Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Mradi wa Umeme wa Makaa ya Mawe Mchuchuma; Serikali imekuwa na kigugumizi cha kuanza utekelezaji wa mradi wa Mchuchuma. Naomba Serikali sasa ianze mara moja kutekeleza Mradi wa Mchuchuma na Liganga kwa sababu ahadi zimekuwa kwa muda mrefu lakini hakuna utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu madini na gesi, naiomba Serikali ihakikishe inakusanya mapato kwenye madini kama kodi za wawekezaji kwani tuna migodi mingi lakini hatukusanyi mapato mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kodi, vyanzo vyote vya mapato vimechukuliwa na Serikali Kuu. Halmashauri zinashindwa kujiendesha kwa sababu hazirudishwi kwenye Halmashauri. Hii inakatisha tamaa kwani watendaji wetu wanashindwa kabisa kuendesha Halmashauri; Halmashauri zinakufa. Naiomba Serikali irudishe vyanzo hivyo vya mapato kwenye Halmashauri zetu ili utendaji wake uwe bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kilimo, asilimia kubwa ya Watanzania ni wakulima. Tunapanga kwenda kwenye Tanzania ya viwanda, hatuwezi kwenda kwenye Tanzania hiyo kama hatujaboresha kilimo. Bado Watanzania tunalima kwa mikono, pembejeo ni gharama, bei ya vyakula ni chini. Tunawezaje kuingia kwenye ushindani wa masoko? Kwa vyovyote vile hakuna soko tena. Matokeo yake hatuwezi kuondoa umaskini katika nchi hii. Naiomba Serikali ione namna gani itaboresha kilimo na kuwasaidia wakulima. Naiomba Serikali ipunguze bei za pembejeo na pembejeo zifike mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara wananyanyasika sana, wanabanwa kila upande, wanatozwa kodi kubwa ambayo hailingani na mitaji yao, hasa wafanyabiashara wadogo. Wafanyabiashara wengi wamefunga biashara zao kwa sababu ya usumbufu mkubwa wanaoupata hapa nchini. Naiomba Serikali iangalie namna ya kuwatoza kodi wafanyabiashara hawa bila kuwanyanyasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.