Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ili niweze kuchangia hoja zilizopo mbele yetu. Nitajikita kwenye taarifa ya Kamati ya PAC ambayo ni mjumbe. Kwanza kabisa nitumie fursa hii kuipongeza Kamati ya PAC kwa taarifa nzuri, lakini nimpongeze Mwenyekiti wangu mama Kaboyoka kwa uongozi wake na ujasiri mkubwa aliouonesha wakati wa kipindi chote cha kuongoza na kuandaa taarifa hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nitaomba kujikita kwenye maeneo machache katika taarifa hii PAC. Kwa kuanza nitaomba kuchangia kwenye mradi wa Mlimani City na kabla sijaanza kuchangia naomba ku- declare interest kwamba nilisoma Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, Focus of Commerce ambayo sasa UDBS (University of Dar es Salaam Business School) nilipata degee ya Accounts, Bachelor of Commerce in Accounting.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa Mlimani City una maajabu, una maajabu mengi lakini naomba nizungumzie maajabu saba ya Mradi wa Mlimani City. Ajabu namba moja mtaji ambao uliowekezwa kwenye mradi huu wa Mlimani City. Tangu mradi huu umeanzishwa Mwekezaji ameweza ku-issue shares 100 tu kati ya shares 1,000 ambazo ziko authorized kwenye mtaji wa hiyo kampuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, share hiyo kwa miaka hiyo iliuzwa Dola 0.75, kwa hiyo mtaji mzima wa Mlimani City ulikuwa ni Dola 75 kwa sasa hivi ni 150,000 au 160,000 sikumbuki by then 2004 exchange rate ilikuwa ngapi ambao mnakumbuka mnaweza mka-calculate na mkajua ni kwa kiasi gani mradi mkubwa kama wa Mlimani City uliweza kuwekezwa kwa mtaji kiasi kidogo namna hiyo. Mpaka leo zaidi ya miaka 10 share 900 kwenye kampuni hiyo bado hazijauzwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu namba mbili, ni mbia mwenye share moja anaitwa Transtor, huu mradi una Wabia wawili Highland View na Transtor ameweza kukopesha Kampuni ya Mlimani City dola za Kimarekani 40,000 wakati yeye ana share moja badala ya kuwekeza kwenye ile Kampuni kwa kununua zile share ambazo mpaka leo hazijauzwa tangu kampuni hiyo imeanzishwa ambayo ina share 900 mpaka sasa hivi haziko issued. Hiyo ni ajabu namba mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini unajiuliza ni sababu gani labda ameamua kukopesha badala ya kununua shares. Wahasibu wenzangu sababu ni mbili tu. Sababu ya kwanza ni yeye kuendelea kupata riba au interest income kutokana na pesa anayoikopesha Mlimani City. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya pili kwa sababu interest expense inapunguza faida kabla ya kupata net income, kwa hiyo automatically faida ya Mlimani City inapungua na mwishoni kabisa na pesa inayolipwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam inapungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninazo hesabu za Mlimani City Holdings hapa zinaonesha kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017 mwaka mmoja tu financial charges kwa maana interest expenses zilikuwa 1.9 Milioni US Dollars, kwa maana hiyo kwa mwaka mmoja tu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimepoteza mapato karibu Dola za Kimarekani Milioni 2. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu namba tatu ya mradi huu wa Mlimani City, ni uwiano uliopo kati ya gawio la faida na rental income au kodi ya pango ambayo wanalipwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Yaani haya ni maajabu na yanaweza kutokea Tanzania tu. Ukiangalia mapato ambayo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeanza kulipwa kuanzia Mwaka 2006 mpaka Mwaka 2017, wamelipwa Dola za Kimarekani Milioni 7.5.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hawa Wabia, actually Mbia ni mmoja kwa sababu ana shares 99 na ile moja unaweza ukairudisha ni redeemable anytime unaweza ukai- redeem kurudi kwenye Kampuni. Kwa hiyo, Mbia ni mmoja, huyu Mbia ameweza kujilipa dividend au gawio la faida la 3.8 milion dollars. Hiyo ni nusu ya pesa iliyolipwa kwa Mlimani City kama Rental Income au Kodi ya Pango kwa miaka, kuanzia Mwaka 2006 mpaka leo; miaka 11. It’s can only happening in Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu namba nne, ya Mkataba huu wa Mlimani City na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni kukiukwa kwa masharti ya Mkataba kwa zaidi ya miaka 10 na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimekaa kimya. Kinachonishangaza ni kwamba hiki Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ndiyo kinazalisha Wanasheria wabobezi, wakiwepo baba yangu Profesa Kabudi, dada yangu Dkt. Tulia, lakini hawakuuona huu upungufu wote mkubwa uliopo kwenye mradi mpaka CAG alivyoenda kufanya Special Audit mwaka jana mwezi wa Nne na akaibua hiyo hoja na wao kuanzia mwezi wa Tano wakaanza kumwandikia mwekezaji kuwa anakiuka masharti. Hiyo ni ajabu namba nne. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu tano, Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba Makamu Mkuu wa Chuo kwa kipindi chote, tunajua nani walikuwa Makamu Mkuu wa Chuo miaka hiyo kuanzia Mkataba umesainiwa mpaka leo. Walikuwa ni sehemu ya bodi kwa maana ni Board Members, ukianza na Profesa Luhanga, Rwekaza Mkandala sasa hivi baada ya Rwekaza kuondoka ameingia Profesa mwingine wote hao ni Maprofesa. Profesa Muhanga, Profesa Mfinanga ameingia sasa hivi ndiyo Board Member amem-replace Mkandala, ana miezi kama miwili au mitatu, walikuwa wanaingia kwenye Bodi ya Mlimani City Holding. Kwa maana hiyo walikuwa ni sehemu ya maamuzi ya Mlimani City Holdings.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa huwa najiuliza, hivi hawa Maprofesa wetu, macho yao yalikuwa yameingia michanga au ni nini, mpaka wanaangalia haya maamuzi ambayo hayana tija kwa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu namba sita, ni going concern ya hii Kampuni ya Milimani City au kuendelea kuwepo kwenye kwa biashara kwa hii Kampuni kwa miezi 12 ijayo au mwaka mzima. Going concern au kuendelea kuwepo kwa biashara kwa Mlimani City Holding kunategemea na ipo kwenye ripoti, ipo kwenye financial statement za Mlimani City Holding, inategemea na uwezo wa shareholders kuendelea kuweka pesa. Willingness ya Shareholders kuweka pesa kwenye huo mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi mkubwa kama huu unategemea jinsi gani mwanahisa atajisikia kuweka pesa kwenye mradi. Kwa hiyo, akiamka hajisikii ina maana huo mradi utakufa, kwa hiyo, we are not sure hatuna uhakika wa kuwepo kwa hii Kampuni ya Mlimani City kwa miezi 12 ijayo hilo ni ajabu lingine la sita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu la saba na la mwisho, yapo mengi lakini nimechukua haya makuu ambayo naomba Serikali mkayafanyie kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajabu la saba, ni huyu mwekezaji ambaye ni Mbotswana, mwenye asili ya Kihindi anaishi Afrika Kusini. Mwekezaji huyu tangu ameanza huu mradi hajawahi kuonekana in physical. Sasa sijui ni mzimu au huyu mwekezaji sijui ni nini, yaani unawekeza pesa zote hizo, unakopesha almost 100 billion maana 49 milioni dollars ni zaidi ya bilioni 100, lakini huoni umuhimu wa kuja in physical kufanya negotiation unawatuma wawakilishi, hajawahi kuonekana. Hilo ni ajabu la saba, it can only happening in Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naona Serikali ya CCM ime-fail kusimamia miradi, tunaanzisha miradi mizuri lakini tunashindwa kusimamia. Imeshindwa kufanya oversight na monitoring na mwisho wa siku tumeishia kuvunja Mikataba na kupata hasara kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe Serikali badala ya tukishasaini tu mnaiacha Mikataba, mnaiacha hamuangalii implementation, ni bora tuache kusaini hii mikataba kuliko kuendelea kupoteza pesa za umma, pesa za walipa kodi maskini na kuacha pesa hizi zinapotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa pili ningependa kuchangia kuhusu Dege, mradi wa Dege Eco Village, mradi huu una utata mkubwa. Mradi wa Dege nilipata fursa ya kwenda kuangalia niliumwa tumbo la uzazi, kwa sababu ni Mwanachama wa NSSF nimekua nikichangia zaidi ya miaka 10, kwa hiyo, nina interest kwenye huo mradi wa Dege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu unautata kuanzia jinsi ulivyoanzishwa kwa maana jinsi gani ardhi ilipatikana mpaka implementation ya huo mradi. Tunaambiwa na Mkaguzi CAG anasema eka moja ilinunuliwa kwa milioni 800 Kigamboni. Sijui kwenye ile sehemu kuna gold, I don’t know labda hawa watu waende wakaangalie inawezekana kuna gold. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba sitaki kuongea maneno mengi naomba tu niishauri Serikali. Kwa vile mradi huu ni pesa za Wanachama wa NSSF na nikiwemo, naitaka Serikali na iazimie kwamba Mradi huu, pesa za NSSF zisiendelee kuingizwa kwenye mradi huu kwa sababu mpaka sasa hivi NSSF wameshaingiza bilioni 219 na ule mradi ni mfu mpaka itakapofanyika independent actuarial valuation, kuona kama pesa zilizoingizwa pale zina-reflect investment cost ya huu mradi sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke kwamba, kila siku gharama zinaongezeka lakini pia depreciation inatokea kwenye yale majengo na hizi gharama zitakuja kulipwa na Wanachama wenyewe.