Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema zake kwa kuniwezesha kufika ndani ya ukumbi huu na nawashukuru wananchi wa Jimbo langu la Magu kunipa Ubunge ili niweze kuwatumikia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naipongeza hotuba ya Mheshimiwa Rais, kwa kadri ambavyo imejikita kuonesha kwamba Watanzania wana mahitaji. Imegusa mahitaji ya kila Mtanzania lakini pia imeonesha huruma kwa Watanzania, naipongeza sana. (Makofi)
Sisi Watanzania tumepata kiongozi. Vitabu Vitakatifu vimeandika, ukisoma 2 Timotheo 2:20, unasema; “Nyumbani mwa Bwana kuna vyombo vingi, viko vyombo vya dhababu, vipo vyombo vya miti.” Mheshimiwa John Pombe Magufuli ndicho chombo cha dhahabu ambacho Mwenyezi Mungu Watanzania ametuandalia. Naomba tumuunge mkono wakati wote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na maji. Jimbo langu la Magu lina matatizo makubwa sana ya maji kama zilivyo wilaya zingine. Sisi wenye nguvu ukirusha jiwe linakwenda moja kwa moja ndani ya maji lakini Wilaya ya Magu haina maji. Tumeahidiwa na viongozi waliopita, Rais wa Awamu ya Tatu, Rais wa Awamu ya Nne mpaka leo Magu haina maji. Bahati nzuri Mheshimiwa John Pombe Magufuli wakati wa kampeni naye ameahidi.
Mimi sina shaka kwa sababu hotuba hii amezungumzia sana suala la maji na sina shaka kwa sababu Waziri wa Fedha ni type ileile ya Mheshimiwa Profesa Muhongo kwamba hataki ubabaishaji kwenye makusanyo ya fedha, nampongeza sana. Ili miradi hii itekelezeke lazima fedha zikusanywe na nawaomba wakaze kamba wasilegeze hata siku moja kwa sababu nchi hii ilikuwa imefikia pabaya sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, unajua asali ni tamu sana lakini wako watu ambao hawanywi asali lakini kila mmoja anakunywa maji. Hebu tuangalie sasa suala hili, Serikali ifanye kila linalowezekana hata kukopa Benki ya Dunia ili kuweza kutekeleza miradi ya maji iliyoko kwenye nchi hii hasa Wilaya ya Magu. Wilaya yangu vijiji vingi havina maji na Wanamagu wana uvumilivu ukubwa sana na hili ndilo lililonileta Bungeni kwamba maji ndilo hitaji la wananchi wa Magu. Ili nirudi tena hapa Bungeni 2020 lazima maji yapatikane. Waziri wa Maji, Waziri wa Fedha, nisaidie hili ili Mheshimiwa Rais aliposema kwamba tumwachie jambo hili la maji Magu litekelezeke kweli kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, upo mradi ambao umeanza upembuzi yakinifu leo ni miaka miwili watu wanachakata, wanachakatia wapi? Mheshimiwa Rais alisema hawa watu wanaochakata watachakatia nje, Mtaalamu Mshauri anachukua miaka miwili anafanya upembuzi yanikinifu bila kukamilisha, hii ni kweli? Hii Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Pombe Magufuli ya „Hapa Kazi Tu‟ imwangalie huyu Mtaalamu Mshauri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la elimu bure Serikali imeanza vizuri. Mpango wa capitation ulikuwepo tangu mwaka 2002 lakini naomba niishauri Serikali kwamba wakati inatoa dola 10 kwa kila mtoto…
NAIBU SPIKA: Naomba umalizie Mheshimiwa.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Exchange rate ilikuwa ni Sh1,000 leo ni Sh.2,200. Kwa hiyo, waangalie hali ilivyo sasa ili kumudu uendeshaji wa shule hizi ili ziweze kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga hoja lakini nina mambo mengi ya kuzungumza, kumbe ningeanzia mchana, basi niishie hapo.