Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru kwa namna ya pekee Mheshimiwa Selasini Mbunge wa Rombo, kunipa dakika chache nami niseme machache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza naunga mkono aliyoyasema kuhusu elimu sitaki kuyarudia ilikuwa niyasemee, lakini ni vizuri hiyo kauli ikatolewa ikaeleweka kwa sababu kama kuna kosa tutalifanya kama Taifa ni kuwafanya watoto wetu washinde kuanzia asubuhi mpaka jioni wasile chochote, kwa hiyo tunahitaji kauli ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine ni suala la asilimia 10 ya vijana na akinamama. Nashukuru Wizara ya TAMISEMI Naibu Mawaziri walifanya ziara katika Jimbo langu la Babati Mjini lakini mkatoa mwongozo, kwamba sasa asilimia mbili ni kwa walemavu, halafu zile asilimia nane zigawanywe kwa akinamama na vijana. Naiomba Serikali ni vizuri mkatenga asilimia zingine mbili kwa ajili ya wazee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna timu kubwa sana ya wazee ambayo hainufaiki na hizi asilimia 10. Kama mliona busara kutenga asilimia mbili kwa ajili ya walemavu, sasa niiombe Serikali au niitake Serikali ione hitaji la wazee la muda mrefu ambalo wamekuwa wakiiomba Serikali iwatengee angalau kiasi fulani kwa kila mwezi wapewe. Sasa hizi asilimia 10 ukiwapatia vijana, akinamama na walemavu na hawa wazee muwakumbuke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni vizuri watu wengine wanapofanya kazi nzuri waweze kukumbukwa katika Serikali hii. Naishukuru sana timu ya wataalam katika Halmashauri yetu ya Mji wa Babati na Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba kama kuna miongoni mwa Halmashauri zinafanya vizuri kuhusu asilimia 10 ni pamoja na Halmashauri ya Babati Mjini. Ni vizuri wakawa-promote wale wataalam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao wataalam ambao wanatusaidia zile fedha zinakuwa revolving fund, lakini Halmashauri zingine zile fedha zikiingia zinaingia kwenye consumption ya kawaida ya OC badala ya kurudi kwenye ule mfuko. Sisi kwa nini tumefanikiwa katika kutoa hiyo mikopo kwa asilimia 100 hiyo asilimia 10, ni kwa sababu tulikuwa na Mwanasheria mzuri sana, wale ambao hawalipi wanapelekwa Mahakamani, imesaidia watu kurejesha kwa sababu wanajua zile fedha lazima zirudi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukawa na timu ya Maendeleo ya Jamii pamoja na Mkuu wao wa Idara ambao zile fedha zikiingia wanaiweka kwenye account ambayo inakuwa revolving. Naomba vitu vingine hata kama vinafanywa na watu wengine ambao hamuwapendi sana kama ni vizuri basi mviige, njooni muone Babati tunafanya nini na tumefanikiwa kwa kiasi gani na nipongeze timu ya Babati Mkurugenzi na timu yake kwa sababu wanafanya kazi nzuri sana katika hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingine ninaotaka kuutoa ni kuhusu Pride Tanzania. Nimeona kwenye ripoti kwamba Kamati imeshauri Serikali iangalie kwa sababu hii Pride ilianzishwa kwa fedha za Serikali kipindi hicho. Naiomba Serikali pamoja na kwenda kuiangalia na kuibinafsisha irudi kwenye mfumo wa Serikali hii Micro Finance ni vizuri wale vijana wetu wasiathirike ajira yao na shirika likaendelea, kwa sababu kama kuna taasisi au kama Micro Finance ambayo imeajiri vijana wengi wa Kitanzania ni pamoja na Pride Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pamoja na kwamba huko nyuma mliuzianauziana kinyemela, lakini mwangalie pia ajira za Watanzania hata kama mnakwenda kuibinafsisha, lakini ni miongoni mwa Micro Finance ambazo zimetoa ajira nyingi kwa Watanzania na imefika katika vijiji na katika remote areas. Kwa hiyo, nitoe ushauri wangu kwamba msikimbilie kubinafsisha tu, sawa mtaangalia mtafanya audit ya kutosha, lakini mwisho wa siku muone jinsi gani ambavyo vijana wetu hawapotezi ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la OC, hebu niombe Serikali tunafanya bajeti, lakini bajeti hii hakuna sababu ya kukaa miezi mitatu au miwili hapa, tuka- budget fedha za maendeleo fedha za OC lakini mwisho wa siku Mheshimiwa Waziri wa Fedha, fedha zikawa haziji kabisa. Mmechukua vyanzo vikubwa vya Halmashauri zetu lakini hivyo vyanzo pia mvifanyie review, mfano nitoe chanzo kimojawapo, mmefuta ushuru wa machinjio katika machinjio zetu, pale Babati Mjini tumetengeneza machinjio mazuri, zaidi ya milioni 50 tumekarabati. Mmefuta ule ushuru at the same time mnamwachia Mkurugenzi alipe bili ya maji, bili ya umeme wakati kuna watu ambao wanachinja ng’ombe wao pale, mmefuta ule ushuru, angalieni…

(Hapa kengele ililia kuashiria muda wa mzunguzaji kwisha)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.