Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wenye dhamana ya Fedha na Mipango kwa kazi kubwa wanayoifanya ili kuhakikisha Ilani ya CCM 2015/2020 inatekelezeka. Baada ya pongezi hizi, nina maombi yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba uangalie uwezekano wa kuutengea na kuuwekea fedha Mfuko wa Taifa wa Watu Wenye Ulemavu kama ambavyo Mfuko wa Vijana unatengewa. Mheshimiwa Waziri, Mfuko wa Taifa wa Watu Wenye Ulemavu (WWU) ni muhimu sana ukatengewa fedha, hii itasaidia sana ustawi wa WWU na hasa ikizingatiwa kuwa wana mahitaji mengi ikiwemo hitaji la mitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi la pili, fedha iongezwe kwenye Kasma 280400 Mafunzo kwa Watu wenye Ulemavu ambapo mwaka 2017/2018 Kasma hii ilitengewa shilingi 600,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti,Idara ya Watu Wenye Ulemavu haina sub vote, hivyo ninaomba Mheshimiwa Waziri uliangalie hili maana mchakato ulishaanza.