Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na Malengo ya Milenia (MDGs) hatukuweza kufikia malengo, tulifanikiwa maeneo matatu tu na hata hivyo UNESCO ilitupatia tuzo katika uandikishaji wa watoto, kwa hilo napongeza japo hatukuweza kuwa na elimu bora kwa watoto wetu japo waliandikishwa kwa wingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu kwa sasa tuna SDGs ambayo malengo yake ni mengi zaidi ya MDSs. Je, katika Mpango huu Serikali imejipangaje kuhakikisha inaingiza katika Mpango huu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nchi yoyote makini, lazima iwe na vipaumbele vichache visivyoweza kushindwa katika utekelezaji, Tanzania kwa sasa ina vipaumbele gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawezaje kuwa na maendeleo na mipango bila kilimo. Viwanda bila kilimo ni uti wa mgongo ni vema tukazingatia kilimo maana viwanda vinategemea malighafi za kilimo.