Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nami nichukue fursa hii kuchangia katika Kamati hizi tatu muhimu sana. Moja naomba wakati ujao ikiwezekana kwa baadhi ya hizi Kamati zingepewa umuhimu siku zingeongezwa ili watu wengi zaidi waweze kuchangia. Ni muhimu kwa kuleta tija ili Serikali iweze kupata mafanikio makubwa sana na wapate mawazo ya Wabunge wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja naomba niishauri Serikali; tumeanza vizuri sana, ndoto ya kuwa na nchi ya viwanda na inawezekana, lakini naomba kabisa Serikali itathmini upya, tuangalie mahali ambapo gharama za uzalishaji. Tusipoweza kuangalia gharama za uzalishaji kwa ajili ya tozo, kodi na ushuru mbalimbali ambao unatozwa na taasisi za udhibiti na taasisi mbalimbali ili mtu aweze kuzalisha hatutaweza kufikia hayo malengo; kwa sababu hatimaye mfanyabiashara anachohitaji ni faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama bidhaa nyingi zinazoagizwa kutoka nje ya nchi na hasa kwa mfano kwenye Afrika Mashariki au SADC ambazo zinaingia bila kodi, halafu huku ndani ya nchi unakuwa na utitiri wa kodi na tozo mbalimbali, ndoto hiyo hatutaifikia. Tuna hizi taasisi za udhibiti ziko nyingi sana lakini pia ushuru na kodi mbalimbali ambayo inafanya bidhaa zetu za Tanzania zisiweze kushindana kutokana na gharama kubwa ya uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano mmoja tu net ambazo zinazalishwa hapa ni kiwanda kikubwa kuliko chochote cha Afrika A to Z. Pia mbolea tunayoizalisha ndani ya nchi unakuta kodi mbalimbali ambayo ile import tax wanatozwa hawaruhusiwi ku-claim back lakini neti ikitoka nje ya nchi au mbolea ikitoka nje ya nchi haina kodi. Sasa viwanda vyetu tunavilinda au ndio tunavimaliza? (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, naomba Serikali iangalie suala hili kwa mapana zaidi na tuwe na one stop center. Kwamba mtu akija akitaka kukata leseni ya biashara yoyote akishakata hapo basi gharama na tozo zote kila kitu viwe hapo hapo ili baadaye pasiwe na kurudi nyuma, kwamba tunadaiwa, leo umekata leseni umeanza biashara, baada ya miaka mitatu anakuja mtu wa OSHA, anakuja NEMC, hizo zote zinakuwa ni kero. Natakiwa nikishalipia hapa; si kila mtu anajua sheria zote na kwenye sheria wansema kutokujua sheria sio kinga, lakini sio wananchi wote watajua hizo sheria, ni vizuri tuwe na one stop center kama TIC iwe ngazi ya mkoa, ngazi ya wilaya mtu akishalipa wagawane.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine la muhimu ni Serikali kuwa na e-government na malipo yote yaendelee kufanyika kwa kupitia hiyo hiyo TRA lakini wabadilishe mfumo. Kwa mfano kodi hii ambayo tumekubaliana ya majengo na kodi ya mabango hayo yote mtu akishalipia pale basi risiti ikitoka na halmashauri yangu iwe inajua kwamba mtu fulani amelipa kiasi fulani na mgao wa Serikali kuu ni kiasi fulani, mgao wa halmashauri yangu ni kiasi fulani na mgao ambao unatakiwa kwenda mpaka ngazi ya chini ni kiasi gani. Kila mmoja akijua hiyo tutawezakufanikiwa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sehemu nyingine kubwa ni kuwekeza kwenye utafiti. Sisi tunaimba tu pesa zote za utafiti asilimia kubwa zaidi ya asilimia 99.8 zinatoka nje ya nchi, za kwetu za ndani hakuna. Ilikuwa tumekubaliana 1% ya total budget imeshindikana, tumekuja thirty billion imeshindikana. Bila utafiti hatutaweza kusonga mbele, hivyo ni vizuri tuwekeze kwenye utafiti hasa kwenye sekta ya kilimo, madini kote huko hata kwenye biashara inataka tuwe na fedha za kutosha za utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia Tume ya Ushindani (FCC) pia iweze kufanya kazi yake vizuri iangalie mambo haya yote lakini mbali na hilo iharakishe lile suala la CETAWICO ambayo inazalisha mvinyo hapa Dodoma iweze kuchukuliwa na breweries ili wakulima wa zabibu hapa Dodoma waweze kunufaika na Watanzania tunywe mvinyo ambao unatoka Tanzania, si huu wa sasa hivi ambao asilimia kubwa unatoka South Africa na sawa na juices nyingi ambazo tunanunua concentrates kutoka nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie kwamba bidhaa zote ambazo tunaweza kuzalisha ndani ya nchi tuwe na muda maalum; kwamba ndani ya miaka miwili au mitatu tutakuwa tunazalisha hapa nchini ikiwa ni pamoja na hizo juice concentrates, mafuta ya kupikia, kwa sababu baada ya bili kubwa ya mafuta ya magari au mafuta ya dizeli ya pili inayofuata kwa gharama kubwa tunayoagiza ni mafuta ya kula ambayo ni vegetable oil tunayoagiza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni sukari; na haya mambo yote tunaweza kuzalisha hapa nchini kwa gharama nzuri, wakulima wetu wakanufaika na pesa zote hizo zikabaki ndani ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine nizungumzie suala la budget cycle. Ni muhimu sana sisi tuangalie kubalisha budget cycle kama Bunge kwa sababu kipindi tunakaa Kamati ya Bajeti na Kamati zingine zote kupitia hizi bajeti hakuna mabadiliko tunayoweza kuleta zaidi ya asilimia moja au mbili. Tungekaa sisi kuanzia Agosti, Oktoba ili kama kuna inputs zote, mawazo yote yaingizwe ili halmashauri zetu na taasisi zote zinapokwenda kupanga bajeti zao basi wajue hii itapanda, itashuka au haitakuwepo; hiyo itatusaidia sisi wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kwamba tuangalie kwenye sekta ambayo ni rasmi na ambayo isiyo rasmi (formal and informal sector). Hii informal sector yaani sekta isiyo rasmi inazidi kukua kutokana na haya masuala ya kodi, tozo na usumbufu mbalimbali. Ingekuwa tumeweka viwango maalum na mtu anajua akishakuja kulipa sehemu moja hatasumbuliwa tena kila mtu atapenda kuwa formal. Pia kila mtu atapenda kwamba mambo yake yaendelee vizuri, lakini yule ambaye hatakiwi kuwa na rekodi yeyote unakuta ana unafuu sana kuliko yule ambaye anaweka record ndiye anayekamuliwa mpaka dakika ya mwisho. Kwa hiyo naomba na hilo pia lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwenye masuala ya madini kuna mengi ambayo tumezungumza kwenye Kamati kama tulivyokuwa tunasema kwamba, ni vizuri kodi nyingi ambazo ziko ni vizuri tupate muda wa kutosha ili tuweze kutoa mawazo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine muhimu ni suala la kulinda ardhi yetu. Nina uhakika kwa kazi nzuri sana ambayo anafanya Mheshimiwa Waziri wa Ardhi ambaye ameondoa kero nyingi pia atatusaidia kuhakikisha ardhi za kilimo zinalindwa. Tukiwa hapa Makao Makuu yetu ya Dodoma, nina uhakika atalinda mashamba yote ya zabibu yasibadilishwe kuwa makazi na utakuwa mfano kama nchi zingine unakuwa na mashamba ndani ya mji, inakuwa ni green belt. Mheshimiwa Waziri najua hicho kitu anakiweza na nina uhakika kwamba hiyo kazi tutafanikiwa vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kupanua wigo wa kodi, tusipopanua wigo wetu wa kodi hatuta…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)