Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa sababu muda ni mchache mengi nitawakilisha kwa maandishi lakini kwa uchache huu niende kuzungumzia baadhi ya mambo kwenye Mpango huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukirejea ukurasa wa 40 kipengele cha kwanza kabisa kimeainisha misingi na matarajio ya ukuaji wa uchumi. Kwenye kipengele cha kwanza kinasema kuendelea kuwepo kwa amani, usalama, utulivu na utengamano wa jamii ndani na pia nchi za jirani. Nafikiri hapa ingetakiwa ibadilishwe iandikwe kuimarishwa kwa amani, usalama, utulivu na mambo mengine kwa sababu sasa hivi ilivyo huwezi kusema kwamba Tanzania tuna usalama ilhali tukishuhudia wananchi wanatekwa, wanauawa, wengine viongozi wakubwa kabisa wanapigwa risasi nyumbani sehemu ambayo ni secured. Hatuwezi kusema kwamba tuna amani ilhali maisha ya Watanzania ni magumu sana. Wale wote ambao mfano wametolewa kwa vyeti fake na wale wengine wameambiwa ni darasa la saba hawajapewa pension, gratuity ya kuondoka leo useme kwamba kuna amani Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tumeshuhudia na Mheshimiwa Msigwa ameomba Mwongozo hapa nchi jirani Kenya kwa yale ambayo yamejiri kwenye kuchomwa kwa vifaranga, ng’ombe kukamatwa na mambo mengine. Kwa hiyo, kipengele namba moja ukibadilishe kiseme, kutakuwepo na matarajio ya ukuaji wa uchumi iwapo kutaimarishwa amani, utulivu, usalama na mambo mengine lakini sio kwamba kuendelea kuwepo ilhali hivyo vitu hatuna. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine siku zote nasema hatuna uhalisia kwenye mipango yetu na bajeti ambazo tunazileta hapa. Tusipokuwa na uhalisia ni dhahiri hatutafika pale ambapo tunataka kufika kama nchi. Leo ukiangalia kwenye kitabu chako mwenyewe umeainisha bajeti ya maendeleo ya mwaka 2016/2017 ambayo ilikuwa ni shilingi trilioni 11.8 ilitekelezwa kwa asilimia 55 tu. Hii ya sasa hivi kwa quarter moja ya mwaka 2017/2018 imetekelezwa kwa asilimia 11, on average mpaka tunamaliza itakuwa asilimia 44 mpaka 50 au ikienda au ikienda zaidi tuseme 60. Sasa ikienda na trend hii ina maana tunapanga vitu bila kuangalia uhalisia, time frame, vipaumbele ni vipi, mwisho wa siku tunakuwa tunapoteza rasilimali za wananchi kukaa hapa tunajadili. Siku zote nashauri kwamba ni bora tuweke vitu ambavyo tunajua tutavifikia ndani ya muda kwa resources tulizonazo walau tunapokuwa tumekuja ku-discuss Mpango mnatuambia kwa mwaka uliopita tumeweza kufanya mambo ya maendeleo kwa asilimia 80 au hata 85, 90 sio kwa asilimia 44 au 50. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine na hiki naomba kabisa tuwe sober kwa nachoenda kukiongelea sasa hivi. Kwenye allocation ya kodi za wananchi, maana imechukua discussion nyingi hapa na watu wamekuwa na hisia tofauti.

Mimi natokea Kanda ya Ziwa lakini hili nalipinga na nalipinga with facts na sisi kama wawakilishi wa wananchi ambao tumetumwa hapa Bungeni tukalitafakari ili tuweze kuishauri Serikali vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunaambiwa ujenzi wa jengo la TRA Chato, ghorofa kubwa sana limejengwa kule. Leo tujiulize Chato kuna mzunguko gani mkubwa wa fedha, kuna biashara gani kubwa kule Chato mpaka twende tuwekeze ghorofa? Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inakusanya mapato gani kule Chato tukawekeze lile ghorofa la mamilioni ya kodi za Watanzania? Tutafakari kama Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni Uwanja wa Ndege wa Chato, kabisa. Mimi sipingi uwanja wa ndege kujengwa Chato lakini Uwanja wa Ndege wa Chato ulitakiwa kuwa ni chini ya kilometa moja ya run way.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo pamoja na kwamba kuna kukiukwa kwa Sheria ya Fedha za Umma ambayo tulipitisha hapa shilingi bilioni mbili, lakini naambiwa zimetumika zaidi ya shilingi bilioni 39, hiyo ni hoja lakini sio hoja kubwa sana kwangu, tujiulize sisi Watanzania na hawa ambao wanamshauri Rais…

T A A R I F A . . .

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, inabidi nicheke kidogo. Wakati tunapitisha na kwenye kitabu chake cha Mpango wakati ule tunapitisha kwa ajili ya upembuzi yakinifu zile shilingi bilioni mbili walisema ule uwanja wa Chato unajengwa kwa ajili ya usafiri ndani ya Geita na mikoa jirani hawakusema otherwise.

TAARIFA . . .

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu hajatoa taarifa ameuliza swali, nitamjibu kesho wakati wa kipindi cha maswali na majibu kama Waziri Kivuli wa eneo husika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, point hapa ipo nimejibu kwamba wakati inakuwa allocated hapa ilikuwa ni uwanja kwa ajili ya usafiri ndani ya Geita na mikoa jirani. Hawakusema kwamba kwa ulinzi, usalama na mambo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwa Mheshimiwa Jenista, ilikuwa ni shilingi bilioni mbili, ukiongeza shilingi bilioni 39 inakuwa ni shilingi bilioni 41, sijui ni sheria ipi hiyo? Pia reallocation yake tunataka tujue imekuwa reallocated kutoka kwenye kifungu kipi kuja kwenye hizo shilingi bilioni 39? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine nimesema kwangu issue siyo sheria zaidi, lakini unaenda kuwekeza huo uwanja mkubwa pale Chato wa runway zaidi ya kilometa tatu ni ndege gani inaenda kutua pale kubwa hivyo? Hiyo ni misuse ya hela za walipa kodi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikajiuliza mara mbili, leo tunasema kwamba Serikali inahamia Dodoma, of which I support 100%; Makamu wa Rais anahamia Disemba, Mheshimiwa Rais tunaambiwa anahamia mwakani. Bunge la Kumi tulipitisha uwanja wa Msalato ujengwe mpaka leo haujajengwa, Rais akija hapa tunatarajia wakija wale Marais, like Trump akija hapa ana ndege ambayo ni Boeing 737 itatua hapa Dodoma au itaenda kutua Chato? Why don’t we rethink tukaja tukajenga kwenye uwanja wa Msalato maana itakuwa ni double cost kwa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wanakuja Marais ambao wanatumia ndege kubwa, Rais Magufuli anaondoka Dodoma kwenda kuwapokea Dar es Salaam maana haka ka-uwanja ka-Dodoma hakawezi kuwapokea. Kwa nini hizo hela tusingeweza kujenga hapa Msalato, kule Chato
tumjengee uwanja wa kuweza kutua ndege ya kawaida like Precision, Bombadier na ndege ya Serikali kuliko kujenga uwanja mkubwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ndiyo hoja yangu kubwa au basi kama tunataka tuijenge Chato tungeweza kujenga hospitali kubwa kabisa ku-save maisha ya Watanzania kuliko ku-sink shilingi bilioni 39 kwenye uwanja ambao hautatumika au tungeweza kujenga Chuo Kikuu pale kama tunataka tuijenge ile Chato ikue vizuri, unlike tulivyofanya sasa hivi. (Makofi)

TAARIFA . . .

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu yangu Mheshimiwa Innocent pale, mtani wangu, kwanza taarifa yake siipokei lakini pili, ngoja nimsamehe nilikuwa nampa dongo moja ila nimsamehe, niendelee kuchangia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Innocent nilimuona juzi wakati Rais amezuru kule, anapiga magoti kumuomba shilingi bilioni 30 za maji. Wajibu wako kama Mbunge ni kuisimamia Serikali hela za walipa kodi zije zifanye kazi kule, not to kneel down before the President ili uweze kuletewa mradi wa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea, Chato bado, tumeona ujenzi wa traffic lights pale Chato, nikajiuliza hawa watu wanamuogopa Magufuli kwa nini wasimshauri vilivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nini dhima kubwa ya hili, ukiangalia kuna miji mingi na ina high congestion ya magari leo mmeenda kujenga Chato na kuna picha niliona sitaki kuamini kama kweli ni ya kule lakini nilivyopita mimi Chato sikuona kama kuna congestion kubwa ya magari mnaweka traffic lights Chato, wanapita punda. Misuse of funds za walipa kodi wa Tanzania wakati tuna majengo ya shule hajajengwa, hospitali nyingi zinakosekana wamama wajawazito wanafariki hakuna huduma proper, mnaenda kujenga traffic lights za Chato. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ndiyo the only way kwa kauli mbiu ya Tanzania ya viwanda kama ingeenda vizuri, tungewekeza kwenye kilimo tungeweza kufikia hii ndoto ya Tanzania ya viwanda. Ukiangalia bajeti ya ruzuku ya mbolea na mbegu ya mwaka 2015/2016 tuliweza ku- allocate kwa kaya zaidi ya 900,000 lakini ukija 2016/2017 tume- allocate ruzuku ya mbolea na mbegu kwa kaya 370,000 tu. Leo tunasema tunaleta ukombozi kwa hawa Watanzania halafu wakilima wanataka kuuza mazao yao, mnawazuia badala ya kuwatafuta masoko. Mwaka 2015 kahawa Tarime ilikuwa inauzwa shilingi 2,000 kwa kilo leo ni shilingi 600 halafu tunasema nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango na watu wako wanaokushauri naomba ukae uangalie vizuri ni jinsi gani tunaweza ku-move na haya ambayo tunakupa hapa kama Wabunge myafanyie kazi ili Tanzania tunayoitaka iweze kufikiwa. Nina imani kabisa kwa vivutio ambavyo Tanzania tumepewa, tungewekeza kwenye utalii kwa nchi hii tusingekuwa wategemezi tungeweza kujitosheleza kabisa. Tuna vivutio vingi vya kitalii ambavyo vingi havipatikani hata kwenye mataifa mengine lakini tume-underutilize, kwa nini? Ni kwa sababu priority zetu zinaenda kwa kinyume, we are thinking backward. Leo TTB ingepewa fedha za kutosha ingeweza kutangaza utalii wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungeweza kuiwezesha TTB kupitia Tourist Development Levy tukapeleka fedha nyingi ili sasa waweze kuvitangaza vivutio vyetu na kufanya wajibu wao kama inavyotakiwa. Leo unakuta TTB wakiomba fedha ili waweze kujiendesha wanapata chini ya asilimia 30, tunashindwa kuvitangaza vivutio vyetu. Ukiangalia tuna beaches nyingi sana, kuna nchi zingine zinajiendesha kwa vivutio vya utalii walivyonavyo ambavyo ni vichache ukilinganisha na Tanzania. Sisi Tanzania aliyeturoga nadhani alishafariki, tulishapewa laana ambayo haifutiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukae tujitafakari sisi kama Wabunge wa Bunge la Kumi na Moja tukiondoka tutakuwa tumeisaidia vipi nchi yetu. Ni wengi humu wanasafiri nchi mbalimbali ikiwemo Mawaziri, mnaposafiri huko mnajifunza nini ambacho mnakileta Tanzania ili tuweze kukitumia kuhakikisha kwamba nchi yetu ina-move? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Deni la Taifa. Nazungumzia deni la ndani, kuna wakandarasi ambao wanaidai Serikali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)