Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Innocent Lugha Bashungwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karagwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kutoa mchango wangu katika Mpango wa Bajeti ya Maendeleo wa Taifa kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa wasilisho zuri la Mapendekezo ya Mpango huu na nimtie moyo kwa sababu ameleta Mpango huu ili tuweze kumpa ushauri na naamini kabisa mna muda wa kutosha kuweza kufanya
review kwa ku-take into account ushauri ambao tunawapa sisi Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze pia kwa kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa namna ya kipekee walivyoweza kusaidia kutoa commitment ambayo iko serious kwa Mradi wa Maji wa Rwakajunju kwa Wanakaragwe, nawashukuru sana Serikali. Pia nawashukuru kwa commitment ya kuweka lami barabara ya Bugene kwenda Benako ambayo itafungua fursa kubwa sana katika Wilaya yetu na Ngara pamoja na nchi za jirani za Rwanda. Nawashukuru pia kwa commitment ya kuweka lami barabara ya Mgakorongo kwenda Morongwa itatufungulia fursa na ndugu zetu wa Uganda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya shukurani hizo pia nitumie nafasi hii kuzungumzia suala la uwanja wa Chato. Mimi nadhani wenzetu upande ule wamekosa, hoja kwa sababu huwezi ukatumia muda mahsusi wa kuchangia Mpango wa Maendeleo wa Taifa unazungumzia taa kufungwa kwenye uwanja wa Chato. Taa za shilingi milioni tano unasimama Bungeni unasema Serikali imetumia shilingi milioni tano, yaani ni kukosa hoja kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia jiografia ya nchi yetu na nchi za jirani East African Communities na nchi za Great Lakes ni sahihi kabisa kuweka uwanja pale Chato kwa sababu lazima tuangalie future, tusiangalie leo. Chato ina access ya Ziwa Victoria pale, kwa hiyo, ukiweka uwekezaji wa reli ambao utaenda mpaka Rwanda, ukaweka dry port ya Isaka (bandari kavu), ukaweka potential ya kutumia usafirishaji wa maboti ya mizigo kwenda Kenya na Uganda, Chato iko strategically located kwa ajili ya kuhudumia mikoa ya kule upande wa Kagera, Geita hata Kigoma, DRC, Burundi na Rwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye siasa tufanye lakini si kwenye mambo ya maendeleo ambayo yako serious. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi katika mpango wa maendeleo ulioko mbele yetu nipende kushauri Wizara ya Fedha, kwamba mfanye re adjustment approach. Serikali na nchi yetu, vision ya kuwa na uchumi wa viwanda by 2025 uko clear kwa wananchi wetu, kwa wadau wa maendeleo na kwa private sector na dunia nzima. Kwa hiyo jambo hilo ni muhimu sana kwa sababu tuna vision ambayo tunataka tuhakikishe mpango mkakati unatupeleka kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ninachokiona ambacho ni changamoto na muda wa kubadilisha mkakati upo Serikali ime front load sana uwekezaji kwenye sekta ya viwanda na biashara moja kwa moja badala ya kuweka effort kubwa ya ku-facilitate sekta binafsi iwekeze katika viwanda halafu nguvu ya Serikali m-front load bajeti kubwa iende kwenye sekta ambazo zinawahusu Watanzania walio wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mpango wewe ni mchumi, ukiichukua ile Douglas Production Function kwa uchumi wa Tanzania ambao hauko complicated mambo ya financial market, financial derivatives sisi Tanzania we have to do the best with what we have. Tuna ardhi ambayo ni arable tunaweza tukafanya kilimo, tuna labor force ya kutosha, asilimia 67 ya Watanzania wako kwenye sekta ya kilimo.

Kwa hiyo, tunachohitaji pale ni kuwa karibu na hawa wakulima, wafugaji, wavuvi na kuangalia katika maisha yao ya kila siku zile shughuli ambazo wanazojishughulisha nazo, tTukiwasaidia wakapiga hatua mbili, ile asilimia 67 ya Watanzania ambao wana…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: ... itasaidia kukuza uchumi na kupunguza umaskini.