Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kutoa mchango wangu kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa mwaka wa fedha 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nitaanza na mchango wangu kipengele cha mazingira wezeshi kwa uendeshaji wa biashara na uwekezaji na hasa sehemu ya miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa inayoifanya katika ujenzi wa barabara katika nchi yetu. Pia kipekee nichukue nafasi hii kuishukuru Serikali kwa kuanza barabara ambayo Wabunge wa Mtwara tulikuwa tunaipigia kelele, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala hadi Masasi; barabara yenye urefu wa kilometa 210. Sasa hivi mkandarasi yuko site anaanza ujenzi wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami kutoka Mtwara hadi Nnivata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni matarajio yetu Wanamtwara kwamba mpango ujao sasa utaonesha maendelezo ya ujenzi wa barabara hii. Tunatarajia sasa tuone kipande kingine cha kilometa 50 kutoka Nnivata kuendelea hadi Newala na hatimaye tukamilishe kilometa 210.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa korosho. Tunapozungumzia korosho Tanzania tunazungumzia Wilaya ya Nanyamba, Tandahimba, Newala na Masasi. Takribani asilimia 60 za korosho ya nchi hii inazalishwa katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa wazo la kuanzisha Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA). Wazo hili ni jema, na wazo hili litaharakisha ujenzi wa barabara ambazo zinamgusa mkulima, zile feeder roads. Hapa ninaomba niishauri Serikali yangu, kwanza niwapongeze TARURA kwamba wameanza vizuri sana. Kuna Mtendaji Mkuu yupo na Wakurugenzi wake wanaanza kuchakarika kwa kasi kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtandao wa barabara za TARURA ni takriban kilometa 108,000. Mtandao huo ni mkubwa na tukiendelea na formula ile ya zamani wa kwenye Road Fund yaani TANROADS wanachukua share kubwa kuliko hii TARURA, sabini kwa thelathini, TARURA watashindwa mara moja.

Kwa hiyo ninaomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha utakapokuja na mpango wa maendeleo wa mwaka 2018/ 2019 utueleze TARURA sasa itapata asilimia ngapi ya fedha za Road Fund na TANROADS watapa asilimia ngapi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ningependekeza, kwa sababu mtandao wa barabara wa TARURA ni mkubwa, kama nilivyosema ni takriban kilometa 108,000 tufanye nusu kwa nusu; yaani 50 iende TANROADS na 50 iende TARURA ili ikajenge barabara ambazo mkulima wan chi hii anatumia kila siku akiwa na baiskeli, bodaboda akibeba mazao yake na kupeleka shambani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa pili unahusu matumizi ya gesi. Wasemaji wengi sana wamechangia kuhusu gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado nchi yetu imejaaliwa kuwa na reserve kubwa ya gesi, lakini kama walivyosema wachangiaji wengi hatujatumia hii fursa vizuri. Matumizi yake bado ni ya kusuasua. Mwekezaji aliyopo Mnazi bay (MNP) ana uwezo wa kuzalisha au kutupa cubic feet milioni 136 kwa siku ili zitumike pale Madimba na Mtwara lakini kwa siku tunatumia cubic feet milioni 40 tu, kwa hiyo utaona ni kiasi gani yule mwekezajia anazalisha lakini hakitumiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba sana Serikali yangu kuongeza kasi ya matumizi ya gesi; mtumiaji mmojawapo ni kiwanda cha Dangote. Hadi leo pamoja na maamuzi ambayo alitoa Mheshimwia Rais akiwa pale Mtwara, kwenye ziara kwamba Dangote apewe gesi hadi leo kiwanda cha Dangote hakujapewa gesi. Kuna urasimu usio wa lazima, hebu tupunguze urasimu tumpe Dangote hiyo gesi na kiwanda cha Dangote kikipata gesi hata bei ya saruji anasema itashuka mpaka shilingi 8,000 kwa mfuko, na hii itawasaidia Watanzania wetu. Kwa hiyo, naomba Serikali yangu iongeze kasi ya kutataua changamoto ambazo zinakwanza Dangote kupewa gesi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ukisoma Mpango wa Maendeleo wa mwaka jana ulisema kuna mradi wa kujenga miundombinu ya kusambaza gesi majumbani kwa mikoa ya Mtwara na Lindi, mradi huu hadi leo haujaanza. Naiomba Serikali yangu itoe pesa kwa TPDC ili mradi huu uanze. Mradi huu ukianza basi matumizi ya gesi yataongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti. kuna mradi mkubwa wa kuchakata gesi na kuwa kimiminika ule wa Lindi, Mradi wa LNG. Mradi huu kila siku tunaambiwa kwamba tupo kwenye maandalizi ya eneo la mradi. Maelezo haya sasa tumeyachoka ni ya muda mrefu tunaomba sasa tuwe na lugha nyingine. Ni mradi mkubwa na naomba Serikali iongeze kasi ya kukubaliana na hawa wafadhili ili mradi huu uanze. Mradi huu ukianza utatoa fursa nyingi za ajira kwa vijana wetu wa Mtwara na Lindi na vile vile tutaongeza matumizi ya gesi ambapo sasa bado gezi ipo ya kutosha lakini matumizi yake bado ni ya kususua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu maji; hakuna Tanzania ya viwanda bila maji ya kutosha. Tangu mwaka juzi tukiwa Bungeni hapa tumeambiwa kuhusu miradi 17 ya maji ambayo itapata ufadhili kutoka Benki ya India. Miradi hii itanufaisha miradi ya Makonde, Muheza, Njombe na Zanzibar. Hadi leo hii tunaambiwa bado kusainiwa financial agreement… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)