Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi nami niweze kuchangia katika hoja zilizoletwa na Kamati hizi mbili. Napenda nizipongeze kwa taarifa nzuri za Kamati zote hizi mbili. Kwa kuanza naomba nijikite katika taarifa ya hesabu za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yetu ilijikita kufanya mahojiano na Halmashauri pamoja na kutembelea miradi ya maendeleo. Katika kufanya mahojiano na Halmashauri, hoja nyingi zilizojitokeza ni Halmashauri kutokujibu hoja za ukaguzi hususani katika hoja za miaka ya nyuma. Halmashauri zinafanya uzembe na mazingira yanaonesha kwamba hawataki kujibu hoja hizo kwa sababu siyo sehemu ya ku- form opinion. Nitoe ushauri kwa Serikali kuchukua hatua ya ziada ili hoja hizo ziweze kupatiwa majibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkaguzi wa Hesabu aliendelea kuibua hoja za ukaguzi ambazo nyingi zilisababishwa na upungufu uliopo katika kutumia mfumo wa kihasibu wa EPICAR. Kama Serikali haitachukua hatua ya ziada kuweza kutatua tatizo katika mfumo wa hesabu (EPICAR version 9.05) hoja nyingi zitaendelea kuibuliwa kutokana na mapungufu yaliyopo katika mfumo wa kihasibu wa EPICAR.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo huu ulianza Julai 2012 leo ni miaka sita mfumo hauna asset modal ambayo inasababisha madeni kutokuripotiwa katika hesabu za mwisho ama Mkurugenzi kuamua kufunga hesabu kwa namna anavyotaka zionekane mwenyewe. Haina ubishi kwamba Mkurugenzi inamlazimu aichukue trial balance afanye export akafanye kwenye excel. Kwa hiyo, hii moja kwa moja anaweza akafanya udanganyifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfumo huu unatumia cash basis na tunajua Halmashauri zinatakiwa zifungwe hesabu kwa matakwa ya IPSAS na full adoption ya IPSAS kwa Tanzania katika Halmashauri ilikuwa ni mwaka 2013 lakini mpaka sasa hivi mfumo huu hauna accrual basis. Halmashauri zimeendelea kuandika LPO nje ya mfumo kwa sababu mfumo hau-support accrual basis.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama una-support cash basis ni changamoto kwa Halmashauri kununua vifaa kwa kutumia cash. Ni dhahiri kwamba siyo muda wote Halmashauri itakuwa na fedha taslimu. Kwa hiyo, inazilazimu Halmashauri ziandike LPO nje ya mfumo na hivyo kujikuta madeni mengine hayatolewi ripoti katika hesabu za mwisho. Kwa hiyo, ile hoja ya kulipa madeni ambayo hayakuwa kwenye hesabu za Halmashauri, hoja hii itaendelea kuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ilifanya ziara katika Mkoa wa Tanga na mikoa mingine, naomba nijikite katika hoja kubwa ambayo ilijitokeza katika miradi, hoja ya upungufu katika miradi ya maji. Tunao mradi wa RWSSP ambao unatekeleza miradi ya maji vijijini. Changamoto mojawapo iliyopo kwanza katika RWSSP kuna component ya sanitation lakini component hiyo imekuwa haifanyiwi kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeenda kukagua miradi ya Tanga ya maji, sikuwahi kuona mahali popote kwamba kuna miradi ya usafi wa mazingira. Tulienda Iringa kukagua miradi, miradi mingine ya maji imekamilika lakini ile component ya sanitation fedha zake amepewa Mkandarasi lakini miradi haijatekelezwa. Kwa hiyo, Serikali pia iangalie kipengele cha sanitation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi iliyokamilika ina jukumu…

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Leah Komanya...

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.