Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia hizi Kamati mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kusema kwamba mwanadamu ameumbwa kufikiria mambo mengi sana kila baada ya dakika moja na fikra hizi anaziwekea mipango matakwa na haraka anaweza akaamua kutekeleza. Sisi Wabunge tena ambao hatuzidi hata 400 tuna kazi ya digest fikra za Watanzania zaidi ya milioni hamsini kuziwekea mipango, bajeti na kusimamia Serikali katika utekelezaji na tunaisimamia Serikali humu Bungeni pia tunaisimamia Serikali tukiwa katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya Wizara ya Maji baada ya bajeti ni kutoa miongozo ya utekelezaji wa miradi ya maji kwenye Halmashauri. Moja ya miongozo ambayo imetolewa ni kwamba Serikali haiwezi kupeleka fedha katika Halmashauri lazima kwanza kazi zitekelezwe, kazi ifanyike katika viwango vinavyotakiwa. Kama kazi yetu sisi Wabunge basi ni kusimamia utekelezaji katika Halmashauri, kama kazi yetu tungeitekeleza vizuri kwenye Halmashauri hata hoja za kuisimamia Serikali ndani ya Bunge kwa vyovyote vile zingepungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimelizungumza hili kwa sababu nazunguka katika Halmashauri mbalimbali, nakutana na changamoto nyingi kama ambavyo zimeainishwa na CAG katika taarifa zake. Waheshimiwa Wabunge wametoa michango,

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lubeleje amezungumzia visima vimechimbwa sita tangu mwaka 2002 lakini havijawekewa pampu. Miongozo ipo nimpongeze sana Mheshimiwa Lubeleje ni kweli amekuwa kila wakati nikikutana naye ananiomba niende kwenye Jimbo lake nikaangalie hali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Mheshimiwa Gerson Lwenge akiwa Waziri aliwahi kwenda kule lakini juzi nimemtuma Naibu Waziri wangu na nimwahidi Mheshimiwa Lubeleje baada ya Bunge nitaenda nae tena kule, nimeshatoa miongozo kwamba kama umechimba kisima na maji yapo tengeneza quotation, lete tukupe fedha ili uweze kununua hiyo pampu ili wananchi wapate maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bobali nikushukuru umeongea vizuri miradi mingi inakamilika bila kuwa na viwango vya thamani ya fedha inayotakiwa. Kama nilivyosema wasimamiaji ni sisi wenyewe kwenye Halmashauri. Sisi ndiyo tunaosimamia Serikali Bungeni na tunasimamia Serikali kwenye Halmashauri. Sheria tumezitunga wenyewe inabidi tuzisimamie na Serikali yetu kwa sasa wenyewe ni mashahidi mtu akifanya ufisadi ni moja kwa moja hatua zinachukuliwa hapohapo. Hili halina mashaka kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Abdallah Chikota umetoa mfano wa mradi wa Korogwe kwa Mheshimiwa Maji marefu ule mradi ulisanifiwa ukaanza kutekelezwa hadi maeneo ya Mlembule lakini ikaja kuonekana kwamba mradi ule unatoa maji kutoka Vuga, watu wa Vuga hawakupewa yale maji, tulipokuja ku-review ule mradi wataalam wetu waliweka hela nyingi sasa hivi tunarudia tena ili uweze kutekelezwa. Ninachoomba tu Waheshimiwa Wabunge tusaidiane katika maeneo yetu ili mambo yaweze kwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wamezungumzia mtiririko wa fedha kama nilivyozungumza, kwanza niwashukuru sana kuweka Mfuko wa Maji. Mfuko wa Maji kila mwezi unatoa fedha hadi Desemba katika bajeti iliyopangwa ya bilioni 158 tayari Hazina imeshatoa bilioni themanini na kila mwezi kila anayezalisha certificate tunamlipa. Kwa hiyo, suala la mtiririko wa fedha ili uwe mzuri ni sisi Waheshimiwa Madiwani maana yake Wabunge lakini tukirudi kwenye Halmashauri tunakuwa Madiwani, tusimamie utekelezaji wa miradi wazalishe walete hati ili tuweze kulipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwalongo ni kweli nilitembelea Njombe. Hii miradi yote aliyoizungumza Utengule na Changalikwa tuliitembelea, tukakuta changamoto utekelezaji haukuwa mzuri, tayari tumeunda Tume iende ikachunguze na kitu chochote kitakachopatikana ambacho ni kibaya, basi sheria itachukua mkondo wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ni dakika tano nimeweka mambo kidogo, nilikuwa na mambo mengi nafikiri haya yanatosheleza. Nakushukuru sana.