Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mchango wangu kwa kuzungumza nina mawazo katika kuimarisha sekta ya sukari kutokana na potential ya soko la ndani na nje. Mfano sisi tunaagiza sukari yenye thamani dola za Kimarekani milioni 60.9 (shilingi bilioni 123 za Kitanzania), majirani zetu kama Angola ambao ni member wa SADC wanaagiza sukari kwa thamani ya dola za Kimarekani milioni 161.1, Ethiopia dola za Kimarekani milioni 188, haya ni masoko wazi lakini ili tuyafaidi. Pamoja na mradi wa Mkulazi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, tufikirie kuwezesha wawekezaji wa ndani kupitia benki za TIB na ile ya kilimo TAB ambayo mpaka sasa ina around shilingi bilioni 164 lakini imekopesha shilingi bilioni 3.4.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuwekeza kiwanda cha kuzalisha tani 150,000 inahitaji wastani wa dola za Kimarekani milioni 80 bila kujenga facilities nyingine. Pamoja na mashamba utahitaji jumla ya dola za Kimarekani milioni 150, hapo tayari una miundombinu ya nishati na barabara. Sasa kumbe tutumie mfumo wa small scale growers ambapo tunakuwa na factory nyingi maeneo mbalimbali kwa kushirikiana na Halmashauri na sekta binafsi. Maeneo potential ya kuzalisha sukari ni pamoja na Bagamoyo tani 120,000; Mkulazi tani 200,000; Ruipa tani 60,000; Rufiji tani 60,000; Kasulu tani 30,000 na Mkongo – Mara tani 30,000, jumla tani 500,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, faida ya kutumia small scale sugar plants ni kama ifuatavyo:-

(i) Inahitaji eneo dogo kama five acres.

(ii) Inahitaji kama shamba la miwa la ekari 3,000 ili kulisha kiwanda.

(iii) Inapunguza gharama za kusafirisha miwa kwenda kiwandani mfano leo hii pale Kilombero kuna miwa inasafirishwa umbali hadi wa kilometa 60 lakini ikiwa ndani ya shamba la eka 3,000 huwezi kuwa na gharama kubwa ya kusafirisha.

(iv) Inachukua wastani wa miezi kumi kujenga kiwanda cha small scale.

(v) Inahitaji mwaka mmoja kuwaendeleza wakulima wadogo (small scale farms).

(vi) Ina promotes ushiriki wa small holder farmers.

(vii) Ni rahisi kutoa extension service na pia mwekezaji hahitaji kugombania ardhi maana yeye atasaidia small holder kwa mbegu na pia huduma nyingine muhimu kuwezesha kupata miwa yenye content kubwa ya sukari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muundo huu umewasaidia sana Brazil ambao wanazalisha 20% ya sukari (tani milioni 36) na wanahodhi 40% ya soko la dunia. Hivyo, potential ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee Benki ya Kilimo. Nimeona juzi hapa benki ikiwa imepata fedha zaidi. Hata hivyo, kuna matatizo makubwa kwenye hii benki kuanzia Mtendaji Mkuu mpaka Bodi. Mfano, hivi Zanzibar State Trading Corporation (ZSTC) waliomba mkopo wa shilingi bilioni 10 ili wanunue karafuu, Bodi ikapitisha lakini kwa uzembe wa Mtendaji Mkuu mkopo ukacheleweshwa, msimu ukapita baadaye ZSTC wakaukataa mkopo. Tujiulize with a capital of over 164 billion, how come wametoa mkopo wa less than five billion? And this is a bank na main core/function of the bank ni kukopesha. Mliangalie hili jambo ili benki hii iwe nyenzo kuelekea uchumi wa viwnada. Ahsante.