Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi na mimi nitoe mchango wangu katika hotuba yetu ya mpango. Mimi nina maeneo matatu/manne na la kwanza ni kilimo. Tunapoingia kwenye uchumi wa viwanda hatuna namna ya kukwepa kuendeleza kilimo na wachangiaji wengi wameeleza. Manufaa ya kilimo yanaonekana na yako wazi, kwanza ina mchango mkubwa sana kwenye uchumi wa Taifa, lakini pia imewaajiri Watanzania wengi. Kilimo kinaweza pia kikatusaidia kwenye soko la ndani la bidhaa zinazotokana na viwanda. Kwa hiyo, kwa vyovyote vile hatuwezi kukwepa. Sasa ninavyoona mimi kwenye Mpango huu na Mipango yote iliyopita hatujatia mkazo wa kutosha kwenye kuimarisha kilimo chetu, ninaomba hili jambo lizingatiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano sisi Mkoa wa Rukwa katika msimu uliopita tumezalisha zaidi ya tani 710,602; mahitaji yetu sisi ni tani 257,553. Kiasi cha mahindi ambayo sisi tumetoa nje ya mkoa na kwa sababu tuna utaratibu wetu kwenye njia zinazotka nje ya mkoa; tumetoa tani 50,189. Ziada tuliyonayo leo ni zaidi ya tani 402,859.

Kwa hiyo nina wasiwasi hata takwimu za Mheshimiwa Waziri; tulikuwa tunaongea nae leo kwamba anasema Taifa lina ziada ya tani 700,000 za chakula kwa sasa ikiwa sisi Mkoa wa Rukwa tu tuna tani 402,859.62.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wananchi wetu mahindi ndiyo kila kitu. Ndiyo kwenda shule, mahindi ndiyo afya zao na ndio uchumi wao. Kwa hiyo, usipoweka mfumo mzuri wa masoko katika mahindi sisi umetuumiza. Nilikuwa nafikiri kama Taifa tuangalie, kwa sababu uzalishaji wa mahindi utaendelea kuwepo, haiwezekani kila mwaka tunakuja hapa kuzungumza kwa kutoa mishipa mingi, kukaza maneno ya hovyo, Wabunge kuweka vikundi vikundi. Lazima kama Taifa mjue kwamba kuna wakulima wa mahindi na mahindi yataendelea kulimwa. Sasa ni lazima tuwe na mfumo unaoeleweka, mkaanzisha hata kitaasisi au NFRA ikaimarishwa, ikapewa hata mtaji ili iwe inanunua katika maeneo ambayo kilimo kinafanya vizuri halafu baadaye inaweza ikafanya biashara ama nje ya nchi au sehemu ambazo kuna upungufu wa chakula katika mataifa mengine kuliko kuwa na jambo lisilo na majibu ya uhakika kila mwaka. Hii nafikisi si nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuimarisha kilimo nina kata yangu ya Nkandasi. Kuna shamba la Milundikwa State Farm limenyang’anywa na Jeshi na wananchi sasa zaidi ya 2000 hawana shughuli ya kufanya. Sasa watachangiaje katika Mpango huu? Ninaiomba Serikali itume wataalam wake wakaone jinsi wananchi hawa ambao wamekaa miaka 18 katika eneo hili lakini leo wanakuja kufukuzwa na Jeshi bila sababu za kutosheleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, waagizeni viongozi wakafanye utafiti waone haki iko wapi kwa sababu eneo hili walipewa kihalali na maandishi yapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la maji. Nimeona Mipango mizuri sana katika ukurasa wa 53 katika kitabu chetu cha Mpango na nimeona pia Wizara inavyojitahidi katika kushughulikia suala hili kwa kipindi hiki, hasa baada ya Bunge kuamua kushughulikia suala hili kikamilifu.

Mheshimiwa Mwneyekiti, dosari niliyoiona ni utoaji wa pesa. Zile pesa ambazo zinapatikana moja kwa moja kutoka Wizarani, zinazokwenda kwenye Wizara kwa maamuzi ya Bunge zinakwenda vizuri kwenye kusukuma miradi. Lakini zile ambazo zinapatikana kutoka Wizara ya Fedha zinachelewa na hazitusaidii sana kusukuma miradi, hii iangaliwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niweke vizuri, Wilaya ya Nkasi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)