruhusuni watu wapeleke mahindi wanapotaka ili waweze kupata faida na waondoke kwenye umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaelekea kweye kupanda watu wanahitaji mbolea na pembejeo, wapeni nafasi wakauze mazao yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Zambia wamezalisha mahindi mengi sana na kwa Wilaya za kina Mheshimiwa Kandege mazao yana trespass kwa njia za kawaida za panya yanaingia hapa. Mazao mengine yanapakiwa pale border yanapita yanakwenda upande wa Kenya. Ukiyaangalia yale mahindi ni meupe ni masafi wanapeleka Kenya hatupati kodi. Hivi leo sisi Watanzania wangepakia wakapeleka Kenya nchi yetu ingekusanya kodi. Mheshimwa Mpango unahitaji kukusanya kodi kutoka kwenye haya mahindi yanayokwenda Kenya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, gunia la kilo mia Kenya ni 7,500 mpaka 8,000, it means unazungumzia karibia shilingi shilingi 140,000. Mheshimiwa Dkt. Mpango ukikusanya pesa ya kodi pale mpakani Holili na Himo, wewe unahitaji pesa, mkulima amepata faida na barabara zetu hazijachimbwa na magari ya wengine badala ya magari yetu na mkulima wetu ameshapata faida. Turuhusu mazao yaende mkulima ata-debate mwenyewe wapi atapata chakula Rais ameshawaaga kwamba hakuna chakula cha msaada. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la lingine tumekuwa na Kakono Project ambayo mwaka jana tuliiwekea mpango hapa fedha zake zipo, mkopo upo wa African Development Bank, Malagarasi ipo, pelekeni pesa hii miradi ianze ili iweze kuongeza umeme kwenye Gridi ya Taifa tuweze kupata faida. Nilihudhuria kikao kimoja pale Kakono, Mtukula nikakaa pale Misenyi, nikazungumza nikaona wale watu wa African Development Bank baadhi yao ni wa Kenya wanaendelea na project. Nilipokaa nikawaza kama this guy’s wapo kwenye hii project wana uwezo wa kuikwamisha mpaka TANESCO yetu hii miradi isiweze ku-take over ili kupata umeme.

Mheshimiwa Mpango naomba hili uende nalo uliangalie ili tuweze kuona ni wapi imekwamia hii Kakono Project na Malagarasi ili tuweze kuzalisha huu umeme wa maji. Leo ukienda Mtera inazalisha megawati 80 lakini Mtera maji hamna, yamekauka, yatashuka kesho kutwa huwezi kuzalisha hizo megawati lakini ule umeme wa Kakono ni maji ya Nile hayatakatika, hayatashuka megawati zetu 87 zitaingia kwenye Gridi ya Taifa na bado tutaendelea kupata faida, naomba hili liangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine uvuvi bahari kuu. Kuna Mheshimiwa mmoja amezungumza hapa, uvuvi wa bahari kuu sasa hivi Tanzania wanachofuata ni suala la leseni shilingi milioni 30, sijui shilingi milioni 40, ukivua saa mbili ndani ya bahari kuu una meli yako unatengeneza shilingi trilioni moja. Hicho ni chanzo Mheshimiwa Mpango nenda nacho, uje na mpango wa kutuambia tunanunua meli, tunavua bahari kuu, samaki za kwetu tu-export samaki tupate faida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Benki ya Kilimo, asilimia 70%, 80% ya Watanzania wanaenda kwenye kilimo, uje na mpango wa kuniambia benki hii inapataje pesa, wewe ndiyo unazo. Hii Benki ya Kilimo leo ndiyo inayokwenda kuokoa watu, benki nyingine sasa hivi zimesha-stuck, haziwezi ku-invest kwenye kilimo kwa sababu ya hali ilivyo na mikopo mingi chechefu sasa hivi ni ile ambayo wali-inject kwenye kilimo hawawezi kwenda zaidi kwa maana hiyo sasa kilimo kitaenda kushuka. Nikuombe Mheshimiwa Mpango, Benki ya China (China Agricultural Bank) ina uwezo wa kutukopesha, itafutie hii benki mtaji iweze kukopesha wakulima wetu ambao ndiyo pesa hiyo itakayozunguka mwisho wa siku utakutana nao kwenye TIN, vioski na mama ntilie, upate watu wa kutoza kodi ambao wameshapata huku kwenye kilimo. Mheshimiwa Mpango hii benki naomba ukija utuambie unaenda kutengeneza shilingi ngapi huko ndani unaichomekea hapo ili iweze kusogea mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko suala la afya. Miaka ya 85 kurudi nyuma tulikuwa na vyuo vyetu vya RMAs (Rural Medical Aids), tulikuwa tuna-produce wale watu ambao walikuwa wanakwenda kufanya kazi kwenye zahanati zetu kule vijijini leo zahanati tunazozijenga kwenye mpango wa Wizara ya Afya kwa maana ya afya hazina wataalamu. Tufanye mpango tuwarudishe hawa Rural Medical Aids wakafanye kazi kwenye zile zahanati zetu kwa sababu kuna nurse mmoja atagawa dawa, atazalisha wanawake au atafunga vidonda. Watu hawa wakipatikana kwenye zahanati zinazojengwa nchi nzima afya za watu wetu zinaweza kubaki salama. Nikuombe muangalie ni namna gani mtapanga kurudisha wataalam hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango nikushukuru kwanza jambo moja ambalo umeonyesha kwenye Mpango hapa, suala la kujenga barabara ya kutoka Handeni - Kibirashi - Kiteto – Chemba - Kondoa – Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe hii barabara sasa kwa sababu imeingia kwenye Mpango ipate pesa iweze kutengenezwa. Wakati hii barabara inatengenezwa tunaomba mtutafutie wafadhili kwenye ukanda huo huo wa kutengeneza viwanda vya kuchambua mchele, kutengeneza unga, kusindika mafuta ya alizeti, kuzalisha juisi ya matunda huko Tanga ili along that road na bomba la mafuta wakati linapita, magari yanapita kupeleka mizigo bandari ya Tanga ili ile mizigo inapopita kuelekea Kanda ya Ziwa, Rwanda, Burundi, Uganda na Kongo basi kuwepo na hivyo viwanda viweze kuzalisha na hayo mazao ya mbegu yaende kwenye hizo nchi ili na sisi wakulima wetu na wananchi kwenye hizo kanda waweze kuwa wamepata faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nikushukuru lakini nikuombe msiwafunge Watanzania waweze kutembea East Africa. Mmeona speech ya Museveni kule kwenye bomba la mafuta Tanga ametukana watu weupe hataki kusikia hii biashara, anasema East Africa tuna population ya one seventy thousand people ambapo tunaweza kuwa ni soko la mazao na kitu chochote tunachozalisha hapa nchini. Watanzania msiwafunge acheni watoke mkiwabana sana they will burst.