Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na mimi naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kupata nafasi ya kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza kwa kuzungumzia uwanja wa ndege wa Chato. Mimi ni Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini na ninashangaa sana watu wanaoona uwanja wa ndege unaojengwa Geita/ unaojengwa Chato kwamba ni matumizi mabaya ya fedha. Watu wana-define uwanja mkubwa kwa urefu wa runway, lakini nadhani wanapungukiwa exposure. Uwanja mkubwa ni facilities na uwanja ule ili uwe mkubwa ungekuta linajengwa jengo la abiria kubwa, kwa hivyo ndipo ungesema uwanja mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwakumbushe tu, wamesema uwanja wa ndege uko pale strategically, wanasahau kwamba kutoka Chato kwenda Rubondo ni kilometa 30 na tunahamasisha utalii. Pia wanasahau kutoka Chato kwenda Biharamulo ambapo kuna mbuga za wanyama za Buligi pamoja na Biharamulo pale ni kilometa
50. Wanasahau kwamba tuko karibu kilometa 100 kwenda mpakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunaposema ni strategic airport watu wengi hawaelewi tunazungumza nini, wanawaza tu kwamba ni uwanja wa Rais kwenda nyumbani. Mimi nasema ule uwanja umejengwa sehemu sahihi na uwanja ule sisi tunauhitaji ungejengwa katika eneo lolote lile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo jingine ambalo watu ni lazima walifahamu Rais alikuwa akitua Mwanza kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza kwenda Chato anatembea kilometa 270 anakwenda kupumzika. Akitua Bukoba anatembea kilometa 250 kwenda kupumzika. Sasa amejenga uwanja karibu anapokwenda kupumzika wanapiga kelele. Mimi nataka niwashauri, issue ya ukubwa si urefu wa uwanja, nenda kasome, issue ya ukubwa ni facilities za uwanja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, habari ya TRA, jengo la TRA watu wanafikiri kurudi nyuma unakwenda mbele unaenda wapi? Badala ya kusema tunajenga jengo likae miaka 50 mbele wewe unawaza kujenga slope.

Mimi nasema hata ofisi za Serikali tuache sasa, tuanze kujenga majengo ya ghorofa. Habari ya taa ni habari ya Halmashauri yenyewe hata kama wangepita punda tunaangalia usalama wa raia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la madini. Serikali ilipoanza kusimamia vizuri madini sisi watu wa Geita Mjini tumeona manufaa yake na nataka nitoe takwimu hapa. Kabla ya Serikali kuweka mikono yake kwenye madini, mapato ya Halmashauri yangu Januari-Machi ilikuwa shilingi milioni 514; Aprili-Juni shilingi milioni 750; yakaongezeka kidogo hapo. Ilipofika Julai-Septemba tumepata bilioni moja kasoro, maana yake ni nini? Kulikuwa kuna wizi mkubwa sana unafanyika hapa kwenye madini. Wito wangu hapa kwa Mheshimiwa Waziri ninashauri ufanyike uchunguzi kurudi nyuma kuona kwa nini baada ya Serikali kutuma wawakilishi kwenye hizi kampuni za madini mapato ya Halmashauri yangu yameongezeka kutoka shilingi milioni 500 mpaka shilingi bilioni moja wakati kazi ni ile ile? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, tulipitisha Sheria hapa ya Local Content, bado watu wa mgodi wanapiga. Bado wana walinzi kutoka nje, bado wana kampuni nyingi kutoka nje ambazo zinaweza kufanya kazi na Watanzania. Wakati wa Mpango wa mwaka uliopita nilishauri hapa kwamba tuna kampuni nyingi sana ambazo zinafanya kazi kwa remote, kampuni iko South Africa, iko Australia, inafanya services katika Mgodi wa Geita, hawalipi kodi! Bado halijafanyiwa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokwenda kuwaomba hawa watu watulipe service levy wanakwambia hii kampuni haipo Tanzania. Naomba kushauri, sheria hii tuliyoipitisha hapa Bungeni, yaelekezwe haya makampuni ya madini yaweze kuisimamia vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu tunajenga reli kuja Dodoma, mimi nasema fine, tunakopa, tunafanya nini, mimi nasema fine, lakini wasiwasi wangu ni mmoja tu, hii reli itakapofika Dodoma kabla haijafika Mwanza itakuwa haina msaada mkubwa kwenye uchumi wa Tanzania. Nataka kushauri, badala ya kufanya vipande vipande kwa muda mrefu ufanyike uamuzi wa mara moja wa kuwekeza reli hii moja kwa moja kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza ili itakapokamilika manufaa yake yaanze kuonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi mimi na Waheshimiwa Wabunge wenzangu tulipata bahati ya kwenda China na tukaenda katika jimbo moja la Guangdong. Tulipotembelea pale, Meya wa mji ule anatuambia jimbo lile limejengwa na private sector, anasema Serikali haijajenga miundombinu katika jimbo lile. Airport, barabara, madaraja wamejenga private sector. Tuache kukopa kujenga miundombinu, tukaribishe… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)